Mkulima Mbunifu imekua ikitembelea wakulima mbali mbali nchini Tanzania ili kuchukua shuhuda mbalimbali za wanufaika na kuzichapisha ziwe chachu kwa wasomaji wengine kujifunza na kufanya kwa vitendo. Je wewe umejifunza nini kutoka Mkulima Mbunifu? Tafadhali tuandikie kupitia mawasiliano yaliyo katika jarida hili. Bwana Santony Yasenti, Nangara – Babati. Ninapenda kutoa shukrani zangu kwa gazeti la Mkulima Mbunifu, nimejifunza mengi kupitia…
Kilimo
Umuhimu wa kulima kiazi sukari (beetroot)
Katika zama za kale, beetroot (kiazi sukari/ bitiruti) ilikuwa ikitumika kama dawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali kama kuvimbiwa, majeraha pamoja na matatizo mbalimbali ya ngozi (mizizi ndiyo iliyokuwa ikitumika). Hadi kufikia karne ya 16 zao hili lilikuwa tayari limekwishapata umaarufu hasa katika Amerika ya Kati na Ulaya ya Mashariki na baadaye kupokelewa katika nchi zingine kama Roma, Ufaransa,…
Dhibiti magonjwa na wadudu kwa kutumia dawa za asili
Madawa ya asili Hizi ni dawa zinazotokana na mimea ambayo hupatikana katika maeneo ya wakulima. Matumizi ya dawa hizi ni njia mojawapo ya kuepuka dawa za viwandani ambazo huathiri udongo, mazingira na afya za watu na wanyama. Hadi sasa kuna dawa takribani 67. Madawa yasipotengenezwa vizuri na kutumiwa ipasavyo yanaweza yasifanye kazi ipasavyo, hivyo huwa ni vigumu kuwashawishi wakulima kuzitumia.…
Namna ya kusindika korosho mara baada ya kuvuna
Korosho ni zao lenye matumizi mengi sana, lakini kubwa kuliko yote ni kwamba kuliwa kama kitafunwa (snacks) wakati wa kunywa chai, juisi, maziwa au kahawa. Makala hii inakusudia kutoa mafunzo ya namna ya kuandaa korosho kwa matumizi ya nyumbani. Hii itawasaidia wakulima wapya wa mikoa hasa iliyoingia kwenye uzalishaji wa zao hili kwa mara ya kwanza. Jinsi ya kuandaa korosho…
Kilimo hai kinachangia uzalishaji katika Kilimo
Tanzania ina ardhi yenye rutuba inayowezesha shughuli za kilimo hai kukua na kuongeza kipato kwa wakulima wadogowadogo. Hii inaweza kufanyika kwa kutumia teknolojia mpya inayoweza kusaidia kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo mbayo yamezalishwa kwa kutumia kilimo hai, kwa ajili ya soko la ndani na la nje. Njia tofauti za kilimo Kwa kawaida viumbe hai wote ni wa asili. Fikra…
Lima Giligilani kukuza uchumi kwa haraka
Kilimo cha Giligilani (Coriander) ni mradi mkubwa unaojitosheleza kukuza maisha ya mkulima kutokana na sababu kuwa zao hili la biashara huchukua muda mfupi toka kuotesha hadi kuvuna. Zao hili linalotumika kama kiungo cha chakula katika mapishi ya vyakula mbalimbali kama nyama, supu au mchuzi linafaa kulimwa wakati wowote na katika maeneo mengi ya Tanzania hususani mikoa ya Mbeya na Iringa.…
Usindikaji wa vitunguu saumu
Kabla ya kusindika vitunguu saumu ni muhimu kuhakikisha kuwa vitunguu vinavyosindikwa vimekomaa vizuri na vipo kwenye kiwango cha ubora na havijaoza. Dalili za vitunguu saumu vilivyokomaa Vitunguu saumu huwa tayari kuvunwa katika kipindi cha miezi mitatu hadi mitano tangu kusia mbegu Vitunguu saumu vilivyokomaa huonyesha majani kunyauka na kubadilika rangi na kuwa ya manjano hadi kahawia. Shingo ya vitunguu saumu…
Ni muhimu kusindika tangawizi ili kuongeza thamani na pato kwa mkulima
Tangawizi ni moja ya mazao ya viungo linalimwa katika mikoa mbalimbali Tanzania kama vile, Tangam Morogoro, Kilimanjaro, Kigoma, Pwani, Iringa, Mbeya na Kagera. Tangawizi ili iweze kusindikwa kwa ajili ya kupata bidhaa mbalimbali, inahitajika kwanza kuhakikisha umezingatia uvunaji sahihi ikiwa ni pamoja na kuvuna mapema ili kuepuka kukomaa zaidi na kuchipua tena pamoja na ufungashaji na uhifadhi uliozingatia ubora. Kuvuna…
Zalisha mbolea za asili kwa ajili ya kilimo hai
Ili uweze kufanya kilimo hai ni lazima uwe na mbolea za asili. Bila mbolea za asili huwezi kufanya kilimo cha aina yeyote kwa misingi ya kilimo hai. Mbolea za asili zipo za aina mbalimbali ama huweza kutengenezwa kwa njia mbalimbali na kwa kutumia malighafi mbalimbali kama vile samadi, majani ya kurundika nakadhalika. Baadhi ya mbolea za asili na njia za…
Unaweza kuuwa wdudu waharibifu kwa kutumia muarobaini
Muarobaini ni moja kati ya miti ya asili, ambayo kwa karne nyingi umekuwa ukitumika kama dawa kwa binadamu, wanyama na mimea. Tunapozungumzia mwarobaini katika kuua wadudu kwenye mazao, tunazungumzia mafuta yaliyomo katika mmea huu. Hii ni dawa ambayo ina uwezo wa kuua wadudu wa aina mbalimbali. Mafuta ya mwarobaini yana dawa inayojulikana kitaalamu kama “AZADIRACHTIN”. Hii ni kemikali isiyo ya…