Zao la muhogo ni maarufu zaidi katika nchi za bara la Afrika. Zao hili hulimwa kwenye nchi zaidi ya 34 barani Afrika. Zao hili linajulikana zaidi kama mlinzi wa njaa kwa wakazi wa vijijini. Asili ya zao la muhogo Mihogo ni zao muhimu kwa chakula kwa nchi nyingi za Afrika na Amerika ya kusini. Kwa mara ya kwanza zao…
Mifugo
Vidokezo muhimu vya lishe kwa makundi tofauti katika jamii
Kumekuwa na maswali mengi kuhusu lishe hasa kutokana na janga la Covid-19. Maswali kama, je, tunapaswa kula nini kujenga na kudumisha mfumo wetu wa kinga ya mwili? Watu wengi wangependa kujua jinsi wanavyoweza kutumia vyakula vinavyopatikana kwa urahisi shambani au sokoni kuhakikisha afya bora kwa familia zao. Katika makala hii, tunaangazia mahitaji ya lishe ya makundi tofauti katika familia na…
Miaka tisa nikitumia jarida la Mkulima Mbunifu na kupata mafanikio lukuki
Mipango thabiti huzaa matunda mema na kila jambo likiwekwa katika mipango imara husababisha mafanikio. Hayo ni maneno ya Mzee Goodluck Lazaro Kimario na mkewe Rose Goodluck Kimario ambao ni miongoni mwa wakulima wa muda mrefu na wanufaika wa jarida la Mkulima Mbunifu. Wakulima hawa walikua wakiishi wilaya ya Tarime mkoani Mara ambapo mzee Goodluck alijishughulisha na majukumu ya kanisa huku…
Ulishaji wa chakula bora kwa kuku hupelekea utagaji wa mayai mengi na yenye ubora
Wafugaji walio wengi mara kwa mara wamekuwa wakilalamika sana hasa katika msimu wa baridi kuwa kuku hawatagi ama wakitaga basi utagaji wao huwa hafifu tofauti na msimu wa joto. Jambo hili limekuwa la kawaida sana na wafugaji wengi wamekuwa hawajishughulishi na ulishaji bora kwa kuku katika msimu wa baridi huku wakilisha vyema katika msimu wa joto. Hii si sawa kwani…
Kuku chotara wanahitaji chanjo kwa utaratibu maalumu
Ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara ni ufugaji ambao hujumuisha muunganiko au mchanganyiko wa aina mbili tofauti za kuku. Kuku chotara wana faida nyingi sana kwa mkulima ikiwa ni pamoja na ustahimilivu wa magonjwa hivyo kupunguza gharama za kutibu. Utagaji mkubwa wa mayai mengi mpaka kufikia 240 kwa mwaka kama ukiwalisha vizuri endapo watalishwa vizuri. Halikadhalika, kuku hawa wanakua haraka…
Mfugaji hana budi kufahamu na kutumia mfumo rahisi wa uchujaji maji kwenye bwawa la samaki
Moja ya changamoto kubwa sana katika ufugaji wa samaki ni uchafukaji wa maji kwenye bwawa ambao hupelekea kutokukua vizuri kwa samaki na kutokuwa na mavuno kwa wakati. Kama mkulima mbunifu ni vema sana kuwa mbunifu katika kutatua changamoto ambazo zinajitokeza katika mradi wako. Ili maji yasichafuke kwa haraka ni vema sana mfugaji apandikize samaki kulingana na ukubwa wa bwawa lake…
Jifunze kuhusu kiwavijeshi vamizi na namna ya kumdhibiti kwa kutumia dawa za kilimo hai
Jinsi ya kuzuia waharibufu wa mahindi kwa kutumia dawa ya kilimo hai Mahindi ni zao muhimu na tegemezi kwa jamii nyingi barani Afrika. Nchini Tanzania zao hili hulimwa mikoa yote kwani ni zao tegemezi kwa chakula. Hata hivyo, zao hili lina changamoto, kwani hushambuliwa na visumbufu mbalimbali vya mimea ikiwamo viwavijeshi vamizi (Fall armyworm). Viwavi hawa hula sehemu zote za…
Kilimo cha mahindi kwa kutumia mashimo na mbolea ya asili kimenihakikishia usalama wa chakula
“Miongoni mwa mafanikio niliyoweza kupata kutoka katika makala mbalimbali za jarida la Mkulima Mbunifu ni pamoja na; ufugaji wa nyuki, uanzishaji wa vitaru vya miti, kilimo cha mboga mboga kwa kutumia mbolea ya asili, pia nimeweza kuboresha uzalishaji wa samaki kwa kutumia lishe ambapo imenisaidia kupata kitoweo. Kutokana na haya kipato changu kimeongezeka na kumudu majukumu ya familia. Hii ni…
Ufugaji wa ndani wa kuku wa asili na banda bora la kufugia
Katika toleo lililopita tulielezea kwa undani kuhusu ufugaji wa kuku wa asili pamoja na mifumo ya ufugaji ikiwa ni mfumo huria na nusu huria. Katika toleo hili tutaangazia mfumo wa ndani na banda la kuku. Mfumo wa ndani ni mfumo ambao kuku hujengewa banda rasmi na hufugwa wakiwa ndani huku wakipatiwa chakula na maji. Kuku kufanyiwa huduma nyingine muhimu wakiwa…
Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na unamuda wa kuwahudumia wanyama hawa. Ufugaji wa sungura si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa. Sungura wanahitaji uangalizi hasa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu. Mabanda Kuna aina mbili ya mabanda ya kufugia: Kwanza ni mabanda ya kufugia ndani muda wote…






