- Mifugo

Nini husababisha magonjwa kwa mifugo

Sambaza chapisho hili

Magonjwa mengi ya mifugo husambazwa na vijidudu ambao huingia kwenye mfumo wa damu na kusababisha homa na baadae madhara makubwa.

Mangonjwa mengi ya mifugo husababishwa na vyanzo kutoka nje ya mwili wa mnyama mfano mazingira machafu anayoishi mnyama, vitu vinavyosababisha vidonda na ambazo vimelea vinaweza kukaa.

Pia mnyama anaweza kupata ugonjwa kutokana na hali za ndani ya mwili kama upungufu wa lishe, mfano; madini, na na magonjwa ya kurithi.

Upungufu wa viinilishe katika chakula cha mifugo husababisha madhara katika mwili.

Madhara hayo ni kama vile majike kutopata joto mapema, ndama kuzaliwa na viungo visivyo komaa, upungufu wa uzalishaji maziwa na kiwango cha uzalishaji kushuka

Kutokuzingatia usafi kwenye banda la ng’ombe, pamoja na kusafisha kiwele vizuri kabla na baada ya kukamua, mkamuaji mwenye kucha ndefu na ambaye hajasafisha mikono vizuri kabla ya kumkamua ng’ombe pia ni chanzo kikubwa cha kueneza magonjwa.

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *