Ufugaji wa kuku ni moja ya sekta ambayo imekuwa na faida kwa wafugaji walio wengi, na hata watu ambao wanafanya shughuli nyinginezo, lakini bado hujishughulisha na ufugaji wa kuku. Pamoja na aina hii ya ufugaji kuwa na mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea wafugaji kipato kikubwa, bado inakumbwa na changamoto mbalimbali. Mojawapo ya changamoto hizo ni pamoja na uwepo…
Mifugo
Ugonjwa wa ng’ombe wa mapele ngozi
Ugonjwa wa mepele ngozi, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kisayansi kwa jina la Capri poxvirus. Takribani asilimia 5 hadi 50 ya ng’ombe katika kundi wanaweza kupatwa na ugonjwa huu, ambapo ng’ombe wa umri wowote anaweza kupatwa na ugonjwa huu. Ugonjwa wa mapele ngozi hauambukizwi kwa binadamu. Chanzo cha maambukizi na namna ugonjwa unavyoenea Maji maji yanayotoka kwenye vidonda na…
Tuelimishane kuhusu mradi wa samaki kwa uzalishaji wenye tija
Ni mazingira gani yanafaa zaidi kwa ufugaji wa samaki! Emma Peter anauliza: Nimefuatilia sana huu ujasiriamali kweli nimevutiwa na ningependa kujaribu kufanya. Nina eneo Rukwa lenye maji yakutosha ya asili takribani mita za mraba 2000, naomba ushauri wako Musa, Jinsi ya kuandaa hayo mabwawa na wapi nitapata samaki hasa sato maeneo ya Mbeya au karibu na Rukwa. Musa Said anajibu:…
Namna ya kuhifadhi mahindi kulinda ubora na kukidhi mahitaji ya chakula
Mahindi ni zao la kwanza katika mazao makuu ya nafaka hapa nchini. Huzalishwa kwa wastani wa tani 2393000 kwa mwaka ambayo ni sawa na asilimia 63 ya mazao yote ya nafaka nchini. Zao la mahindi hulimwa karibu katika mikoa yote, lakini hulimwa zaidi katika mikoa ya Rukwa, Ruvuma, Iringa, Mbeya, Morogoro, Dodoma, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Tanga, Mwanza na Shinyanga. Licha…
Karibu maonyesho ya Nane Nane 2020
Kama ilivyo ada kila mwaka nchini Tanzania, wakulima hujumuika pamoja kusherehekea wiki ya kitaifa ya kilimo ambayo hufanyika kikanda nchini Tanzania. Maonyesho hayo mahususi hutoa fursa kwa wakulima kufahamiana na kuonesha bunifu mbalimbali, nyenzo za kilimo, usindikaji na masoko ya bidhaa mbalimbali za kilimo. Mwaka huu maonyesho hayo yatafanyika kitaifa mkoani Simiyu, Mkulima Mbunifu itashiriki kikamilifu hivyo usiache kututembelea katika…
Fahamu na dhibiti ugonjwa wa Coenurosis
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na viluwiluwi vinavyojulikana kitaalamu kwa jina la Coenurusis Cerebralis unaoshambulia mfumo wa fahamu wa kati (ubongo na uti wa mgongo) wa mbuzi na kondoo. Chanzo cha viluwiluwi Viluwiluwi vya ugonjwa huu vinatokana na minyoo aina ya tiniamaltisepts iliyopo katika utumbo wa mbwa au wanyama pori jamii…
Zalisha bilinganya nyeupe kuongeza pato na lishe
Bilinganya nyeupe (Long White Eggplant) ni moja ya zao la mbogamboga ambalo lina viini lishe vingi na muhimu kama vile madini aina ya chokaa na chuma, Vitamini A, B na C, wanga, protini na maji. Kisayansi zao hili hujulikana kama Solanum Melongenai na kilimo chake huweza kufanyika katika majira yote ya mwaka. Hali ya Hewa Zao hili huhitaji hali ya…
Jifunze namna ya kuhifadhi mazao ya mikunde baada ya mavuno
Kabla mkulima hajavuna mazao yake, ni vyema akatambua namna ya kuyahifadhi kwa lengo la kuhakikisha zao linabaki katika ubora wake kwa muda mrefu. Kwa nini kuhifadhi Mazao yanapovunwa, ni vyema kuhifadhiwa ili kuhakikisha usalama wa chakula katika kaya na taifa kwa ujumla. Kuweka akiba kwa matumizi ya baadaye au kuhifadhi kwa ajili ya matumizi ya mbegu. Mikunde huhifadhiwa kwenye maghala…
Usisafirishe kuku kwa kuwarundika au kuning’iniza kichwa chini
Kumekuwa na tabia ya wafugaji walio wengi kutokuzingatia njia sahihi ya kusafirisha kuku wakati wa kupeleka sokoni au hata kuhamisha toka sehemu moja kwenda nyingine. Hali hii imekuwa ikisababisha mateso pamoja na vifo kwa kuku jambo ambalo pia husababisha hasara. Ni vizuri kuku wakawekwa kwenye tenga au trei yenye nafasi na hewa ya kutosha. Haifai kubananisha kuku kwenye sehemu moja.…
Ubora wa zizi huinua uzalishaji wa mbuzi na kondoo
Ufugaji wa Mbuzi na kondoo ni wa gharama nafuu sana hasa ukilinganisha na ng’ombe kwani wanyama hawa wana uwezo wa kuishi mahali popote na katika mazingira magumu kama yenye maradhi na ukame. Wanyama hawa kulingana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo huku wakihudumiwa na familia zenye nguvu kazi ndogo na kipato cha chini. Wanyama hawa ambao hufugwa…