Ni muhimu kwa mkulima kuhakikisha anauilisha udongo kwa kutumia virutubisho vya asili, ili kuweza kuwa na rutuba na kuzalisha mazao yenye tija. Rutuba ya udongo inafafanuliwa kwa uwezo wake wa kutoa virutubisho vyote muhimu. Hii ni kwa kiasi kinachotosheleza na katika urari sahihi kwa ajili ya ukuaji wa mimea, bila ya kutegemea matumizi ya moja kwa moja ya virutubisho. Vipengele…
Binadamu
Tukumbushane namna ya kuhifadhi malighafi na chakula cha samaki
Bamia ni zao linalolimwa sana nchi za joto. Zao hili hutumika kama mboga inayoliwa matunda.
Je, Una swali lolote kuhusiana na ufugaji wa Samaki? Tuulize, Tukujibu
Ni utaratibu wa kawaida kabisa kwa MkM kuthamini maoni yako na kujibu maswali yenu kwa kupitia wataalamu wa kada mbalimbali. Katika toleo hili Musa Said ambaye ni mtaalamu wa Samaki anaendelea kujibu maswali kuhusiana na ufugaji wa samaki. Shime, kama nawe una maswali basi usisite ili upate jibu na uondokane na dukuduku. Lai otieno anauliza: Mimi natoka Musoma mjini na…
Lishe na vyanzo asili ya chakula
Lishe bora inajumuisha aina mbalimbali za vyakula kutoka makundi tofauti ya chakula, na hutoa virutubisho na ladha tofauti. Makundi haya ni muhimu kwa afya na ukuaji wa mwili: Nafaka na mizizi: Mahindi, viazi, ndizi — hutoa wanga kwa ajili ya kuongeza nguvu. Mikunde: Maharagwe, soya — chanzo cha protini kwa ajili ya kujenga mwili. Karanga na mbegu: Njugu, korosho —…
Mifano ya ujumuishaji yanayotumiwa na wakulima
1. Mifumo Mseto Wakulima wanalima mazao makuu pamoja na kufuga ng’ombe, wakitumia mabaki ya mazao kulisha ng’ombe na samadi kurutubisha mashamba. 2. Kilimo cha mzunguko na malisho ya muda Mzunguko wa mazao na malisho ya muda mfupi ambayo huliwa na mifugo. Awamu ya malisho inaboresha rutuba ya udongo kwa mazao yanayofuata, na mifugo hunufaika na malisho. 3. Malisho kwenye bustani…
Je, wajua kuwa unaweza kufanya ufugaji mesto wa Samaki, kuku na mboga katika eneo dogo, kwa gharama nafuu na kipato kikubwa?
Ufugaji wa samaki umeendelea kukua hata katika maeneo ambayo hakuna ziwa, bahari, bwana na kusaidia jamii kujipatia kipato kinachokidhi mahitaji muhimu, na hata kufanya maendeleo binafsi. Mafanikio ya ufugaji wa Samaki ni kutokana na uhakika mkubwa wa soko. Katika Makala hii Mkulima Mbunifu inakuletea Ufugaji mesto wa Kuku, Samaki na uzalishaji wa mboga katika mbinu rahisi. Ufugaji wa mesto ni…
Je, wajua kuwa unaweza kulima mboga kwenye matairi na ukafanikiwa?
Hupunguza uchafuzi wa mazingira Kila siku watumiaji wa vyombo vya usafiri hubadilisha matairi. Mbali na kuwa matairi hutumika kutengeneza vitu kama viatu, mipini ya mapanga n.k, pia matairi yanaweza kutumiwa katika kilimo cha mbogamboga na matunda badala ya kuchoma matairi na kuzalisha kemikali zenye sumu kwa binadamu. Ni rahisi kutumia Ukilinganisha na kulima kwa kutengeneza matuta ya mbao au mawe,…
MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE; TUAMBIE UMEJIFUNZA NINI? JE, UNAKWAMA WAPI?
Kama umeweza kuhudhuria maonyesho ya wakulima Nanenane katika kanda yeyote, njoo utuambie ni kipi umejifunza kipya, au ni maarifa ama ujuzi gani umeongeza? Je, ni wapi unakwama au changamoto uliyonayo ni ipi? Njoo tusemezane ewe mkulima!!!!!!!!!!!!!
Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai
Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo. Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja…
HIVI UKISIKIA WAKULIMA WAKISEMA MBEGU UNAFIKIRIJE? AMA KWA UFAHAMU WAKO MBEGU NI NINI
Mbegu ni nini? Mbegu ni sehemu ya mmea ambayo ina uwezo wa kuota na kutoa mmea mpya. Kuna makundi makuu mawili ya mbegu tunayoyazungumzia katika kilimo ambayo ni punje na shina/ mizizi. Punje Hizi ni mbegu za nafaka au za matunda, ambazo huzalishwa kwa uchavushaji. Kawaida huwa na kiini na chakula chake huhifadhiwa ndani ya ganda gumu la mbegu. Mfano,…









