Uchaguzi wa Mbuzi/Kondoo wa Kufuga Madhumuni ya kuchagua mbuzi au kondoo wa kufuga ni kuboresha uzalishaji na kuendeleza kizazi bora. Kuna aina nyingi za mbuzi/kondoo wanaoweza kufugwa kulingana na mazingira na mahitaji ya mfugaji. Uchaguzi hufanyika kwa kuangalia umbile, uzalishaji na kumbukumbu za wazazi kama vile umbo kubwa, ukuaji wa haraka, uwezo wa kutunza vitoto na kutoa maziwa mengi. Mbuzi/kondoo…
Mifugo
Ni muhimu kutambua minyoo inayoshambulia mazao
Mara nyingi tumekuwa tukizungumza kuhusu wadudu rafiki na halikadhalika kuweka wazi kuhusu wadudu wanaoshambulia mazao. Katika toleo hili tutajifunza kuhusu minyoo inayoshambulia mazao. Ipo minyoo ya aina nyingi ambayo inafaida katika urutubishaji wa udongo na mingine ambayo ina madhara kwa mimea, wanyama pamoja na binadamu. Minyoo hutofautiana kwa ukubwa wa maumbile, mfano ipo inayoonekana kwa macho ya kawaida na ile…
Je, tunajali lishe bora kwa ajili ya watoto wetu kila siku?
Tofauti na ilivyo kwa watu wazima, watoto wanahitaji kupata lishe bora kila siku ili kuweza kujenga miili yao, na kukua katika kiwango kinachotakiwa na hatimae kuwa watu wazima. Ni muhimu kufahamu lishe inayotakiwa kwa watoto. Lishe bora ni nini? Lishe bora ni mlo unaojumuisha uwiano unaotakiwa wa virutubisho vyote muhimu vinavyotakiwa kutoka katika makundi makubwa ya vyakula. Miili yetu huhitaji…
Usimamizi wa rutuba ya udongo kwa njia za kilimo hai
Usimamizi wa rutuba ya udongo sio tu kuweka mbolea au kupata mavuno mengi peke yake. Ni kuhusu kujenga udongo wenye rutuba thabiti na hai. Mifumo ya kilimo yenye uzalishaji endelevu inahitaji usimamizi mzuri wa rutuba ya udongo ili kuhakikisha uendelevu wa muda mrefu wa uzalishaji wa chakula wa kwao wenyewe. Ndio sababu kwa nini usimamizi sahihi wa rutuba ya…
Soko na utayarishaji wa mazao ya nguruwe
Kwa muda mrefu na katika makala tofauti, MkM imeeleza kwa undani namna nzuri ya uzalishaji wa nguruwe bora, pamoja na lishe yake na mambo kadha wa kadha yanayohusiana na nguruwe. Katika makala hii utapata kufahamu kuhusiana na soko na namna ya utayarishaji wa mazao. Soko la mazao yatokanayo na nguruwe ni sawa na soko la mazao mengine yaliyo sokoni na…
Nimepata mafanikio makubwa katika utengenezaji na matumizi ya mbolea ya maji
Mkulima anaweza kupunguza gharama, kuongeza rutuba kwenye udongo, mavuno pamoja na kipato kwa kutengeneza mbolea mwenyewe. Mimea inaweza kukuonyesha inahitaji nini. Ni rahisi sana kugundua endapo mimea haipati virutubisho vya kutosha. Majani kubadili rangi ni ishara tosha kuwa mimea ina upungufu wa virutubisho. Ni lazima mkulima awe tayari kutatua tatizo hilo kwa haraka kabla hali haijawa mbaya. Upungufu wa madini…
Jinsi ya kugundua upungufu wa virutubisho katika mmea
Nitrogen Dalili: Mahindi, maharage na mboga hukua kwa taabu sana, majani yanakuwa na kijani mpauko. Sukumawiki na kabichi majani yanakuwa na mchanganyiko wa rangi ya njano. Majani ya chini ndiyo huathiriwa kwanza, na kiwango cha maua kuchanua hupungua au kuchelewa. Kutibu: Ongeza kiasi cha kutosha cha mbolea za asili. Panda mimea inayosaidia kuongeza nitrojen kama lablab, desmodium(figiri) na lusina. Weka…
Utupa (Tephrosia vogelii) Mmea wenye faida nyingi kwa mazingira na wanyama
Utupa ua kitaalamu Tephrosia vogelii ni mti mdogo wa jamii ya mikunde, wenye mizizi yenye vifundo vyenye bakteria maalumu wenye uwezo wa kubadili hewa ya Nitrogeni iweze kutumiwa na mmea kama nishati inayohitajika kwenye ukuaji wake. Utupa unaweza kupandwa kwa ajili ya kuboresha na kurutubisha udongo, kuni, kuua wadudu washambuliao mazao yaliyohifadhiwa na wadudu warukao (wanaoshambulia mazao wakati wa ukuaji).…
Ugonjwa wa kichocho na hatari zake kiafya
Ugonjwa wa kichocho umekua changamoto kwa jamii zinazoishi kandokando ya mito, na hasa katika maeneo yenye mashamba ya umwagiliaji. Tafiti zinaonesha asilimia 51% ya watanzania wapo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu hasa maeneo ya ukanda wa Pwani, ukanda wa ziwa Victoria, Tanganyika, Bwawa la nyumba ya Mungu-Mwanga na maeneo mengine yenye mashamba ya umwagiliaji. Ugonjwa wa kichocho (schistosomiasis/snail fever/bilharzia)…
Kilimo hai ni rafiki kwa mazingira
Njia nyingi zinazotumika katika kilimo siyo rafiki na mazingira. Njia za kawaida/ mazoea za kilimo ikiwemo, kilimo cha kuhama hama, kufyeka misitu na kuchoma majani/mabaki, vyote husababisha uharibifu wa mazingira. Maana ya Kilimo rafiki kwa mazingira Hii ni aina ya kilimo chenye kutumia mbinu bora za kilimo zenye tija kwa mkulima na kuyalinda mazingira. Ni mfumo unaohusisha ulimaji / matumizi…








