Karakara ni zao la matunda ambalo ni muhimu kwa biashara na chakula linalolimwa katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Dar es Salaam, Tanga, Kigoma, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha. Mara nyingi wakulima huzalisha zao hili kwa wingi sana kwa msimu mmoja na hatimae kushuka kwa soko lake na kufanya kuwepo kwa upotevu na uharibifu wa matunda haya. Ili kuondokana na uharibifu huu,…
Usindikaji
HERI YA MWAKA MPYA WA 2022
Heri ya mwaka mpya 2022 Ni matumaini yetu kuwa sote tumevuka salama na tumejiandaa vyema katika kuukabili tena mwaka huu kwa kishindo katika kilimo na ufugaji ili kuongeza tija na kukuza uchumi lakini pia tukizalisha kwa misingi ya kilimo hai kwa ajili ya kulinda afya zetu, wanyama, mazingira na mimea. Ni hakika, mwaka uliopita haukuwa mbaya sana kwani pamoja na…
Je, unafahamu kuwa kilimo hai kinalipa
Bonyeza hapo juu kusikiliza kuhusu kilimo hai
Ufugaji mseto wa samaki na mazao mengine
Katika toleo lililopita tuliangalia utangulizi wa mada hii ya ufugaji mseto wa samaki na mazao mengine. Tuliweza kuangazia mambo kadha wa kadha muhimu, na miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na faida za ufugaji huo, pamoja na manufaa ya ufugaji wa namna hiyo; Aina ya samaki wanaofaa katika kilimo mseto Perege na Kambale ni samaki wanaofugwa katika maeneo mabalimbali nchini…
Uzalishaji wa mafuta ya karanga
Karanga hutumika kama kiungo katika mapishi mbalimbali au kukaangwa ili kutumika kama vitafunwa lakini pia kusindikwa ili kupata mafuta, siagi na rojo. Karanga zina virutubisho vingi kama vile; maji asilimia 7, nguvu kilokari 570, protini gramu 23, mafuta gramu 45, wanga gramu 20, kalishamu miligramu 49, chuma miligramu 3.8, patasiamu miligramu 680, vitamini B miligramu 15.5 na vitamini A (I.U…
Utengenezaji wa jibini ngumu
Hii ni jibini aina ya cheddar ambayo asili yake ni huko Uingereza lakini kwasasa hutengenezwa katika nchi mbalimbali dunian. Hatua za utengenezaji Pima ubora wa maziwa Pasha moto maziwa kufikia nyuzi joto 65C yaache katika joto kwa dakika 30 au nyuzi joto 71.5C kwa sekunde 15 Poza maziwa kufikia nyuzi joto 22 hadi 25C Weka kimea cha mtindi (mesophilic) asilimia…
Ukaushaji wa mbogamboga
Kikundi cha usindikaji cha mbogamboga na matunda kutoka SAT (Sustainable Agriculture Tanzania) Mbogamboga jamii ya majani Majani ya maboga na mchicha Chagua majaNi mabichi na laini Chambua mboga na kuondoa nyuzinyuzi Osha majani yako kwa maji safi Tumbukiza mboga kwenye maji ya vuguvugu kwa dakiki 3-5 ,kisha weka mboga kwenye maji ya baridi Kwa dakika 1 ipoe ili kuzia kuendele…
TUNAOMBA RADHI KWA KUCHELEWA KUTUMA JARIDA LA OKTOBA
Habari ndugu msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu. Ni matumaini yetu kuwa uko salama na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku. Tunaomba radhi kwa kuchelewa kukutumia nakala yako ya jarida la Mkulima Mbunifu. Hii ni kutokana na kuwepo kwa changamoto kidogo zilizokuwa nje ya uwezo wetu ambazo zimepelekea kusindwa kuchapisha nakala ya mwezi Oktoba kwa wakati. Jarida hili…
Tunaomba radhi kwa kutokusikika hewani
Ndugu msikilizaji na mfuatiliaji wa vipindi vya radio vya Mkulima Mbunifu/SAT, tunaomba radhi kutokana na kipindi chetu kilichokusudiwa kurushwa hewasi siku ya jumamosi tarehe 30 Oktoba 2021 kutokusikika. Hii ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Sasa kipindi hicho cha kilimo kilichokuwa kinahusu kilimo mseto na kilimo cha mzunguko wa mazao kitarushwa upya siku ya jumamosi ya tarehe…
Sikiliza vipindi vya redio vya Mkulima Mbunifu
Tunapenda kuwataarifu na kuwakumbusha wasomaji wetu kusikiliza vipindi vya radio vya Mkulima Mbunifu Vinavyosikika kupitia TBC Taifa kila siku ya jumamosi saa mbili na robo usiku (2:15) na marudio siku ya alhamisi saa tisa na nusu mchana (9:30) Kupitia vipindi hivi, MkM inatoa elimu stahiki kwa kurusha mada mbalimbali kwa wakulima wadogo na hata wakubwa, kuweka kipaumbele katika kuthamini misingi…