1. Mifumo Mseto Wakulima wanalima mazao makuu pamoja na kufuga ng’ombe, wakitumia mabaki ya mazao kulisha ng’ombe na samadi kurutubisha mashamba. 2. Kilimo cha mzunguko na malisho ya muda Mzunguko wa mazao na malisho ya muda mfupi ambayo huliwa na mifugo. Awamu ya malisho inaboresha rutuba ya udongo kwa mazao yanayofuata, na mifugo hunufaika na malisho. 3. Malisho kwenye bustani…
Binadamu
Je, wajua kuwa unaweza kufanya ufugaji mesto wa Samaki, kuku na mboga katika eneo dogo, kwa gharama nafuu na kipato kikubwa?
Ufugaji wa samaki umeendelea kukua hata katika maeneo ambayo hakuna ziwa, bahari, bwana na kusaidia jamii kujipatia kipato kinachokidhi mahitaji muhimu, na hata kufanya maendeleo binafsi. Mafanikio ya ufugaji wa Samaki ni kutokana na uhakika mkubwa wa soko. Katika Makala hii Mkulima Mbunifu inakuletea Ufugaji mesto wa Kuku, Samaki na uzalishaji wa mboga katika mbinu rahisi. Ufugaji wa mesto ni…
Je, wajua kuwa unaweza kulima mboga kwenye matairi na ukafanikiwa?
Hupunguza uchafuzi wa mazingira Kila siku watumiaji wa vyombo vya usafiri hubadilisha matairi. Mbali na kuwa matairi hutumika kutengeneza vitu kama viatu, mipini ya mapanga n.k, pia matairi yanaweza kutumiwa katika kilimo cha mbogamboga na matunda badala ya kuchoma matairi na kuzalisha kemikali zenye sumu kwa binadamu. Ni rahisi kutumia Ukilinganisha na kulima kwa kutengeneza matuta ya mbao au mawe,…
MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE; TUAMBIE UMEJIFUNZA NINI? JE, UNAKWAMA WAPI?
Kama umeweza kuhudhuria maonyesho ya wakulima Nanenane katika kanda yeyote, njoo utuambie ni kipi umejifunza kipya, au ni maarifa ama ujuzi gani umeongeza? Je, ni wapi unakwama au changamoto uliyonayo ni ipi? Njoo tusemezane ewe mkulima!!!!!!!!!!!!!
Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai
Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo. Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja…
HIVI UKISIKIA WAKULIMA WAKISEMA MBEGU UNAFIKIRIJE? AMA KWA UFAHAMU WAKO MBEGU NI NINI
Mbegu ni nini? Mbegu ni sehemu ya mmea ambayo ina uwezo wa kuota na kutoa mmea mpya. Kuna makundi makuu mawili ya mbegu tunayoyazungumzia katika kilimo ambayo ni punje na shina/ mizizi. Punje Hizi ni mbegu za nafaka au za matunda, ambazo huzalishwa kwa uchavushaji. Kawaida huwa na kiini na chakula chake huhifadhiwa ndani ya ganda gumu la mbegu. Mfano,…
MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE, EWE MKULIMA, MFUGAJI NA MJASIRIAMALI VIPI UMEJIANDAAJE?
“Hayawi hayawi sasa yamekuwa”. Kama ilivyo ada mwezi wa nane, huwa ni mwezi wenye shughuli nyingi zinazohusiana na kilimo, ufugaji, uvuvi wasindikaji na hata kilimo biashara tangu mwanzoni kabisa mwa mwezi hadi katikati ya mwezi. Wakulima, wafugaji na wadau wengine hupata fursa ya kukutana katika maeneo mbalilmbali ili kuonesha kazi zao pamoja na kushirikishana uzoefu katika suala zima la kilimo…
Wakulima vinara wa MkM ni mabalozi wa kilimo endelevu
Nchini Tanzania, kilimo si kazi tu, ni sehemu ya maisha ya kila siku. Kilimo kinatoa ajira kwa takribani asilimia 80 ya Watanzania na kuchangia takribani asilimia 30 ya pato la taifa. Kiasi kikubwa cha chakula chetu kinazalishwa na wakulima wadogo. Hata hivyo, licha ya mchango wao mkubwa, wakulima hawa hukumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na udongo kupoteza rutuba,…
Tengeneza unga wa mbegu za parachichi na tumia kwa afya
Unga wa mbegu za parachichi Parachichi ni moja ya matunda maarufu duniani kote. Tunda hili hutumika kwa shughuli mbalimbali, kama vile kuliwa kama tunda, utengenezaji wa mafuta ya kula, vipodozi, n.k. Pia, matawi ya mparachichi yanaweza kutumika kama malisho kwa mifugo, huku mti wake ukitumika kama kuni au hata magogo ya kujengea. Hivi karibuni imegundulika kuwa mbegu za parachichi zina…
Namna ya kutengeneza unga wa maboga
Katika jamii yetu, watu huchukulia kuwa boga ni chakula cha watu masikini ambao hawana namna ya kupata chakula kizuri. Hata badhi ya wakulima hawakubali kujiingiza katika kilimo cha zao hili. Ukweli ni kwamba, hili ni zao ambalo lina manufaa makubwa sana hasa kwa afya ya binadamu. Hii ni kwa sabababu tunda la boga lina kiasi kikubwa cha kalishamu. Boga ni…






