Uyoga ni moja ya vyakula muhimu katika mwili wa binadamu, vinavyoupa mwili nguvu na virutubisho vya kujenga mwili. Uyoga ni mmea uliopo katika kundi la mimea aina ya fangasi, na umetajwa na wataalamu mbalimbali kuwa na faida kwenye suala la afya kwa binadamu ikiwa ni pamoja na kuondoa seli mfu zilizoko mwilini. Kilimo cha uyoga ni rahisi na unaweza ukavuna…
Mimea
Tumia eneo ndogo kuanzisha bustani ya nyumbani
Bustani ya nyumbani ni eneo lililokaribu na nyumbani au jikoni ambalo linaweza kutumika kwa kulima aina mbalimbali za mboga, matunda na viungo vya chakula. Jinsi ya kuandaa bustani ya gunia Mahitaji muhimu Gunia au mfuko wa salfeti iliotobolewa pande zote Kokoto au mawe madogo Nguzo au ubao wa 4’ kwa 2’ wenye urefu wa mila moja na nusu Mbolea ya…
Viazi vitamu: Hukabili uhaba wa chakula
Viazi vitamu ni moja ya mazao yanayotumika kama kinga ya kukabiliana na uhaba wa chakula kutokana na sifa yake ya kuvumilia ukame kwa muda mrefu. Sehemu kubwa ya zao hili hulimwa kwa matumizi ya nyumbani. Viazi vitamu ni moja kati ya mazao makuu ya mizizi nchini Tanzania. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula. Viazi vitamu, asilia yake ni Amerika ya Kati…
Fahamu namna bora ya upandaji wa zao la vanilla ili kuongeza kipato
Vanilla ni moja ya zao la viungo ambalo hutumika kila siku nyumbani na maeneo mengine. Matumizi makubwa ya zao hili ni kuongeza harufu nzuri na ladha ya vyakula na vinjwaji mbali mbali. Baadhi ya vyakula ambavyo vanilla huwekwa ni pamoja na chokoleti, keki, maandazi, biskuti, uji, barafu pia vinjwaji baridi kama soda na juisi. Mbali na utengenezaji wa vyakula, vanilla…
Unaweza kuokoa pesa nyingi kwa kutumia mwarobaini
Mimi ni msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu, na nimefaidika mengi sana. Ningependa kufahamu kuhusiana na mti wa mwarobaini ambao nimekuwa nikisikia kwa muda mrefu kuwa unatibu wanyama na binadamu. Je naweza kuutumia kutibu kuku na mifugo mingine ninayofuga, na je unafaa kwa mazao?-Msomaji MkM Mwarobaini (Azadirachta indica) ni mti unaofahamika kwa uwezo wake wa kutibu magonjwa ya aina mbalimbali.…
Unaweza kufaidika na kuongeza pato kwa kuzalisha bamia
Bamia ni zao linalolimwa sana nchi za joto. Zao hili hutumika kama mboga inayoliwa matunda. Asili ya mboga hii ni Afrika ya Kati na ya Mashariki, lakini kwa sasa zao hili limeenea katika sehemu nyingi za kitropiki, kama Visiwa vya Caribbean, Malaysia na Philipines. Zipo aina nyingi za bamia, aina zile za kiasili nazo hutofautiana kulingana na eneo moja na…
Wakulima wanasemaje kuhusu masoko ya mazao ya kilimo hai
Mkulima anaezalisha kwa mazao kwa kufuata misingi ya kilimo hai, Bw. Zadock Kitomari alisema kuwa, unapoanza kujishughulisha na kilimo hai ambacho hakitumii kemikali unaona kuwa uzalishaji unakuwa mdogo lakini kwa kadri unavyoendelea uzalishaji unakuwa mkubwa. Anaeleza kuwa, kilimo hai ni aina ya kilimo kinachoangalia uhai wa mazingira, uhakika na usalama wa mlaji na usalama wa chakula jambo ambalo linamuhakikishia mkulima…
Vijana wanaweza kujifunza mengi kutokana na ubunifu kwenye kilimo hai
Kilimo hai kinafanyika kwa ufanisi na manufaa endapo wakulima wenyewe wanafanya ubunifu kulingana na mazingira yao. Ili kilimo hai kiwe endelevu ni muhimu ubunifu kutoka kwa vijana kutiliwa mkazo. Kilimo kwa kutumia mifuko (viroba) Kilimo cha kutumia mifuko (viroba), ni kilimo kizuri na chenye manufaa kwa wakulima, kwani unaweza kulima sehemu yeyote pasipo kuathiri mazingira. Watu wengi wanakijua kilimo hiki…
Tushirikiane kupata soko la mazao ya kilimo hai
Kwa sasa katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania, ni wazi kuwa shughuli za kilimo hai zimeshika kasi, huku kukiwa na ongezeko la wazalishaji wa bidhaa za kilimo hai. Hili ni jambo jema sana kwa kuwa waswahili wanasema taratibu ndiyo mwendo, na kidogo kidogo hujaza kibaba. Na hapa taratibu tunaona mwanga wa dunia kurudi katika hali yake ya uasili, ya awali…
Usindikaji wa ndizi ili kuongeza kipato
Zao la migomba lina asili ya Philipino. Shina la mgomba limeundwa na vikonyo vya majani 12 hadi 30, kila kimoja kikiwa na urefu wa mita 7.6. Vikonyo hivyo pamoja na majani ya migomba hutumika kutengenezea nyuzi. Pamoja na nyuzi, zao kuu linalotokana na migomba ni ndizi, ambazo pamoja na kuwa ni chakula cha binadamu, lakini pia hutumika kwa njia nyinginezo…









