Utupa ua kitaalamu Tephrosia vogelii ni mti mdogo wa jamii ya mikunde, wenye mizizi yenye vifundo vyenye bakteria maalumu wenye uwezo wa kubadili hewa ya Nitrogeni iweze kutumiwa na mmea kama nishati inayohitajika kwenye ukuaji wake. Utupa unaweza kupandwa kwa ajili ya kuboresha na kurutubisha udongo, kuni, kuua wadudu washambuliao mazao yaliyohifadhiwa na wadudu warukao (wanaoshambulia mazao wakati wa ukuaji).…
Mifugo
Ugonjwa wa kichocho na hatari zake kiafya
Ugonjwa wa kichocho umekua changamoto kwa jamii zinazoishi kandokando ya mito, na hasa katika maeneo yenye mashamba ya umwagiliaji. Tafiti zinaonesha asilimia 51% ya watanzania wapo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu hasa maeneo ya ukanda wa Pwani, ukanda wa ziwa Victoria, Tanganyika, Bwawa la nyumba ya Mungu-Mwanga na maeneo mengine yenye mashamba ya umwagiliaji. Ugonjwa wa kichocho (schistosomiasis/snail fever/bilharzia)…
Kilimo hai ni rafiki kwa mazingira
Njia nyingi zinazotumika katika kilimo siyo rafiki na mazingira. Njia za kawaida/ mazoea za kilimo ikiwemo, kilimo cha kuhama hama, kufyeka misitu na kuchoma majani/mabaki, vyote husababisha uharibifu wa mazingira. Maana ya Kilimo rafiki kwa mazingira Hii ni aina ya kilimo chenye kutumia mbinu bora za kilimo zenye tija kwa mkulima na kuyalinda mazingira. Ni mfumo unaohusisha ulimaji / matumizi…
Unaweza kuepuka umaskini kwa kufanya kilimo cha mihogo
Zao la muhogo ni maarufu zaidi katika nchi za bara la Afrika. Zao hili hulimwa kwenye nchi zaidi ya 34 barani Afrika. Zao hili linajulikana zaidi kama mlinzi wa njaa kwa wakazi wa vijijini. Asili ya zao la muhogo Mihogo ni zao muhimu kwa chakula kwa nchi nyingi za Afrika na Amerika ya kusini. Kwa mara ya kwanza zao…
Vidokezo muhimu vya lishe kwa makundi tofauti katika jamii
Kumekuwa na maswali mengi kuhusu lishe hasa kutokana na janga la Covid-19. Maswali kama, je, tunapaswa kula nini kujenga na kudumisha mfumo wetu wa kinga ya mwili? Watu wengi wangependa kujua jinsi wanavyoweza kutumia vyakula vinavyopatikana kwa urahisi shambani au sokoni kuhakikisha afya bora kwa familia zao. Katika makala hii, tunaangazia mahitaji ya lishe ya makundi tofauti katika familia na…
Miaka tisa nikitumia jarida la Mkulima Mbunifu na kupata mafanikio lukuki
Mipango thabiti huzaa matunda mema na kila jambo likiwekwa katika mipango imara husababisha mafanikio. Hayo ni maneno ya Mzee Goodluck Lazaro Kimario na mkewe Rose Goodluck Kimario ambao ni miongoni mwa wakulima wa muda mrefu na wanufaika wa jarida la Mkulima Mbunifu. Wakulima hawa walikua wakiishi wilaya ya Tarime mkoani Mara ambapo mzee Goodluck alijishughulisha na majukumu ya kanisa huku…
Ulishaji wa chakula bora kwa kuku hupelekea utagaji wa mayai mengi na yenye ubora
Wafugaji walio wengi mara kwa mara wamekuwa wakilalamika sana hasa katika msimu wa baridi kuwa kuku hawatagi ama wakitaga basi utagaji wao huwa hafifu tofauti na msimu wa joto. Jambo hili limekuwa la kawaida sana na wafugaji wengi wamekuwa hawajishughulishi na ulishaji bora kwa kuku katika msimu wa baridi huku wakilisha vyema katika msimu wa joto. Hii si sawa kwani…
Kuku chotara wanahitaji chanjo kwa utaratibu maalumu
Ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara ni ufugaji ambao hujumuisha muunganiko au mchanganyiko wa aina mbili tofauti za kuku. Kuku chotara wana faida nyingi sana kwa mkulima ikiwa ni pamoja na ustahimilivu wa magonjwa hivyo kupunguza gharama za kutibu. Utagaji mkubwa wa mayai mengi mpaka kufikia 240 kwa mwaka kama ukiwalisha vizuri endapo watalishwa vizuri. Halikadhalika, kuku hawa wanakua haraka…
Mfugaji hana budi kufahamu na kutumia mfumo rahisi wa uchujaji maji kwenye bwawa la samaki
Moja ya changamoto kubwa sana katika ufugaji wa samaki ni uchafukaji wa maji kwenye bwawa ambao hupelekea kutokukua vizuri kwa samaki na kutokuwa na mavuno kwa wakati. Kama mkulima mbunifu ni vema sana kuwa mbunifu katika kutatua changamoto ambazo zinajitokeza katika mradi wako. Ili maji yasichafuke kwa haraka ni vema sana mfugaji apandikize samaki kulingana na ukubwa wa bwawa lake…
Jifunze kuhusu kiwavijeshi vamizi na namna ya kumdhibiti kwa kutumia dawa za kilimo hai
Jinsi ya kuzuia waharibufu wa mahindi kwa kutumia dawa ya kilimo hai Mahindi ni zao muhimu na tegemezi kwa jamii nyingi barani Afrika. Nchini Tanzania zao hili hulimwa mikoa yote kwani ni zao tegemezi kwa chakula. Hata hivyo, zao hili lina changamoto, kwani hushambuliwa na visumbufu mbalimbali vya mimea ikiwamo viwavijeshi vamizi (Fall armyworm). Viwavi hawa hula sehemu zote za…







