Mifugo

- Mifugo

Fahamu na uzingatie kanuni bora za ufugaji wa mbuzi na kondoo

Uchaguzi wa Mbuzi/Kondoo wa Kufuga Madhumuni ya kuchagua mbuzi au kondoo wa kufuga ni kuboresha uzalishaji na kuendeleza kizazi bora. Kuna aina nyingi za mbuzi/kondoo wanaoweza kufugwa kulingana na mazingira na mahitaji ya mfugaji. Uchaguzi hufanyika kwa kuangalia umbile, uzalishaji na kumbukumbu za wazazi kama vile umbo kubwa, ukuaji wa haraka, uwezo wa kutunza vitoto na kutoa maziwa mengi. Mbuzi/kondoo…

Soma Zaidi

- Mifugo

Ni muhimu kutambua minyoo inayoshambulia mazao

Mara nyingi tumekuwa tukizungumza kuhusu wadudu rafiki na halikadhalika kuweka wazi kuhusu wadudu wanaoshambulia mazao. Katika toleo hili tutajifunza kuhusu minyoo inayoshambulia mazao. Ipo minyoo ya aina nyingi ambayo inafaida katika urutubishaji wa udongo na mingine ambayo ina madhara kwa mimea, wanyama pamoja na binadamu. Minyoo hutofautiana kwa ukubwa wa maumbile, mfano ipo inayoonekana kwa macho ya kawaida na ile…

Soma Zaidi

- Mifugo

Je, tunajali lishe bora kwa ajili ya watoto wetu kila siku?

Tofauti na ilivyo kwa watu wazima, watoto wanahitaji kupata lishe bora kila siku ili kuweza kujenga miili yao, na kukua katika kiwango kinachotakiwa na hatimae kuwa watu wazima. Ni muhimu kufahamu lishe inayotakiwa kwa watoto. Lishe bora ni nini? Lishe bora ni mlo unaojumuisha uwiano unaotakiwa wa virutubisho vyote muhimu vinavyotakiwa kutoka katika makundi makubwa ya vyakula. Miili yetu huhitaji…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Usimamizi wa rutuba ya udongo kwa njia za kilimo hai

Usimamizi wa rutuba ya udongo sio tu kuweka mbolea au kupata mavuno mengi peke yake. Ni kuhusu kujenga udongo wenye rutuba thabiti na hai.    Mifumo ya kilimo yenye uzalishaji endelevu inahitaji usimamizi mzuri wa rutuba ya udongo ili kuhakikisha uendelevu wa muda mrefu wa uzalishaji wa chakula wa kwao wenyewe. Ndio sababu kwa nini usimamizi sahihi wa rutuba ya…

Soma Zaidi

- Mifugo

Soko na utayarishaji wa mazao ya nguruwe

Kwa muda mrefu na katika makala tofauti, MkM imeeleza kwa undani namna nzuri ya uzalishaji wa nguruwe bora, pamoja na lishe yake na mambo kadha wa kadha yanayohusiana na nguruwe. Katika makala hii utapata kufahamu kuhusiana na soko na namna ya utayarishaji wa mazao. Soko la mazao yatokanayo na nguruwe ni sawa na soko la mazao mengine yaliyo sokoni na…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Nimepata mafanikio makubwa katika utengenezaji na matumizi ya mbolea ya maji

Mkulima anaweza kupunguza gharama, kuongeza rutuba kwenye udongo, mavuno pamoja na kipato kwa kutengeneza mbolea mwenyewe. Mimea inaweza kukuonyesha inahitaji nini. Ni rahisi sana kugundua endapo mimea haipati virutubisho vya kutosha. Majani kubadili rangi ni ishara tosha kuwa mimea ina upungufu wa virutubisho. Ni lazima mkulima awe tayari kutatua tatizo hilo kwa haraka kabla hali haijawa mbaya. Upungufu wa madini…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Jinsi ya kugundua upungufu wa virutubisho katika mmea

 Nitrogen Dalili: Mahindi, maharage na mboga hukua kwa taabu sana, majani yanakuwa na kijani mpauko. Sukumawiki na kabichi majani yanakuwa na mchanganyiko wa rangi ya njano. Majani ya chini ndiyo huathiriwa kwanza, na kiwango cha maua kuchanua hupungua au kuchelewa. Kutibu: Ongeza kiasi cha kutosha cha mbolea za asili. Panda mimea inayosaidia kuongeza nitrojen kama lablab, desmodium(figiri) na lusina. Weka…

Soma Zaidi

- Mifugo

Utupa (Tephrosia vogelii) Mmea wenye faida nyingi kwa mazingira na wanyama

Utupa ua kitaalamu Tephrosia vogelii ni mti mdogo wa jamii ya mikunde, wenye mizizi yenye vifundo vyenye bakteria maalumu wenye uwezo wa kubadili hewa ya Nitrogeni iweze kutumiwa na mmea kama nishati inayohitajika kwenye ukuaji wake. Utupa unaweza kupandwa kwa ajili ya kuboresha na kurutubisha udongo, kuni, kuua wadudu washambuliao mazao yaliyohifadhiwa na wadudu warukao (wanaoshambulia mazao wakati wa ukuaji).…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Ugonjwa wa kichocho na hatari zake kiafya

Ugonjwa wa kichocho umekua changamoto kwa jamii zinazoishi kandokando ya mito, na hasa katika maeneo yenye mashamba ya umwagiliaji. Tafiti zinaonesha asilimia 51% ya watanzania wapo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu hasa maeneo ya ukanda wa Pwani, ukanda wa ziwa Victoria, Tanganyika, Bwawa la nyumba ya Mungu-Mwanga na maeneo mengine yenye mashamba ya umwagiliaji. Ugonjwa wa kichocho (schistosomiasis/snail fever/bilharzia)…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Kilimo hai ni rafiki kwa mazingira

Njia nyingi zinazotumika katika kilimo siyo rafiki na mazingira. Njia za kawaida/ mazoea za kilimo ikiwemo, kilimo cha kuhama hama, kufyeka misitu na kuchoma majani/mabaki, vyote husababisha uharibifu wa mazingira. Maana ya Kilimo rafiki kwa mazingira Hii ni aina ya kilimo chenye kutumia mbinu bora za kilimo zenye tija kwa mkulima na kuyalinda mazingira. Ni mfumo unaohusisha ulimaji / matumizi…

Soma Zaidi