- Kilimo, Mimea

Samadi ya wanyama na mimea

Ubora wa samadi ya wanyama hutegemea zaidi kile kilicholiwa na mnyama. Ikiwa wamelishwa chakula duni au nyasi zilizomea katika udongo usio na rutuba, basi samadi yao pia itakuwa na ubora duni. Ikiwa wanyama wamelishwa chakula kizuri basi samadi pia itakuwa bora na iliyojaa virutubisho. Samadi iliyo tayari kwa matumizi Samadi huhitaji kupevuka kwa majuma au miezi kadhaa kabla ya kuwa…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Mapapai bora hupelekea soko lenye tija

Mapapai ni zao moja kati ya mazao ya matunda yenye vitamin A na madini ya kalsiamu kwa wingi na zao hili hulimwa karibu kila mahali hapa nchini kwa wastani wa tani 2,582 kwa mwaka. Ili kuweza kuzalisha zao la papai kwa wingi na kwa ubora unaotakiwa ni muhimu kuhakikisha unazingatia kanuni zote za kilimo bora za uzalishaji wa mapapai. Ubora…

Soma Zaidi

- Mifugo

Chokaa au majivu huweza kuangamizi kiwavijeshi vamizi

Wakulima walio wengi katika mikoa mbalimbali hapa nchini wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiwavijeshi vamizi, mdudu ambaye husababisha hasara kubwa kwa wakulima hasa wa mahindi kwani hupoteza maelfu ya hekari za mazao endapo watavamiwa na mdudu huyu. Kuna mbinu mbalimbali za kudhibiti mdudu huyu kama vilekufanya kilimo bora mfano kupanda kwa wakati, matumizi ya mbegu kinzani (tolerant/resistant varieties), matumizi ya viumbe…

Soma Zaidi

- Mifugo

Dume bora ni chanzo cha uzalishaji bora

Unapojipanga kwa ajili ya ufugaji wa ng’ombe kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa au nyama, jambo la msingi ni kuhakikisha ni aina gani ya ng’ombe utachagua/utanunua au utatumia katika uzalishaji. Aina hii ya ng’ombe pia pamoja na kuwa utanunua lakini hutokana na dume bora hivyo ni jambo la msingi sana kujua aina ya uzalishaji wako umetokana na dume mwenye ubora.…

Soma Zaidi

- Mifugo

Ongeza lishe kwa kutumia njia rahisi za ufugaji samaki

Ufugaji wa samaki ni moja ya shughuli ambazo hivi karibuni imejipatia umaarufu mkubwa sana miongoni mwa wafugaji. Kazi hii imekuwa ikifanywa na makundi mbalimbali bila kujali wanafanya shughuli gani nyingine. Kutokana na uhitaji mkubwa wa lishe inayotokana na samaki, kumekuwa na aina mbalimbali za ugunduzi unaosaidia ufugaji wa samaki kwa njia rahisi. Katika makala hii tutaeleza ugunduzi mpya wa kutengeneza…

Soma Zaidi

- Kilimo

Jifunze namna bora ya ubebeshaji wa miche ya matunda mbalimbali

Ubebeshaji maana yake ni uunganishaji wa sehemu mbili au zaidi za mimea tofauti na kuwa mmea wenye shina moja. Ubebeshaji hufanyika katika mimea ya mazao ambayo yako katika jamii au ukoo mmoja kwa mfano; embe dodo na viringe, chungwa na limao, parachichi aina ya hass na la kienyeji, passion zambarau na njano, biringanya za aina tofauti, maua ya waridi ya…

Soma Zaidi

- Mifugo

Utaratibu wa kinga za magonjwa kwenye kuku wa asili/kienyeji

Kuku wa kienyeji nao wanahitaji kupata chanjo ya magonjwa na kwa utaratibu unaofaa. Ugonjwa Jinsi ya kuudhibiti Mdondo/kideri (Newcastle disease) Kama tete lilichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki tatu za kwanza za maisha yao.   Wachanje vifaranga hawa dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.   Vifaranga ambao historia…

Soma Zaidi

- Mifugo

Uzalishaji wa minyoo kwa ajili ya kuku, bata na samaki

Minyoo redworms ni chakula kizuri sana kwa kuku, bata na samaki kwani minyoo wana protini nyingi sana na kuku wakipewa au kulishia minyoo wanakua kwa haraka sana na huwafanya kuwa na maumbile makubwa sana (wanakuwa na uzito mkubwa pia). Kutengeneza minyoo ya chakula ni utaratibu wa kuzalisha minyoo kwa ajili ya kuku, bata na samaki. Namna ya kuzalisha Chukua mavi…

Soma Zaidi

- Mimea

Nimepiga hatua kwa kulima Canavalia

“Nilikuwa naotesha ekari tatu za mahindi na maharage lakini niliishia kuvuna chini ya gunia 10 za mahindi lakini pia nikipata maharage kidogo sana”. Hivyo ndivyo alivyoanza kueleza Bi. Edvester O. Yambazi (68), mkazi wa Sanya Juu ambaye kwasasa ameamua kufanya kilimo cha mahindi huku akiotesha zao funikizi aina ya Canavalia. Safari ya kilimo Bi. Yambazi anaeleza kuwa, aliteseka kwa muda…

Soma Zaidi

- Binadamu, Mimea

Tumia mazao funikizi kwa chakula na kulisha mifugo

Mazao funikizi siyo mageni sana kwa wakulima walio wengi isipokuwa kwa wale ambao ndio kwanza wanaanza kujiingiza katika kilimo hifadhi. Si mazao yote funikizi yanayoweza kutumika kulishia mifugo moja kwa moja mara baada ya kuvuna kutoka shambani. Mengine ni lazima yafanyiwe maandalizi fulani ndipo yatumike kulishia. Mazao funikizi kama vile, canavalia yanahitajika kukaushwa kwanza na kuandaliwa vyema kabla ya kulisha…

Soma Zaidi