Busta za asili ni nyongeza ya virutubisho kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa mmea ili kua na uzalishaji mzuri hususani pale ambapo mimea imeanza kuzorota kutokana na kupungua/kukosekana kwa virutubisho vya kutosha kwenye udongo, busta hizi zina sifa ya kuupa mmea virutubisho kwa haraka sana na kuleta matokeo mazuri kwenye mimea ndani ya muda mfupi(siku 3). Aina za busta 1.…
Mikakati Madhubuti ya Kuuza Mazao ya kilimo hai
Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na mabadiliko makubwa katika kilimo na mbinu za uzalishaji. Utafiti umeonyesha kuwa mbinu asilia za kilimo hai zina faida zaidi kuliko zile zinazojumuisha kemikali au vitu vingine hatari. Siku hizi, bidhaa za kilimo hai zinapatikana kwa urahisi katika maeneo mengi. Hii inamaanisha kuwa kuna ushindani kati ya wazalishaji wa kilimo hai. Ikiwa unataka kufanikiwa…
Ufugaji wa ng,ombe wenye tija
Naomba ushauri, nina ng’ombe mmoja ambaye namfuga ndani. Amezaa uzao wa kwanza ndama dume. Kwa sasa, ninapata lita 10 kwa siku. Ng’ombe ana uzito wa kilo 400. Gharama za utunzaji ni 70%. Nifanye nini ili awe na tija? Faida zinazotokana na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa zinatokana na kujumuisha mambo mawili muhimu; aina ya ng’ombe na utunzaji wake. Utunzaji huchukua…
Mkulima hupaswi kuwa maskini
Swali hili limekuwa likijirudia mara kwa mara, kuwa ni kwa nini wakulima wawe maskini? Kwa watu walio wengi hata wakulima wenyewe, wana majibu mengi sana ambayo wamekuwa wakiyatoa, hasa katika kutetea huko hiyo, huku wakiweka kuwa wao ni watu wa chini na wanaokubaliana na hali hiyo ya umaskini. Kuna wale ambao watasema kuwa ni maskini kwa sababu ya zana duni…
Namna ya kufanya candling (uchunguzi wa mayai yanayototoleshwa)
Makala hii ni muendelezo wa makala iliyopita ambapo ilijikita katika kuelezea namna ya kutotolesha mayai kwa njia ya asili na pia kwa njia ya mashine (Incubator). Katika muendelezo huu tutaangalia kwa undani jinsi ya kuchunguza yai kwa kutumia mwanga. Candling ni njia ya kuchunguza mayai kwa kutumia mwanga aidha wa mshumaa au tochi. Tochi ambayo ni kifaa cha kisasa ni…
Ifahamu ndizi kitarasa na faida zake
Ndizi ya Kitarasa ni moja ya ndizi inayotumika kama chakula cha kitamaduni kwa wachaga waishio katika mkoa wa Kilimanjaro. Aina hii ya ndizi hutumiwa kutengeneza unga wa uji, kutengeneza bia ya kitamaduni na kama mchanganyiko wa chakula cha kitamaduni katika sahani. Hata hivyo, wazalishaji wa kitarasa walipungua, kutokana na mabadiliko ya utamaduni, mtindo wa maisha, upatikanaji duni wa soko na…
Tengeneza mbolea ya chai ya alizeti pori (Tithonia diversifolia)
Alizeti pori maarufu kisayansi tithionia diversifolia ni aina ya mmea unaomea karibu kila mahali kando ya barabara na hata kwenye kingo za mito katika ardhi isiyokuwa na rutuba au hata katika maeneo ya bustani. Mmea huu ni mrefu na una mashina mengi kuanbzia sehemu ya chini hadi sehemu kunakotoa maua. Kwenye udongo wenye rutuba, mmea huu huweza kufikia urefu wa…
Mambo muhimu ya kuzingatia kwa unenepeshaji wa nguruwe
Nguruwe wanaonenepeshwa wanahitaji kutunzwa vizuri ili waweze kufikia uzito wa kuchinjwa mapema. Nguruwe waanze kunenepeshwa wakiwa na umri wa wiki 9 hadi 14 na uzito wa kilo 25 hyadi 30. Nguruwe wana uwezo wa kuongezeka uzito wa hadi gramu 700 na 800 kwa siku kuitegemeana na aina ya nguruwe na matunzo. Nguruwe wanaweza kunenepeshwa na kufikisha uzito wa kuchinjwa yaani…