Kilimo

- Kilimo, Kilimo Biashara, Masoko

Udhibiti wa wadudu na magonjwa katika kilimo hai

Katika uzalishaji wa mazao kwa misingi ya kilimo hai ambacho ni aina ya kilimo kinachozingatia usalama wa chakula na kuondokana na matumizi ya kemikali za viwandani changamoto ya magonjwa na wadudu pia hutokea, jambo linalohitaji usimamizi mzuri ili kuleta uzalishaji wenye tija. Faida ya kuzalisha kwa misingi ya kilimo hai hasa katika kukabiliana na magonjwa na wadudu ni kuwa njia…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara, Masoko, Mazingira, Mifugo, Redio, Usindikaji

MKULIMA MBUNIFU INTERN ADVERT

S.L.P 14402, Arusha, Tanzania Simu :+255 (0) 0714 266 0007 Barua pepe: info@mkulimambunifu.org TERMS OF REFERENCE FOR MKULIMA MBUNIFU INTERN Mkulima Mbunifu is seeking to recruit suitably qualified intern to support MkM work in content development and distribution of MkM magazine. The intern will also support monitoring activities of the project, data management and feedback from users of knowledge products…

Soma Zaidi

- Kilimo, Kilimo Biashara, Masoko

Fursa ya kibiashara kwa misingi ya Kilimo hai

‘’Mimi ni mkulima wa mfano, ninazalisha mazao mbalimbali kwa misingi ya kilimo hai na nimefaidika sana’’. Hayo ni maneno ya mkulima wa kilimo hai, Bw. Michael Laizer (73), toka Kijiji cha Emaoi, Ngaramtoni, mkoani Arusha ambaye anajishughulisha na uzalishaji wa mazao ya biashara kwa misingi ya kilimo hai. Bw. Laizer, ambaye jina la kibiashara linalotambulika kama nembo kwenye bidhaa zake…

Soma Zaidi

- Kilimo, Masoko

Mkulima atumia kilimo hai kujiendeleza baada ya kustaafu

“Naitwa Felister Mangalu (64) mkulima wa kilimo hai. Nilikua mfanyakazi wa serikali na nikastaafu mwaka wa 2019. Kabla ya kustaafu nilikuwa nikijiuliza maswali kuhusu nini nitafanya ili kuendelea kujikimu kimaisha endapo muda wangu wa ajira ukiisha. Najua hili ni swali ambalo watu wengi hujiuliza wakiwa na sababu kama zangu. Hata hivyo, najua tumejaliwa vipawa mbalimbali na tuna uwezo tofauti tofauti.…

Soma Zaidi

- Kilimo, Masoko

Soko la mazao ya kilimo hai Tanzania

Ingawa taasisi nyingi zinasisitiza kilimo hai nchini Tanzania, kuna walaji wachache sana walio na uelewa wa bidhaa za kilimo hai. Soko la mazao ya kilimo hai lipo tu na kufahamika katika miji mikubwa kama vile Dar es Salaam na Arusha, na mashirika machache yaliyoidhinishwa katika kuuza mazao kwa misingi ya kilimo hai kwa ajili ya soko la ndani na hata…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo

Zingatia lishe sahihi na mifumo endelevu ya uzalishaji wa chakula salama

Tunapozungumzia lishe tunamaanisha kupata kiasi na ubora wa chakula na maji kwa vipindi vinavyofaa ili kuruhusu mwili kufanya kazi vizuri “balanced diet” yaani mlo kamili. Mahitaji ya lishe hutofautiana kulingana na jinsia, umri, shughuli za kila siku, ujauzito/kunyonyesha na hali ya afya ya mtu binafsi. Chakula kinapovunjwa, hutoa nishati ya kujenga mwili na kuupa kinga. Nishati hupimwa kwa kilokari au…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara, Kutuhusu, Mazingira, Mifugo, Mimea, Redio, Shuhuda, Usindikaji

Taarifa: Mkulima Mbunifu ni mara moja kwa miezi miwili tangu sasa

Mwaka umeanza ukiwa na baraka tele na habari njema kwa wakulima na wasomaji kwa ujumla. Kuanzia mwezi huu jarida lako ulipendalo la Mkulima Mbunifu (MkM) litakuwa likichapishwa na kuletwa kwako kila baada ya miezi miwili. Tangu jarida hili lilipozinduliwa mwezi Julai 2011, limekuwa likichapishwa na kusambazwa kwa wakulima kila baada ya miezi miwili. Hata hivyo sababu ilikua ni kujenga msingi…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mazingira

Panda miti kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabia nchi

Wakulima wanaweza kuchangia uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti na kutumia mbinu za kilimo hai. Kupanda miti ina manufaa nyingi ikiwa ni pamoja na kutunza mazingira, kuwa chanzo cha malisho ya mifugo, asali, mbao, na hewa safi. Kipindi kirefu cha ukame ambacho kimeripotiwa katika kanda hii ya Afrika Mashariki imesababisha maeneo mengi kuwa kavu na hata ardhi kumomonyolewa na upepo…

Soma Zaidi

- Kilimo

Weka mipango thabiti kwa kuzalisha kibiashara

Kilimo kinachangia kwa kiasi kikubwa kutoa ajira, na mchango mkubwa katika kuondoa umasikini, hasa katika nchi zinazoendelea, nyingi zikiwa Barani Afrika. Hivi sasa kuna msukumo mkubwa kutoka kwa serikali na wadau mbalimbali wanaohimiza wakulima kuangali kilimo katika mtizamo wa kibiashara. Kwamba, wakulima wasizalishe tu kwa minajili ya chakula. Kuanzisha kilimo cha biashara ni tofauti na kulima tu kawaida, kupanda na…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo

Bustani ya nyumbani inaweza kukukwamua kiuchumi na kuboresha afya yafamilia

Bustani ya nyumbani, ni eneo dogo lililokaribu na nyumba linaloandaliwa na wanafamilia na kupandwa mazao mbalimbali ya mbogamboga kwaajili ya familia. Hata hivyo, katika maeneo mengi wanawake ndio wamekua wakijishughulisha na bustani ndogo za nyumbani. Mara nyingi bustani ya nyumbani hujumuisha uzalishaji wa mazao ya muda mfupi hasa mbogamboga kwani ni rahisi kuyahudumia kwa gharama nafuu lakini pia yanazalisha kwa…

Soma Zaidi