Mifugo

- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara, Kutuhusu, Mazingira, Mifugo, Mimea, Redio, Usindikaji

Miaka 10 ya huduma kwa wakulima wadogo

Maoni kutoka kwa wakulima yanaonyesha kuwa wakulima wadogo wana hamu ya kujifunza njia mpya na endelevu za kilimo ambazo zinaboresha mapato yao. Inaonyesha kwamba wanatambua na kuthamini mchango wa MkM katika kuendeleza na kupanua kilimo biashara na kutunza mazingira. Tangu kuanzishwa kwa jarida hili mnamo Julai 2011, Mkulima Mbunifu, maarufu kwa wakulima kama MkM limejikita katika kuwaelimisha wakulima kuthamini msingi…

Soma Zaidi

- Mifugo

Ufugaji holela wa kuku haufai na ni hatari

Nimekuwa mfugaji wa kuku kwa kipindi cha miaka mingi sana, tatizo ni kwamba kuku wangu hawana banda maalumu na hukutana nao jioni tu wanapoingia jikoni, na kutoka asubuhi, nimesoma kidogo kwa jirani yangu aliekuwa na Mkulima mbunifu juu ya ufugaji wenye tija, je nikianza haitanigharimu sana kwa kuwa wao hujitafutia chakula wenyewe?-Haule, Iringa. Kuku kama ilivyo kwa mifugo wengine, wanahitaji…

Soma Zaidi

- Mifugo

Fahamu ugonjwa wa ukurutu na namna ya kuudhibiti

  Ukurutu ni ugonjwa wa ngozi ambao huambukizwa kwa njia ya kugusana kati ya mnyama aliyeathiriwa na aliye mzima. Kitaalamu ugonjwa huu hujulikana kwa jina la menji (Mange) na husababishwa na utitiri ambao kitaalamu wanaitwa mange mites. Wadudu hawa hujikita kwenye ngozi na kufanya ngozi kuwa ngumu kama yenye magaga, kumfanya mnyama kuwashwa na mwisho manyoya kupukutika na kuondoka kabisa.…

Soma Zaidi

- Mifugo

Usafi hukinga mifugo dhidi ya ugonjwa wa ngozi

Wafugaji walio wengi, hudhania kuwa wanyama hawana hadhi ya kufanyiwa usafi au kuwekwa katika mazingira safi kama ilivyo kwa binadamu. Hata kama viwango hutofautiana, lakini ifahamike kuwa mifugo pia inastahili kuishi katika mazingira ambayo ni safi na salama. Kwa kufanya hivyo, itasaidia kuepusha wanyama kushambuliwa na magonjwa ya aina mbalimbali ikiwepo magonjwa ya ngozi yanayosababishwa na vimelea vinavyotokana na uchafu.…

Soma Zaidi

- Mifugo

Fahamu zao la sumu ya nyuki na uvunaji wake

Nchini Tanzania na maeneo mbalimbali barani Afrika, kumekuwa na ufugaji wa nyuki kwa ajili ya uvunaji wa mazao yake ili kujipatia fedha. Nyuki huvunwa mazao sita ambayo ni Asali(Honey), Nta (Wax), Chavua (Pollen), Gundi ya nyuki (Propolis), maziwa ya nyuki (Royal Jerry) pamoja na Sumu ya nyuki (Bee Venom). Lakini wafugaji wengi wamekuwa wakihagaika zaidi na zao la Asali na…

Soma Zaidi

- Mifugo

Fuata vidokezo kuhusu uuzaji wa mifugo ili kupata bei ya juu

Wafugaji wengi hawaelewi mienendo ya soko la mifugo. Wanaishia kuuza wanyama kwa bei ya chini wakati wanyama wale wale wangeweza kupata bei nzuri ikiwa mfugaji angekuwa mvumilivu na kuchukua muda kuelewa mwenendo wa soko na kuzingatia kanuni muhimu za uuzaji. Usifanye mauzo ya wanyama wachache na ya muda mfupi au kushtukiza. Hii ni kwa sababu mauzo yasiyo rasmi ni njia…

Soma Zaidi

- Mifugo

Boresha mikakati ya kutunza ng’ombe wa nyama

Tanzania ina uwezo mkubwa wa ufugaji wa ng’ombe wa nyama jambo ambalo linaweza kupelekea wakulima wadogo kupata fedha ikiwa watafanya usimamizi wa hali ya juu kuzalisha nyama kwa muda mfupi. Hata hivyo, malisho na maji bado ni changamoto kwa ufugaji wa ng’ombe wa nyama nchini kwani nyasi huwa nyingi wakati wa msimu wa mvua na hupunguka wakati wa kiangazi. Ili…

Soma Zaidi

- Mifugo

Umuhimu wa kuokoa makundi ya nyuki wadogo

Nyuki wadogo huitwa kwa jina maarufu la nyuki wasiouma.  Nyuki hawa wana umbo dogo kulinganisha na nyuki wanaouma lakini pia kila kabila katika Tanzania huwa na majina yake kama nyori, mbuyaa, mpunze, n.k. Mzinga uliotegeshwa katika tundu wanaoingilia nyuki wadogo ardhini kwa lengo la kuwaokoa toka ardhini kuingia kwenye mzinga huo. Nyuki hawa pia hutofautiana kulingana na meneo wanayopatikana.  Wapo…

Soma Zaidi

- Mifugo

Kutunza kumbukumbu za shamba la samaki na masoko

Kumbukumbu ambazo ni muhimu kwa ajili ya kutunzwa ni kama, ukubwa wa bwawa, idadi ya samaki, sehemu mbegu ilipochukuliwa, uzito wa mwanzo wa samaki, tarehe ya kupanda samaki, kiwango cha chakula kwa kila siku/wiki/mwezi, ubora wa maji, mahitaji ya kila siku na gharama zake , tarehe ya kuchukua sampuli, na wastani wa uzito wa samaki kwa kila mwezi. Taarifa hizi…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Anzisha miradi tofauti kuongeza pato lako

Kuna msemo mmoja maarufu sana wa Kiswahili usemao, kidole kimoja hakivunji chawa. Hii inamaanisha kuwa endapo unategemea jambo moja tu, inakuwa ni vigumu sana kutimiza malengo yako au kufanikiwa kufanya jambo fulani. Hii ni changamoto kwako mkulima kuhakikisha kuwa unatumia nafasi uliyo nayo ipasavyo. Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa unaanzisha miradi ya aina mbalimbali kulinganga na uwezo wako. Hiyo itakuwezesha…

Soma Zaidi