TERMS OF REFERENCE (TOR) FOR PRINTING MKULIMA MBUNIFU MAGAZINE ABOUT MKULIMA MBUNIFU (MkM) Mkulima Mbunifu (MkM) Magazine is a Farmer Communication Programme project that is implemented in Tanzania since July 2011 with support from Biovision Foundation, Switzerland and Biovision Africa Trust (BvAT), Nairobi, Kenya. The publication aims to provide information to smallholder farmers to enable them adopt improved sustainable agriculture…
Mifugo
Mkulima Mbunifu imenihamasisha kuanza kufanya kilimo hai
“Nimeamua kuanza kufanya kilimo hai kwani ni rahisi, sitatumia dawa za kemikali wala mbolea za viwandani. Nilikua nikifanya kilimo cha mazoea bila kujali afya yangu na watu wengine. Sikufahamu madhara kwa mazingira yani ardhi, mimea na hata wanyama”. Hayo ni maneno ya Godwin Zakaria Axwesso (52) anayeishi kijiji cha Bashay, wilaya ya Karatu Mkoa wa Arusha. Alifanya kilimo cha kawaida…
Je, unafahamu umuhimu wa njia za moto?
Hivi karibuni tumeshuhudia uwepo wa mlipuko wa moto katika sehemu mbalimbali hapa nchini, na katika nchi nyingi duniani. Hii inatokana na mabadiliko ya tabia nchi na utunzaji hafifu wa mazingira yetu. Ni jambo lisilopingika kuwa wakulima wamekuwa na bidii sana katika kuhakikisha kuwa wanazalisha na kupata chakula pamoja na kipato kwa ajili ya familia zao. Halikadhalika wakulima wamekuwa mstari wa…
Kilimo bora cha kabeji ya kichina
Kabeji ya kichina kwa miaka mingi ilikuwa inalimwa na kuliwa sana katika nchi za China, India na Japani. Ikijulikana kwa majina ya common choy, pak choy na gai choy au Indian mustard. Miaka ya karibu mboga hii ya majani imepata umaarufu katika nchi yetu na hulimwa kwa ajili ya kuboresha lishe na kama zao la biashara, lijulikanavyo katika maeneo mengi…
Fahamu namna ya kufanya ufugaji wa nyuki wadogo
Nchini Tanzania na maeneo mbalimbali barani Afrika, imekuwa ni mazoea kwa wanaotaka kufanya ufugaji wa nyuki kufuga nyuki wakubwa au maarufu kama nyuki wakali. Aina hii ya nyuki imekuwa ni rahisi kufugwa kwa kuwa uzalishaji wake ni mkubwa zaidi na wanaweza kufugwa kwenye maeneo tofauti tofauti ili mradi kuwe na mahitaji muhimu yanayowawezesha nyuki kuzalisha. Nyuki wakubwa wanaweza kufugwa katika…
Ni muhimu wazalishaji wa maziwa kujiunga kwenye vyama vya ushirika
Wakulima na wafugaji wanashauriwa kuwa katika vikundi au vyama vya ushirika ili kukuza na kupanua kilimo biashara. Ushirika ni biashara zinazojikita kwa watu; zinamilikiwa, zinadhibitiwa na zinaendeshwa na wanachama na kwa madhumuni ya kufikia mahitaji na malengo yao ya pamoja, ya kiuchumi, kijamii, na kitamaduni. Kupitia vyama vya ushirika, wakulima wanaweza kuokoa pesa kutokana na gharama za usafiririshaji wa maziwa…
Siku ya tokomeza gugu karoti Arusha (2020)
Athari za gugu karoti na mbinu za kukabiliana nalo Gugu karoti ambalo kitaalamu linajulikana kama (Parthenium hysterophorus) ni mmea vamizi ambao una athiri binadamu, mazao, wanyama au mifugo pamoja na kuharibu uoto wa asili. Nchini Tanzania, gugu karoti limegundulika au kuonekana kuwepo tangu mwaka 2010 katika mkoa wa Arusha hasa maeneo ya pembezoni mwa baadhi ya barabara, na baadaye kuanza…
Nini husababisha magonjwa kwa mifugo
Magonjwa mengi ya mifugo husambazwa na vijidudu ambao huingia kwenye mfumo wa damu na kusababisha homa na baadae madhara makubwa. Mangonjwa mengi ya mifugo husababishwa na vyanzo kutoka nje ya mwili wa mnyama mfano mazingira machafu anayoishi mnyama, vitu vinavyosababisha vidonda na ambazo vimelea vinaweza kukaa. Pia mnyama anaweza kupata ugonjwa kutokana na hali za ndani ya mwili kama upungufu…
Zikaushe mboga za ziada kwa matumizi ya baadaye
Kukausha mavuno kutoka shambani mwako, ni njia nzuri zaidi kukuwezesha kukabiliana na hali ngumu. Kukausha mboga na matunda ni njia rahisi sana ya uhifadhi inayotumika duniani kote. Hata hivyo, ili kupata matokeo mazuri na bora, baadhi ya kanuni ni lazima zifuatwe. Kukausha kwa jua Jua hutumika kwa mazao ambayo hayaharibiki yanapokaushwa kwa kutumia jua moja kwa moja, mfano maharagwe, karanga…
Vuna zaidi kwa kutumia mbinu ya tumbukiza
Tumbukiza ni mbinu inayofaa katika eneo ambalo ni kame na lisilokuwa kame. Ni mbinu ya kuhifadhi maji, na kutoa mavuno mengi zaidi. Ni mbinu ambayo imepokelewa kwa kiasi kikubwa na wafugaji wa ng’ombe wa maziwa kutoka sehemu ambazo wana eneo dogo kwa ajili ya uzalishaji wa malisho. Ni ufumbuzi ambao umeonekana kuleta ongezeko la uzalishaji wa matete kwa asilimia 20…






