Katika suala zima la ufugaji kuna kanuni na taratibu za kufuata kutoka na mabadiliko mbalimbali ya hali ya hewa. Msimu wa kiangazi na msimu wa masika ni muhimu kuifuatilia ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza. Katika makala hii Mkulima Mbunifu inakuangazia mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa msimu wa jua na wakati wa msimu wa mvua ili kufanikisha ufugaji wako. Msimu…
Mifugo
Chanja kuku kuepuka magonjwa yanayoambatana na mvua
Wafugaji wamekua wakijisahau juu ya umuhimu wa chanjo kwa mifugo, Katika msimu wa mvua za masika, mifugo mingi imekua ikiathirika kutokana na magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bacteria pia virus. Wafugaji wa kuku haswa wakienyeji, wameishia kupoteza mifugo yao kutokana na kutozingatia chanjo. Mara nyingi mvua hizi huambatana na magonjwa mengi kwa kuku kama vile gumboro, ndui ya kuku, kideri, kipindupindu…
Taarifa muhimu kuhusu ufugaji wa mbuzi
Mbuzi na kondoo ni wanyama ambao wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu pia ni wavumilivu wa ukame na maradhi tofauti na ngo’mbe kwa kua wana umbile dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na nguvu kazi ndogo na hata kwa wenye kipato kidogo. Katika makala hii Mkulima Mbunifu inangazia kuhusu ufugaji wa Mbuzi. Makala kama hii inaweza kua umeshasoma, ila kwaajili maombi…
Namna ya kuanza kilimo hai
Kumekua na maswali kadhaa juu ya kuanzisha kilimo hai. Yamkini, wewe pia unajiuliza swali hili, vile unavyoweza kuzalisha kwa mfumo wa kilimo hai shambani mwako. Jarida la Mkulima Mbunifu ni mahususi kwa ajili yako na katika makala hii tunakukumbusha tena. Kama una nia thabiti ya kuanzisha kilimo hai, fuata hatua zifuatazo; Angalia uwezekano wa kupata soko kwanza Jiulize mwenyewe: Ni…
Changamoto katika kilimo na ufugaji msimu wa mvua
Kilimo katika msimu wa mvua Huu ni msimu wa mvua katika maeneo mengi nchini. Bila shaka wengi wetu ni wakulima na wafugaji hivyo bado tunaendelea na shughuli zetu za kila siku. Je, ni changamoto zipi unazopitia katika msimu huu wa mvua kwenye shughuli zako za kila siku za kilimo? Tushirikishe/tueleze ili tuweze kupeana ushauri nini chakufanya Tuma ujumbe wako hapa…
Ufugaji wa samaki kibiashara ni njia rahisi yakuongeza kipato
Kumekuwa na mfumko wa watu wengi mijini na vijijini kuingia katika ufugaji wa samaki. Miradi hii huwagharimu fedha nyingi, lakini hufa baada ya muda mfupi. Ili mfugaji aweze kuwa na ufugaji wenye tija, hana budi kujifunza ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa ambao hufanyika kwenye mabwawa ya kuchimbwa au visima na vifaa vingine vinavofanana na hivyo, vyenye uwezo wa…
Tahadhari za kuchukua nyakati za msimu wa mvua katika ufugaji samaki
Ufugaji wa samaki una kanuni na taratibu za kufuata ili kuendana na mabadiliko ya hali ya hewa. Msimu wa masika ni muhimu kuufuatilia ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza. Katika makala hii Mkulima Mbunifu linakuangazia hatua muhimu za kuzingatia wakati wa masika ili kufanya ufugaji samaki wenye tija. Nyakati za msimu wa mvua ni vema kuzingatia hatua zifuatazo ili kuepuka madhara…
Fahamu mikakati rahisi inayoweza kutumika ili kupanua mradi wa ufugaji wa kuku
Ufugaji wa kuku unaweza kumpa mkulima kipato kikubwa. Hii inawezekana ikiwa mfugaji mdogo wa kuku atapanua kiwango na idadi ya kuku anaowafuga. Kuku ni ndege maarufu na anayefugwa sana nchini Tanzania. Karibu kaya nyingi zinafuga kuku, kwa ajili ya nyama yake yenye ladha nzuri, mayai, pia ni ishara muhimu ya kitamaduni katika baadhi ya jamii. Kwa nini ni vigumu kuongeza kipato…
Ulishaji wa majani makavu: Usisahau maji
Kabla ya kulisha wanyama majani makavu ni muhimu sana kufahamu ni kwa namna gani yanahitajika kulisha kwani majani haya ni tofauti na majani mabichi. Kiwango cha majani makavu kiwe kidogo zaidi ya majani mabichi. Robota moja la kilo 15 la majani makavu ni sawa na kilo 75 za majani mabichi, na yanaweza kulishwa kwa ng’ombe anaetoa maziwa vizuri mara moja…
Fuata kanuni sahihi za kilimo upate mavuno bora
Wakulima walio wengi wamekuwa wakijikita zaidi katika matumizi ya mbolea ili kupata matokeo mazuri katika kilimo, na kusahau kuwa kanuni bora za uzalishaji pia huchangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka na kupatikana kwa mavuno yenye ubora. Nini cha kuzingatia ili kupata mavuno bora Ni lazima mkulima kufuata utaratibu wa uzalishaji wa mazao katika kila msimu wa kilimo. Hatua zifuatazo ni lazima…