Mifugo
Ukisoma jarida la Mkulima Mbunifu kila siku utakuwa na tabasamu usoni mwako
Hebu waangalie wanufaika wa jarida la Mkulima Mbunifu wakifurahia kupata nakala zao
Uzalishaji wa malisho
Bonyeza hapa na sikiliza kuhusu malisho aina ya matete na faida zake
Mimi nasoma Jarida la Mkulima Mbunifu, wewe Je?
Hebu tazama tabasamu la mama huyu usoni, mara tu aonapo jarida la Mkulima Mbunifu na azidi pale anapokutana na taarifa muhimu kwake? Ni furaha iliyoje? Hebu na wewe kuwa mmojawapo wa wanufaika wa jarida hili, nakuahidi hutajutia….. Jarida pekee lililosheheni taarifa za kilimo hai, ufugaji wa mifugo aina mbalimbali, utunzaji wa udongo, mazingira na afya ya mwadamau kwa ujumla…… Mkulima…
Kutunza ndama wa ng’ombe/mbuzi iwapo mama yake amekufa
Mara tuu baada ya kuzaliwa na kwa kipindi cha siku 3 hadi 4 za mwanzo, ndama huhitaji maziwa ya mwanzo ya mama yake yaani dang’a (colostrum) Ni jambo la muhimu sana kuhakikisha kuwa baada ya kuzaliwa ndama anapata maziwa haya ya mwanzo kabla yakupita masaa mawili. Faida ya maziwa ya mwanzo Maziwa ya mwanzo yana kiwango kikubwa zaidi cha viinilishe…
Je, unawatendea haki kuku wako kulinda afya zao na yako
Kumekuwa na imani potofu kutoka kwa watu wengi ikiwamo mafunzo ya kigeni kuwa ufugaji wa kuku kwenye vibanda vidogo vya chuma visivyowapa nafasi ya kutoka ndiyo ufugaji wa kisasa wenye tija jambo hili ni hatari na ukiukwaji wa haki za wanyama. Kuku ni aina ya ndege wanaofugwa na binadamu kwa madhumuni mbalimbali. Asili ya ndege hawa kama ilivyo kwa wengine…
TUNAOMBA RADHI KWA KUCHELEWA KUTUMA JARIDA LA OKTOBA
Habari ndugu msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu. Ni matumaini yetu kuwa uko salama na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku. Tunaomba radhi kwa kuchelewa kukutumia nakala yako ya jarida la Mkulima Mbunifu. Hii ni kutokana na kuwepo kwa changamoto kidogo zilizokuwa nje ya uwezo wetu ambazo zimepelekea kusindwa kuchapisha nakala ya mwezi Oktoba kwa wakati. Jarida hili…
Umuhimu wa kuotesha malisho kukabili ukame Malisho yaliyo mengi hapa nchini ya asili ambayo hutegemewa na mifugo hukomaa na kukauka mapema zaidi na hivyo kusababisha lishe kwa wanyama kuwa duni wakati wa kiangazi ambapo wanyama huhangaika sana kupata chakula. Kutokana na upungufu huo ni vyema wafugaji kuotesha aina mbalimbali za malisho bora ili kunusuru mifugo yao wakati wa ukosefu wa…
Tunaomba radhi kwa kutokusikika hewani
Ndugu msikilizaji na mfuatiliaji wa vipindi vya radio vya Mkulima Mbunifu/SAT, tunaomba radhi kutokana na kipindi chetu kilichokusudiwa kurushwa hewasi siku ya jumamosi tarehe 30 Oktoba 2021 kutokusikika. Hii ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Sasa kipindi hicho cha kilimo kilichokuwa kinahusu kilimo mseto na kilimo cha mzunguko wa mazao kitarushwa upya siku ya jumamosi ya tarehe…







