Matandazo kwa ajili ya kilimo katika msingi wa kilimo hai huweza kutokana na njia mbalimbali kama vile mazao funikizi, mabaki ya mazao, majani kutoka katika miti au vichaka na katika mimea mbalimbali. Ikiwa matandazo yanategemewa kupatikana katika mazao funikizi, basi maandalizi ya eneo la kuoteshea na kukuzia mazao hayo ni lazima ufanyike. Matandazo kutoka katika mazao funikizi Baadhi ya mazao…
Kilimo
Kilimo Hifadhi ni muhimu kwa uzalishaji wenye tija
Kwa muda mwingi nimekuwa nikisikia kuhusu kilimo hifadhi, lakini sielewi na natamani kufahamu. Mnaweza kunieleza kwa ufupi ni nini maana yake na kinafanyikaje?. Shukuru, Msomaji MkM Hili ni swali muhimu sana na ambalo bila shaka wakulima wengi wamekuwa wakiuliza na kujiuliza pia. Ni muhimu kufahamu na kufanya kilimo hifadhi kwani itasaidia katika uhifadhi wa mazingira, ardhi na uzalishaji wa mazao…
Jifunze kutayarisha mboji kwa kurundika malighafi
Naomba kujua namna ya kuzalisha mboji kwa kurundika takataka ili kutumia kwenye bustani yangu ya mbogamboga (Joyce Evance Dodoma, 0763 772655) Mbinu ya kutayarisha mboji kwa kurundika hufaa zaidi kufanyika katika maeneo yanayopata mvua nyingi. Katika maeneo yanayopata mvua kidogo mbinu ya kutengeneza mboji kwa kutumia shimo hupendekezwa na ni njia nzuri zaidi. Ili kufanikisha zoezi la uzalishaji wa mboji…
Jaffer J. Kesowani anasema: Habari Mkulima Mbunifu. Nimeona makala yako ya nyanya pori na nimeazimia kulima. Mtihani niliokutana nao ni wapi nitapata mbegu. Nikaona swali hili nilirudishe kwenu. Mkulima Mbunifu anajibu: Mbegu za nyanya pori zinapatikana madukani kwenye maduka ya pembejeo na zinauzwa kama mbegu zingine. Mkulima anahitajika kununua kulingana na ukubwa wa shamba lake. Nestory Mwangoka anasema: Mkulima mbunifu…
Matumizi ya molases na faida zake kwa uzalishaji wa mazao
Katika kilimo, matumizi ya Molases ni muhimu kwa kuboresha hali ya udongo, kdhibiti wadudu, kuwezesha udongo kuwa na rutuba, kurekebisha hali ya udongo na pia kupunguza matatoizo kwa mimea inayopandikizwa. Matumizi ya Molases husaidia kusafisha mipira ya umwagiliaji. Utafiti unaonyesha kuwa Molases husaidia kuboresha ubora wa udongo. Matumizi na kiasi cha kutumia Kuboresha umbile la udongo molases husaidia kuboresha udongo…
Tumia kilimo cha mzunguko kudhibiti wadudu na magonjwa
Katika kilimo hai kama ilivyo kwa aina nyingine ya kilimo na uzalishaji wa mazao, mara nyingi wadudu na magonjwa vinaweza kuwa moja ya sababu kwa mkulima kukosa mavuno au kupata mavuno hafifu na yasiyokidhi soko lakini pia yasiyokuwa na ubora. Wadudu na magonjwa visipodhibitiwa, humsababishia mkulima hasara kwa kiasi cha asilimia 20 hadi 80. Kutokana na hali hiyo, ni muhimu…
Tumia kitunguu saumu kudhibiti wadudu
Vitungu saumu na vitunguu maji vina manufaa sana katika kukabiliana na aina mbalimbali za wadudu waharibifu na baadhi ya magonjwa. Harufu kali husaidia kuwafukuza wadudu kama vudukari, bungo na hata panya. Saga kitunguu saumu kimoja, changanya kwenye lita moja ya maji na nyunyizia kwenye mazao. Unaweza pia kusaga vitunguu saumu 3, kisha changanya na mafuta taa, acha ikae kwa siku…
Mitego ya kukamata wadudu wanaoshambulia mimea shambani
Wadudu walio wengi huvutiwa na rangi mbalimbali. Ili kupunguza uharibifu kwenye mazao, wadudu kama nyigu na vidukari wanaweza kudhitiwa kwa kutengeneza chombo kidogo, kipakwe rangi ya njano na kijazwe maji ya sabuni. Wadudu wanaweza kutota kwenye hayo maji na kama wakikusanywa wanaweza kuwa chakula cha samaki au kuku. Mkulima pia anaweza kufanya jaribio la kutumia rangi tofautu tofauti ili kufahamu…
Unafahamu fuko ni mdudu mwenye faida pia?
Mkulima yeyote atawachukia wadudu kutokana na uharibifu wanaosababisha kwenye mazao. Lakini jambo ambalo wakulima wengi hawalijui ni kuwa kuna baadhi ya wadudu na wanyama ambao ni muhimu sana katika shughuli zao za kilimo. Chukulia mfano wa Fuko ambao huwa wanakula baadhi ya wadudu waharibifu na mashimo yao husaidia kupunguza maji yanayozidi shambani. Ili kupunguza uharibifu wao kwa mimea mkulima anaweza…
Zalisha mbolea za asili kwa ajili ya kilimo hai
Ili uweze kufanya kilimo hai ni lazima uwe na mbolea za asili. Bila mbolea za asili huwezi kufanya kilimo cha aina yeyote kwa misingi ya kilimo hai. Mbolea za asili zipo za aina mbalimbali ama huweza kutengenezwa kwa njia mbalimbali na kwa kutumia malighafi mbalimbali kama vile samadi, majani ya kurundika nakadhalika. Baadhi ya mbolea za asili na njia za…








