Muda wa kumlisha au kumnywesha ndama unatakiwa uwe sawa kila siku na joto la maziwa lisibadilike, liwe hilohilo kila siku. Aidha, unyweshaji wa maziwa sharti ufanywe katika hali ya usafi ili kuondoa uwezekano wa ndama kuharisha au kupata ugonjwa wa pneumonia na magonjwa mengine. Tahadhari za kuchukua wakati wa kumnywesha ndama Hakikisha maziwa unayomlisha ndama hayajazidi kiwango kinachostahili ndama kulisha…
Mifugo
Namna ya kupata faida kutokana na uzalishaji wa maziwa
Wafugaji huzalisha maziwa na kuyauza moja kwa moja sokoni na mara nyingi maziwa hayo huweza kusalia kwa kukosa wanunuzi. Maziwa hayo kutumika kwa matumizi ya nyumbani na wakati mwingine huweza kuharibika na kupelekea kumwaga. Hii imekuwa changamoto na kusababisha hasara kwa wafugaji. Katika makala mbalimbali zilizopita tumejaribu kueleza namna ya kuzalisha maziwa kwa wingi. Pia jinsi ya kufanya usindikaji. Kuna…
Umuhimu wa maji katika mnyororo wa ongezeko la thamani
Kwa muda mrefu sasa sehemu kubwa ya nchi ya Tanzania imekumbwa na ukame. Hali hii imefifisha kwa kiasi kikubwa shughuli za wakulima na wafugaji kwa kuwa asilimia kubwa hutegemea mvua. Kama wasemavyo maji ni uhai sio kwa binadamu peke yake, hata kwa wanyama na mimea pia. Kwa mkulima kutegemea mvua hawezi kuwa na kilimo cha kibiashara kwa kuwa hana uhakika…
Chukua hatua kuboresha udongo ili kuinua kilimo hai
Uelewa wa mahitaji ya mimea humwezesha mkulima kuchukua hatua kuimarisha udongo ili kulisha mimea na kuongeza mavuno. Katika kilimo, rutuba kwenye udongo na upatikanaji wa maji ni mambo muhimu ya kuzingatia kwani huweza kuathiri uzalishaji, usalama wa chakula, na wa mazingira. Hivyo basi, mkulima anapotunza udongo anatarajia kwamba udongo huo utaweza kulisha mimea na kuzalisha mimea, inayoweza kustahimili magonjwa, athari…
Athari za ukame kwa mifugo na namna ya kukabiliana nayo
Ukosefu wa mvua umeathiri wafugaji na mifugo yao kwani maeneo ya malisho yanakauka na maji hayapatikani. Hii imepelekea maeneo mengi ya malisho kukauka na pia wafugaji wengi kuhama na mifugo yao ili kutafuta maeneo yenye maji na malisho. Athari za ukame zimeonekana wazi katika maeneo mengi ya wafugaji. Mifugo kukonda, afya za mifugo imezidi kuwa mbaya kutokana ukosefu wa…
Biovision Foundation visit to Tanzania [Mkulima Mbunifu]
MkM project had an opportunity to meet with Biovision foundation, the donors of FCP program [Dr. Franklin Eyhorn [Executive Director] and [Martin Schmid] Co-Head Development Projects on 14th and 15th March 2022. The team selected farmer groups and partners to visit [within Arusha and Kilimanjaro] to allow for Biovision Foundation explore the project engagement with different partners and how useful has been…
Fahamu maandalizi muhimu kabla ya nguruwe kuzaa
Nguruwe wanaozaa kwa mara ya kwanza wanaweza kupelekwa kwenye nyumba ya kuzalia masaa machache kwa siku kutoka siku kumi kabla ya siku ya kuzaa ili waweze kuzoea mazingira. Mara nyingi tumekuwa na makala zinazoelezea ufugaji wa nguruwe katika nyanja tofauti, ikiwa ni pamoja na aina, matunzo na magonjwa ya nguruwe na hata bidhaa zinazotokana na nguruwe na usindikaji wake. Katika…
Kinga dhidi ya magonjwa
Magonjwa yaenezwayo na kupe Ndigana kali, ndigana baridi, kukojoa damu na moyo kujaa maji. Kinga: Ogesha wanyama wako kwa kutumia dawa ya kuua kupe mara moja kwa wiki. Magonjwa yaenezwayo na mbung’o Ndorobo ni ugonjwa mkuu uletwao na mbung’o Kinga: Wachanje ng’ombe kwa kutumia dawa iitwayo samorini kila baada ya miezi mitatu. Magonjwa yasababishwayo na virusi Ugonjwa wa midomo na…
Dondoo muhimu za ufugaji bora wa ng’ombe
Ng’ombe ni mifugo ambayo inategemewa sana na wananchi walio wengi hapa nchini. Kuna aina tatu za ng’ombe wafugwao hapa nchini ambayo ni ng’ombe wa kisasa, kienyeji, na machotara. Zifuatazo ni faida zipatikanazo na ufugaji wa ng’ombe Chakula kama vile maziwa na nyama Mbolea Ngozi ambayo hutumika kama malighafi kutengeneza, viatu, mikanda, mikoba, nguo na vitanda Kujipatia pesa, pia ni akiba…
Chakula rahisi kwa utunzaji wa nguruwe wadogo wanaokuwa
Nguruwe ni mnyama anaeweza kuishi sehemu za vijijini kwani mijini kule wengi huwa hawapendelei sanaana ufugaji huu. Nguruwe hubeba mimba kwa muda wa miezi mitatu na wiki mbili. Ili kuwa na ufanisi na kwa gharama ndogo, mfugaji anapaswa kuzingatia matunzo na kufahamu njia sahihi za ulishaji wa nguruwe wadogo, ili waweze kukua kwa haraka. Mfugaji anaweza kutumia malighafi zifuatazo ili…