Kumbukumbu ambazo ni muhimu kwa ajili ya kutunzwa ni kama, ukubwa wa bwawa, idadi ya samaki, sehemu mbegu ilipochukuliwa, uzito wa mwanzo wa samaki, tarehe ya kupanda samaki, kiwango cha chakula kwa kila siku/wiki/mwezi, ubora wa maji, mahitaji ya kila siku na gharama zake , tarehe ya kuchukua sampuli, na wastani wa uzito wa samaki kwa kila mwezi. Taarifa hizi…
Mifugo
Anzisha miradi tofauti kuongeza pato lako
Kuna msemo mmoja maarufu sana wa Kiswahili usemao, kidole kimoja hakivunji chawa. Hii inamaanisha kuwa endapo unategemea jambo moja tu, inakuwa ni vigumu sana kutimiza malengo yako au kufanikiwa kufanya jambo fulani. Hii ni changamoto kwako mkulima kuhakikisha kuwa unatumia nafasi uliyo nayo ipasavyo. Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa unaanzisha miradi ya aina mbalimbali kulinganga na uwezo wako. Hiyo itakuwezesha…
Ubora wa zizi huinua uzalishaji wa mbuzi na kondoo
Ufugaji wa Mbuzi na kondoo ni wa gharama nafuu sana hasa ukilinganisha na ng’ombe kwani wanyama hawa wana uwezo wa kuishi mahali popote na katika mazingira magumu kama yenye maradhi na ukame. Wanyama hawa kulingana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo huku wakihudumiwa na familia zenye nguvu kazi ndogo na kipato cha chini. Wanyama hawa ambao hufugwa…
Mfugaji anaweza kuongeza pato kwa kufuga bata
Wafugaji wengi wa ndege wamekuwa wakikazana zaidi namna ya kufuga aina mbalimbali za ndege bila kujumisha bata. Aina hii ya ndege wanaweza pia kuwa chanzo kizuri cha kuongeza pato. Wafugaji wengi wadogo wa bata nchini Tanzania hufuga bata chotara ambao wamechanganyika na aina mbalimbali za jamii ya bata. Aina nyingine inaweza kuwa bata bukini, bata maji, au bata mzinga. Matumizi…
Fahamu sifa, faida na changamoto za ufugaji kuku wa asili
Kuku wa asili ni aina ya kuku ambao wamekuwepo nchini kwa muda wa miaka mingi na damu au koo zao hazikuchanganywa na aina yeyote ya kuku wa kienyeji. Kuku hawa wana rangi na maumbo mbalimbali. Kwa kawaida ufugaji wa kuku wa asili nchini Tanzania hufanywa na wafugaji wadogo wadogo wanaoishi kandokando ya miji na wale wanaoishi hasa vijijini. Kuku hawa…
Unaweza kusindika ngozi kiasili kupata bidhaa bora
Usindikaji wa viwandani unahitaji mitambo mikubwa, maeneo makubwa nguvu kazi kubwa, malighafi nyingi. Hivyo inahitaji mtaji mkubwa. Njia hii pia inahitaji kemikali za viwandani hivyo sio rafiki kwa mazingira. Usindikaji wa asili ni rahisi kwani malighafi za uchakataji hupatikana katika mazingira yanayotuzunguka. Njia hii inashauriwa sana kwa wajasiriamali wadogo wadogo ambao hawana mitaji mikubwa na unaweza kuchakata ngozi moja kwa…
Wafahamu Nzi Chuma (Black soldier Fly), protini mbadala kwa mifugo
Nzi chuma (Black Soldier Fly), kwa kisayansi Hermetia illucens (Linnaeus) ni aina ya nzi katika kundi la Stratiomyidae ambao hupatikana sana katika ukanda wa Magharaibi mwa hemisphere yaani mabara ya Marekani ya kusini na kaskazini, sehemu ya Africa, Ulaya, Antactical, Asia na pia Australia. Nzi hawa wana protini ya kutosha kulishia mifugo. Nzi hawa hawana madhara ya aina yoyote kwa…
Call for Proposals to Develop a Television Spot on Healthy Food Production and Consumption
Mkulima Mbunifu (MkM) is a farmer information service based in Arusha, Tanzania, and implemented since July 2011 with support from Biovision Foundation, Switzerland and Biovision Africa Trust (BvAT), Nairobi, Kenya. MkM aims to provide information to smallholder farmers to enable them adopt improved sustainable agriculture technologies and practices. MkM also aims to provide information to extension workers, researchers and students and…
Mbolea hai na madawa ya asili ni muhimu kwa mimea, wanyama na binadamu
Mkulima anapotumia mbolea za viwandani na kemikali kwa muda mrefu, ni dhahiri kuwa udongo hudhoofika na kushindwa kuzalisha. Afya yake pia ipo mashakani kwa kuwa kemikali zina madhara makubwa sana. Kilimo ni lazima kuwezesha na kuongeza afya ya udongo, mimea, wanyama na binadamu. Udongo ni nguzo muhimu katika maisha ya viumbe wote kwa ujumla. Udongo ulioharibiwa hauwezi kuzalisha chakula vizuri,…
Ugonjwa wa kiwele (mastitis)
Katika toleo lililopita tulizungumzia kwa ufupi kuhusu ugonjwa wa kiwele, madhara pamoja na dalili zake. Aidha tuliona jinsi ugonjwa huu unavyosababisha uvimbe, muwasho na joto kwenye kiwele cha mnyama na usababishwa na aina nyingi ya wadudu aina ya bakteria. Katika toleo hili, tutamalizia mada hii kwa undani ili mfugaji aweze kufahamu namna ya kuzuia ama kukabiliana na ugonjwa huu mara…









