Kilimo

- Kilimo, Kilimo Biashara, Mtama, Usindikaji

Unaweza kuongezea thamani Mtama kwa kuzalisha mvinyo

“Kwa karne nyingi, mtama umekuwa ukichukuliwa kama chakula cha watu maskini au chakula cha njaa, hili sasa limegeuka na kutoa matumaini mapya kwa wakulima wa mtama nchini Tanzania” Mtama ni kundi la mbegu ndogo ndogo aina ya mazao ya nafaka, yanayolimwa sana duniani kote kwa ajili ya chakula na lishe. Hii ni aina ya mazao yanayolimwa katika mazingira magumu kama…

Soma Zaidi

- Kilimo

Mahindi zao kuu la chakula linalopendwa na kutumiwa sana

Huu ni mwendelezo wa makala inayokuhusu kilimo cha mahindi kutoka toleo lililopita Inapendekezwa kuweka mbolea baada ya udongo kupimwa. Mbegu ya mahindi iliyoboreshwa inaweza kufanya vizuri inapowekewa mbolea halisi inayohitajika, kulingana na uhitaji wa virutubisho.  Mbolea ya mboji inaweza kuwekwa kwenye shimo wakati wa kupanda. Palizi Hakikisha kuwa, shamba lako halina magugu ambayo hushindana na mazao kupata maji na virutubisho.…

Soma Zaidi

- Kilimo

Ujue mmea wa mnazi pamoja na kanuni za kilimo bora cha zao hili

Minazi ni zao la biashara nchini Tanzania ambalo hulimwa na kustawi zaidi ukanda wa pwani ya Tanzania. Mikoa kama Lindi, Mtwara, Pwani, Dar es salaam, Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba, pia kwa uchache Minazi hulimwa kwenye mikoa ya Mbeya, Kigoma na Tabora. Aina za minazi Kuna aina kuu tatu za Minazi inayolimwa hapa Tanzania nayo ni (i) Minazi…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Mimea

Ijue teknolojia ya vijidudu vidogo vidogo na matumizi yake katika kilimo

Kumekuwa na changamoto kadhaa za kwenye kilimo ikiwemo kukosekana na rutuba magonjwa na wadudu waharibifu. Teknolojia ya EM imekuwa ikitumiwa nchi mbali mbali duniani na pia Tanzania.   Baadhi ya maeneo ya ardhi hayana rutuba kutokana na mambo kadhaa kama vile kulimwa kwa muda mrefu au matumizi ya mbolea za viwandani. Ingawaje mbolea za viwandani zinasaidia kuongeza rutuba, lakini ni…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Mimea

Fahamu aina mbalimbali za viungo muhimu kwa afya ya binadamu

Pamoja na viungo kutumika kuongeza ladha katika vyakula, pia vina manufaa katika mwili wa binadamu. Mara nyingi wakulima wamekuwa mstari wa mbele kuzalisha mazao muhimu kwa manufaa ya jamii, ilhali wao wakijisahau kuwa wanahitaji pia kutumia ili kuimarisha afya zao. Viungo mbalimbali kama tangawizi, vitunguu saumu, vitunguu maji, pilipili na limao ni muhimu katika kuimarisha kinga ya mwili. Je ni…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Kwa nini tunafanya kilimo? Falsafa na umuhimu

Kilimo kimekuwepo tangu zama za mababu zetu. Binadamu wa kwanza walipata chakula chao kwenye mazingira yanayowazunguka na kwa juhudi kama uwindaji kabla ya kuanza kulima ardhi, kupanda mazao na kufuga mifugo kama vyanzo vya lishe. Hii ni pamoja na nafaka, mazao ya mizizi, karanga, matunda, nyama, maziwa, na hata mayai. Kilimo kimebadilisha maisha na maisha pia yamebadilisha muundo wa kilimo.…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Wakulima wanasemaje kuhusu masoko ya mazao ya kilimo hai

Mkulima anaezalisha kwa mazao kwa kufuata misingi ya kilimo hai, Bw. Zadock Kitomari alisema kuwa, unapoanza kujishughulisha na kilimo hai ambacho hakitumii kemikali unaona kuwa uzalishaji unakuwa mdogo lakini kwa kadri unavyoendelea uzalishaji unakuwa mkubwa. Anaeleza kuwa, kilimo hai ni aina ya kilimo kinachoangalia uhai wa mazingira, uhakika na usalama wa mlaji na usalama wa chakula jambo ambalo linamuhakikishia mkulima…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Vijana wanaweza kujifunza mengi kutokana na ubunifu kwenye kilimo hai

Kilimo hai kinafanyika kwa ufanisi na manufaa endapo wakulima wenyewe wanafanya ubunifu kulingana na mazingira yao. Ili kilimo hai kiwe endelevu ni muhimu ubunifu kutoka kwa vijana kutiliwa mkazo. Kilimo kwa kutumia mifuko (viroba) Kilimo cha kutumia mifuko (viroba), ni kilimo kizuri na chenye manufaa kwa wakulima, kwani unaweza kulima sehemu yeyote pasipo kuathiri mazingira. Watu wengi wanakijua kilimo hiki…

Soma Zaidi

- Kilimo

Faida za kufunika udongo katika kilimo

Ni kwa namna gani udongo unaweza kufunikwa wakati wote, wakati shughuli nyingine zinaendelea kwenye udongo huo huo? Hili ni swali muhimu wanalojiuliza wakulima wengi. Hii inategemeana na utunzaji na aina ya shughuli zinazofanyika kwenye udongo huo, na kama shughuli zenyewe zinafanyika kwa kutumia mikono au mashine. Moja ya shughuli ambazo zinasumbua udongo kwa kiasi kikubwa ni kulima kwa kutumia plau.…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Tushirikiane kupata soko la mazao ya kilimo hai

Kwa sasa katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania, ni wazi kuwa shughuli za kilimo hai zimeshika kasi, huku kukiwa na ongezeko la wazalishaji wa bidhaa za kilimo hai. Hili ni jambo jema sana kwa kuwa waswahili wanasema taratibu ndiyo mwendo, na kidogo kidogo hujaza kibaba. Na hapa taratibu tunaona mwanga wa dunia kurudi katika hali yake ya uasili, ya awali…

Soma Zaidi