Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Vipande vya vitu au sehemu za viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda…
Kilimo
Matumizi ya Molasi na faida zake kwa uzalishaji wa mazao
Katika kilimo, matumizi ya Molasi ni muhimu kwa kuboresha hali ya udongo, kudhibiti wadudu, kuwezesha udongo kuwa na rutuba, kurekebisha hali ya udongo na pia kupunguza matatizo kwa mimea inayopandikizwa. Matumizi ya Molasi husaidia kusafisha mipira ya umwagiliaji lakini pia utafiti unaonyesha kuwa Molasi husaidia kuboresha ubora wa udongo. Matumizi na kiasi cha kutumia Kuboresha umbile la udongo. Molasi…
Zao lenye faida kubwa kiuchumi na kiafya
Nanasi ni moja kati ya matunda ambayo yanapendwa sana na watu wa kada zote. Tunda hili halihitaji gharama kubwa ya uzalishaji, huku likiwa na bei nzuri tofauti na ilivyo kwa aina nyinginezo za matunda. Nchini Tanzania, zao hili hulimwa zaidi katika maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Geita, Mwanza, Tanga, Mtwara, Lindi, Zanzibar na maeneo mengine. Zao hili lina kiasi kikubwa…
Mkulima Mbunifu inazidi kupenya katika vijiji kuwafikia wakulima wadogo
Mhariri wa jarida la Mkulima Mbunifu Erica Rugabandana (Wa kwanza kulia waliosimama) baada ya kutembelea kikundi cha wakulima wanufaika wa jarida la MkM wilayani Lushoto
Wasemavyo wanufaika wa jarida la Mkulima Mbunifu
Mkulima Mbunifu imekua ikitembelea wakulima mbali mbali nchini Tanzania ili kuchukua shuhuda mbalimbali za wanufaika na kuzichapisha ziwe chachu kwa wasomaji wengine kujifunza na kufanya kwa vitendo. Je wewe umejifunza nini kutoka Mkulima Mbunifu? Tafadhali tuandikie kupitia mawasiliano yaliyo katika jarida hili. Bwana Santony Yasenti, Nangara – Babati. Ninapenda kutoa shukrani zangu kwa gazeti la Mkulima Mbunifu, nimejifunza mengi kupitia…
Umuhimu wa kulima kiazi sukari (beetroot)
Katika zama za kale, beetroot (kiazi sukari/ bitiruti) ilikuwa ikitumika kama dawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali kama kuvimbiwa, majeraha pamoja na matatizo mbalimbali ya ngozi (mizizi ndiyo iliyokuwa ikitumika). Hadi kufikia karne ya 16 zao hili lilikuwa tayari limekwishapata umaarufu hasa katika Amerika ya Kati na Ulaya ya Mashariki na baadaye kupokelewa katika nchi zingine kama Roma, Ufaransa,…
Dhibiti magonjwa na wadudu kwa kutumia dawa za asili
Madawa ya asili Hizi ni dawa zinazotokana na mimea ambayo hupatikana katika maeneo ya wakulima. Matumizi ya dawa hizi ni njia mojawapo ya kuepuka dawa za viwandani ambazo huathiri udongo, mazingira na afya za watu na wanyama. Hadi sasa kuna dawa takribani 67. Madawa yasipotengenezwa vizuri na kutumiwa ipasavyo yanaweza yasifanye kazi ipasavyo, hivyo huwa ni vigumu kuwashawishi wakulima kuzitumia.…
Namna ya kusindika korosho mara baada ya kuvuna
Korosho ni zao lenye matumizi mengi sana, lakini kubwa kuliko yote ni kwamba kuliwa kama kitafunwa (snacks) wakati wa kunywa chai, juisi, maziwa au kahawa. Makala hii inakusudia kutoa mafunzo ya namna ya kuandaa korosho kwa matumizi ya nyumbani. Hii itawasaidia wakulima wapya wa mikoa hasa iliyoingia kwenye uzalishaji wa zao hili kwa mara ya kwanza. Jinsi ya kuandaa korosho…
Kilimo hai kinachangia uzalishaji katika Kilimo
Tanzania ina ardhi yenye rutuba inayowezesha shughuli za kilimo hai kukua na kuongeza kipato kwa wakulima wadogowadogo. Hii inaweza kufanyika kwa kutumia teknolojia mpya inayoweza kusaidia kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo mbayo yamezalishwa kwa kutumia kilimo hai, kwa ajili ya soko la ndani na la nje. Njia tofauti za kilimo Kwa kawaida viumbe hai wote ni wa asili. Fikra…
Lima Giligilani kukuza uchumi kwa haraka
Kilimo cha Giligilani (Coriander) ni mradi mkubwa unaojitosheleza kukuza maisha ya mkulima kutokana na sababu kuwa zao hili la biashara huchukua muda mfupi toka kuotesha hadi kuvuna. Zao hili linalotumika kama kiungo cha chakula katika mapishi ya vyakula mbalimbali kama nyama, supu au mchuzi linafaa kulimwa wakati wowote na katika maeneo mengi ya Tanzania hususani mikoa ya Mbeya na Iringa.…









