Katika kilimo, matumizi ya Molases ni muhimu kwa kuboresha hali ya udongo, kdhibiti wadudu, kuwezesha udongo kuwa na rutuba, kurekebisha hali ya udongo na pia kupunguza matatoizo kwa mimea inayopandikizwa. Matumizi ya Molases husaidia kusafisha mipira ya umwagiliaji. Utafiti unaonyesha kuwa Molases husaidia kuboresha ubora wa udongo. Matumizi na kiasi cha kutumia Kuboresha umbile la udongo molases husaidia kuboresha udongo…
Mifugo
Nyasi aina ya Boma ni chakula kizuri kwa ng’ombe
Nyasi ni rahisi kukua na endapo yatatunzwa vizuri, hukuhakikishia uzalishaji wa hali ya juu wa maziwa. Nchini Tanzania, eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya malisho, bado ni dogo ikilinganisha na umuhimu unaoweza kuwepo kwenye uzalishaji wa maziwa kutokana na kuwa na eneo la malisho. Matete na nyasi ni moja ya malisho muhimu, yanayotoa kiasi kikubwa cha malisho kwa ajili ya…
Namna ya kuwavutia nyuki kuingia mzinga mpya
Tatizo kubwa linalowakabili wakulima wanaotaka kuanzisha ufugaji wa nyuki ni mzinga mpya kukaa muda mrefu bila nyuki. Tatizo hili linapotokea ni vizuri kuzingatia yafuatayo; Weka nta kwenye mizinga yako. Weka mizinga yako katika hali ya usafi na kusiwe na wadudu. Nyuki hawapendi mzinga mchafu. Hakikisha hakuna siafu wala panya wanaoishi kwenye mzinga. Ning’iniza mzinga msimu ambao kuna makundi mengi ya…
Ndege wenye manufaa kwa mkulima
Ufugaji wa bata na bata mzinga hauonekana kuwa si kazi yenye manufaa sana kwa mfugaji. Ingawa ndege hawa ni rahisi sana kuwalisha kwa kuwa huwa wanakula majani na magugu ya aina nyingi. Bata mzinga wanaweza kutumika kama walinzi kwa kuwa ni wakali sana, mtu mgeni anapoingia katika eneo lao. Bata hula wadudu kama konokono na babaje kwenye vitalu vya mbegu.…
Mambo msingi ya kuzingatiwa katika utunzaji bora wa mazingira
Mabadiliko ya tabia nchi yamekuwa ni Dhahiri na hatarishi kwa Maisha ya binadamu kila uchwao. Hii inatokana na uduni katika kutunza mazingira yetu, ambayo kwa kiasi kikubwa yanatawaliwa na miti. Ili kutunza mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, ni muhimu kahakikisha kuwa katika mazingita yetu, imepandwa miti ya kutosha na kutunzwa vyema. Yafuatayo ni mambo muhimu katika upandaji…
Unafanya nini msimu huu wa mvua
Unakumbuka vile ng’ombe walivyokufa msimu wa ukame/kiangazi. Ulijiuliza ni kutokana na nini na je, msimu huu wa mvua unakusaidia vipi kujikinga na athari za kiangazi kwa msimu ujao. Hakikisha unafanya uzalishaji wa malisho kwa wingi msimu huu wa mvua kwa ajili ya kujikinga na athari za ukame. Je, umefikiia kuhusu malisho ya mifugo au umefikiria kuhusu kupunguza idadi ya mifugo.…
Ubora wa maziwa unatokana na usafi na utunzaji
Maziwa ni sehemu ya mlo kamili wenye virutubisho vya kutosha au viini lishe sawia vinavyohitajika katika mwili wa binadamu. Katika toleo lililopita, tulizungumzia kwa ufupi sana kuhusu usafi wa maziwa na mada hii tutaikamilisha kwa kueleza kwa undani vipengele kadhaa vinavyohusiana na usafi wa maziwa. Maziwa ni nini Maziwa ni maji meupe yenye viini lishe yanayokamuliwa kutoka kwenye mifugo mbalimbali…
Jifunze kutengeneza chakula cha kuku mwenyewe
Vyakula vya kuku vinaweza kupatikana madukani au kutengenezwa na mfugaji mwenyewe. Ili kuku aweze kukua haraka na kutoa mazao mengi na bora ni lazima chakula kitengenezwe katika mchanganyiko wenye uwiano mzuri uliopendekezwa. Chakula cha kuku ni lazima kiwe na viinilishe muhimu kama vile protini, wanga, madini na vitamini. Hakikisha chakula unachotengeneza kina mchanganyiko ufuatao: Vyakula vya kujenga mwili kama vile…
Uliza kuhusu samaki kama una changamoto unayopitia kwenye mradi wako
Kanyalo anauliza:Naomba kujua ni wakati gani ninatakiwa kubadili maji katika bwawa ikiwa maji ninayotumia ni ya kujaza? Muda wa kubalisha maji kwa kawaida siwezi kusema moja kwa moja ni baada ya muda kadhaa ila naomba unielewe kuwa uchafukaji wa maji katika bwawa inategemea na utunzaji katika bwawa lako. Mfano; ukilishia vyakula ambavyo sio sahihi kwa samaki huenda ukalazimika ukabadilisha maji…
Namna ya kutunza mifugo wakati wa msimu wa mvua
Ni ukweli usiopingika kwamba msimu wa mvua ni mzuri kwa ustawi wa mifugo. Hii ni kutokana na ongezeko la malisho kwa mifugo hasa kwa wafugaji wanaojishughulisha na ufugaji wa mifugo kama vile ng’ombe, kuku, sungura, mbuzi, kondoo, nguruwe, punda n.k. Msimu wa mvua kwa wafugaji huambatana na changamoto zisizo rafiki kwa maisha ya mifugo. Hii ni pamoja na magonjwa na…





