- Mazingira

Matumizi ya samadi ya wanyama na mimea kwenye kilimo hai

Ubora wa samadi ya wanyama hutegemea zaidi kile kilicholiwa na mnyama. Ikiwa wamelishwa chakula duni au nyasi zilizomea katika udongo usio na rutuba, basi samadi yao pia itakuwa na ubora duni. Ikiwa wanyama wamelishwa chakula kizuri basi samadi pia itakuwa bora na iliyojaa virutubisho. Samadi iliyo tayari kwa matumizi Samadi huhitaji kupevuka kwa majuma au miezi kadhaa kabla ya kuwa…

Soma Zaidi

- Mifugo

Unawezaje kutambua mnyama mwenye afya nzuri na mwenye matatizo ya kiafya?

Afya ya mifugo ni tatizo kubwa linalowakabili wafugaji walio wengi katika sehemu mbalimbali za nchi. Wapo wataalamu mbalimbali katika maeneo na mikoa yote ya nchi wanaotoa huduma ya mifugo lakini, bado kuna changamoto nyingi zinazowakumba wafugaji. Katika sehemu ambazo mawasiliano ikijumuisha pia miundo mbinu kuwa duni, wafugaji wamekuwa wakipoteza mifugo hasa kutokana na sababu kuwa mara ugonjwa unapoikumba inakuwa si…

Soma Zaidi

- Binadamu

Je tunajali lishe bora kwa ajili ya watoto wetu kila siku

Tofauti na ilivyo kwa watu wazima, watoto wanahitaji kupata lishe bora kila siku ili kuweza kujenga miili yao, na kukua katika kiwango kinachotakiwa na hatimae kuwa watu wazima. Ni muhimu kufahamu lishe inayotakiwa kwa watoto. Lishe bora ni nini? Lishe bora ni mlo unaojumuisha uwiano unaotakiwa wa virutubisho vyote muhimu vinavyotakiwa kutoka katika makundi makubwa ya vyakula. Miili yetu huhitaji…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Wakulima wanasemaje kuhusu masoko ya mazao ya kilimo hai

Mkulima anaezalisha kwa mazao kwa kufuata misingi ya kilimo hai, Bw. Zadock Kitomari alisema kuwa, unapoanza kujishughulisha na kilimo hai ambacho hakitumii kemikali unaona kuwa uzalishaji unakuwa mdogo lakini kwa kadri unavyoendelea uzalishaji unakuwa mkubwa. Anaeleza kuwa, kilimo hai ni aina ya kilimo kinachoangalia uhai wa mazingira, uhakika na usalama wa mlaji na usalama wa chakula jambo ambalo linamuhakikishia mkulima…

Soma Zaidi

- Mifugo

Fahamu maandalizi muhimu kabla ya nguruwe kuzaa

Nguruwe wanaozaa kwa mara ya kwanza wanaweza kupelekwa kwenye nyumba ya kuzalia masaa machache kwa siku kutoka siku kumi kabla ya siku ya kuzaa ili waweze kuzoea mazingira. Mara nyingi tumekuwa na makala zinazoelezea ufugaji wa nguruwe katika nyanja tofauti, ikiwa ni pamoja na aina, matunzo na magonjwa ya nguruwe na hata bidhaa zinazotokana na nguruwe na usindikaji wake. Katika…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Vijana wanaweza kujifunza mengi kutokana na ubunifu kwenye kilimo hai

Kilimo hai kinafanyika kwa ufanisi na manufaa endapo wakulima wenyewe wanafanya ubunifu kulingana na mazingira yao. Ili kilimo hai kiwe endelevu ni muhimu ubunifu kutoka kwa vijana kutiliwa mkazo. Kilimo kwa kutumia mifuko (viroba) Kilimo cha kutumia mifuko (viroba), ni kilimo kizuri na chenye manufaa kwa wakulima, kwani unaweza kulima sehemu yeyote pasipo kuathiri mazingira. Watu wengi wanakijua kilimo hiki…

Soma Zaidi

- Mifugo

Shubiri mwitu (aloe) tiba ya magonjwa ya kuku

Kuku ni moja ya miradi inayofanywa kwa wingi na watu wa kada mbalimbali, wakiwamo wakulima na wafugaji, na wanaofanya shughuli nyinginezo. Moja ya changamoto ambazo zimekuwa zikiwakabili na kuzungumziwa mara kwa mara ni magonjwa yanayoshambulia kuku, bila wafugaji kufahamu ni nini cha kufanya. Kumekuwepo na njia mbalimbali za kutibu kuku, zikiwemo za asili na zisizokuwa za asili. Moja wapo ya…

Soma Zaidi

- Mifugo

Nyuki wadogo: Mjasiriamali asiyekuwa na gharama wala madhara

Ninataka kufuga nyuki wadogo, kwa kuwa nasikia wana faida kubwa sana, lakini sijui namna ya kuwapata na jinsi ya kuwatunza, naombeni msaada-Msomaji MkM Nchini Tanzania na maeneo mbalimbali barani Afrika, imekuwa ni mazoea kwa wanaotaka kufanya ufugaji wa nyuki kufuga nyuki wakubwa au maarufu kama nyuki wakali. Aina hii ya nyuki imekuwa ni rahisi kufugwa kwa kuwa uzalishaji wake ni…

Soma Zaidi

- Kilimo

Faida za kufunika udongo katika kilimo

Ni kwa namna gani udongo unaweza kufunikwa wakati wote, wakati shughuli nyingine zinaendelea kwenye udongo huo huo? Hili ni swali muhimu wanalojiuliza wakulima wengi. Hii inategemeana na utunzaji na aina ya shughuli zinazofanyika kwenye udongo huo, na kama shughuli zenyewe zinafanyika kwa kutumia mikono au mashine. Moja ya shughuli ambazo zinasumbua udongo kwa kiasi kikubwa ni kulima kwa kutumia plau.…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Tushirikiane kupata soko la mazao ya kilimo hai

Kwa sasa katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania, ni wazi kuwa shughuli za kilimo hai zimeshika kasi, huku kukiwa na ongezeko la wazalishaji wa bidhaa za kilimo hai. Hili ni jambo jema sana kwa kuwa waswahili wanasema taratibu ndiyo mwendo, na kidogo kidogo hujaza kibaba. Na hapa taratibu tunaona mwanga wa dunia kurudi katika hali yake ya uasili, ya awali…

Soma Zaidi