Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kuwa nyuzi za mihogo zinaweza kutumika kwa ajili ya chakula cha kuku wanaotaga. Sekta ya kuku hapa Tanzania hutegemea nafaka pamoja na jamii ya kunde kwa ajili ya kutengeneza lishe ya kuku. Nafaka kama vile mahindi, mtama, ngano na shayiri ni chanzo kikubwa cha vyakula vya nguvu katika ulishaji wa kuku. Jamii ya kunde kama…
Mifugo
Kwa nini tunafanya kilimo? Falsafa na umuhimu
Kilimo kimekuwepo tangu zama za mababu zetu. Binadamu wa kwanza walipata chakula chao kwenye mazingira yanayowazunguka na kwa juhudi kama uwindaji kabla ya kuanza kulima ardhi, kupanda mazao na kufuga mifugo kama vyanzo vya lishe. Hii ni pamoja na nafaka, mazao ya mizizi, karanga, matunda, nyama, maziwa, na hata mayai. Kilimo kimebadilisha maisha na maisha pia yamebadilisha muundo wa kilimo.…
Uzoefu husaidia kutambua mnyama anapokuwa kwenye joto
Uzalishaji wenye faida kwa ng’ombe wa maziwa huhitaji uangalizi wa karibu, unaowezesha kutambua ni wakati gani ng’ombe ana joto, hivyo kufanya uhamilishaji kwa wakati unaotakiwa. Kushindwa kutambua joto ni chanzo kikubwa cha urutubishaji hafifu. Mbali na Tanzania, kulingana na utafiti uliofanywa na chuo cha PennState huko Marekani, takriban nusu ya joto hushindwa kutambulika katika uzalishaji wa maziwa nchini humo. Hata…
Fuga kondoo kisasa uboreshe pato lako
Kwa siku za nyuma, jumla ya idadi ya kondoo wanaofugwa hapa nchini Tanzania ilikaribiana kuwa sawa na idadi ya mbuzi nchini kote. Kwa sasa, idadi ya kondoo imepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na idadi ya mbuzi. Hii imetokana na wafugaji kuhamishia mapenzi yao kwenye ufugaji wa mbuzi. Kama walivyo mbuzi, kondoo pia wanaweza kufugwa na wafugaji wadogo wadogo na kwenye…
Ulishaji wa majani machanga ni hatari kwa afya ya mifugo
Mabadiliko ya hali ya hewa ni jambo muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku, hata katika ufugaji mabadiliko haya ya hewa yanaweza kuleta athari katika mifugo yetu. Ukame wa muda mrefu unasababisha kupungua au kuisha kwa malisho ya wanyama. Majani machanga ni yapi Majani machanga ni yale yanayo chipua baada tu ya mvua kunyesha. Majani haya ni hatari sana…
Sumu zinazoweza kuathiri mbuzi
Pamoja na kuwa kuna magonjwa mengi yanayoweza kuathiri mbuzi, pia sumu zinazopatikana katika baadhi ya miti, mimea, dawa au hata wanyama, huweza kusababisha mbuzi kufa mara atakapokula. Baadhi ya sumu zinazoweza kusababisha mbuzi kufa ni kama zifuatayo; 1. Sumu ya lukina Mmea huu una sumu iitwayo mimosine, ambayo ikiliwa kwa kiasi kikubwa huleta madhara kwa mbuzi. Dalili Mbuzi aliyekula sumu…
Mazao ya kilimo hai yanahitaji virutubisho vya asili
Kabla ya yote, ni muhimu mkulima kujiuliza na kufahamu ni namna gani virutubisho vya asili vya mimea hufanya kazi? Mimea ya kijani ina uwezo wa kufanya (photosynthesis). Mwanga wa jua, hewa ya ukaa pamoja na maji huzalisha chakula cha mimea aina ya wanga, ambacho baadaye husafirishwa sehemu mbalimbali za mimea na kuhifadhiwa kwa namna ya wanga (carbohydrates). Chakula hicho hutumiwa…
Mabaki ya mazao yanaweza kuwa malisho wakati wa kiangazi
Mabaki ya mazao ndicho chakula halisi kinachotumika kwa malisho wakati wa kiangazi katika nchi za ukanda wa tropiki, ila ubora wake ni mdogo sana. Ng’ombe wa maziwa huwa wanateseka kwa kutopatiwa chakula cha kutosha, na matokeo yake ni kuzalisha kiwango kidogo cha maziwa, uwezo mdogo wa kuzaliana, kuwa na uzito mdogo, ndama kufa au kuwa na umbo dogo na dhaifu,…
Fahamu namna ya Kuandaa na kupanda mbegu za miembe
Mimi ni msomaji wa jarida la Mkulima mbunifu, nimejifunza mengi, lakini natamani kufahamu namna ya kuandaa na kupanda mbegu za miembe – Msomaji MkM Wakulima walio wengi nchini Tanzania, wamekuwa wakipanda aina mbalimbali za miti ya matunda, bila kuzingatia kanuni na taratibu za upandaji wa miti hiyo, jambo ambali limekuwa likiwasababishia hasara kwa kuwa na miti isiyokuwa na tija. Ni…
Funza walisha kuku: Ubunifu mpya wa asili kwa wafugaji
Funza ni nini? Funza ni aina ya wadudu ambao wanapatikana kwenye mbolea ya samadi inayotokana na mifugo kama vile ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Funza wanazalishwa kutokana na nini Wadudu hawa wanaweza kuzalishwa kutokana na kinyesi cha wanyama kama vile ng’ombe, mbuzi, kondoo, na nguruwe kwa kuchanganywa na tope chujio linalotokana na mtambo wa biyogesi (biogas). Sehemu ya kuzalishia wadudu…