- Binadamu, Kilimo

Je wajua kuhusu mti wa Mlonge (Moringa)

Sambaza chapisho hili

Moringa (Moringa spp.)  maarufu kama  mlonge  ni  miongoni  mwa  miti  muhimu kwa matumizi ya binadamu, wanyama na hata katika kutengeneza virutubishi kadhaa.

Mti huu  ukuao haraka hupandwa katika maeneo mengi na hutumika kama chakula cha binadamu, lishe ya mifugo, tiba mbadala na kusafisha maji.

Faida na matumizi ya mti wa Moringa

1.Virutubishi

Faida na matumizi ya mti wa MoringaKaribu  kila  sehemu  ya  mti  wa  Moringa  inatumika  au  inalika kama  chakula.

Majani  ndio  sehemu  kuu  ya  mti  wa  Moringa,  unaweza  kuyala  yakiwa  mabichi  au  yakiwa  yamepikwa  kama  mboga  yoyote  ya  majani.

Unaweza  ukayakausha na kuyahifadhi kama unga-unga kwa miezi mingi huku ukitumia kama kiungo kwenye mboga na mchuzi. Pia majani yanaweza kutumika kama lishe bora ya mifugo.

Utafiti wa kisayansi umeonesha kuwa majani ya Moringa ni chanzo kikubwa cha virutubishi.  Virutubishi hivi  ni pamoja na;

Vitamini C – Kirutubishi  hiki ni  muhimu  katika  kutengeneza  kinga  ya  mwili  dhidi ya magonjwa mbalimbali.    Kiwango  chake katika majani ya Moringa ni zaidi ya mara saba ya ile inayopatikana kutoka kwenye machungwa.

Calcium (madini chuma)- Kirutubishi hiki ni muhimu katika kuimarisha pamoja  na  kujenga mifupa  na  meno  mwilini.  Kiwango chake katika majani ya Moringa ni mara nne zaidi ya yale yanayopatikana kutoka kwenye maziwa.

Protini- Kirutubishi  hiki  ni  muhimu  katika  kujenga  mwili  na  kuimarisha  ngozi.  Kiwango  chake  katika  majani  ya  Moringa ni mara mbili zaidi ya ile inayopatikana kutoka kwenye maziwa.

Vitamini  A-  Kirutubishi  hiki  ni  muhimu  katika  kuimarisha  macho  na  kuongeza  uwezo  wa  kuona.    Kiwango  chake  katika majani ya Moringa ni mara nne zaidi ya ile inayopatikana kutoka kwenye Karoti.

Potassium-  Kirutubishi  hiki  ni  muhimu  katika  kujenga  na  kuupatia  mwili  nguvu.  Kiwango  chake  katika  majani  ya  Moringa ni mara tatu zaidi ya ile ipatikanayo kutoka kwenye ndizi.

Maua  ya  Moringa  yamejaliwa  madini  chuma  (calcium)  na  Potassium  kwa  wingi    na    yanaweza  kuchemshwa  au  kupikwa na kuliwa kama mboga.

2.Mboga

Majani  ya  Moringa  huliwa  kama  mboga  nyingine  za  majani  kwa  mfano mchicha.  Majani  yanaweza  kuvunwa  wakati  wa kiangazi ambapo mboga nyingine hazipatikani.

Pia matunda mateke ya Moringa huweza kutumika kama mboga, hutayariswa kama maharage mabichi (machanga).Matunda yalikomaa hutoa mbegu ambazo zinaweza kutumika kama njegere au kukaangwa kama karanga.

3.Mafuta

Mafuta  kutoka  kwenye  mbegu  za  mti  wa  Moringa  huweza  kutumika  katika  kupikia  na  kuwasha  katika  nyumba.  Pia  hutumika  sana  kwenye  viwanda  katika  utengenazaji  wa  sabuni  na  bidhaa  za  urembo.  Mafuta hukamuliwa kutoka kwenye mbegu kama ambavyo alizeti hukamuliwa.

 

 

4.Lishe ya Mifugo

Majani  ya  Moringa  huliwa  na  ng’ombe,    mbuzi,  kondoo,  sungura  na  kuku.  Mbegu  huliwa  na  kuku  pamoja  na  wanyama wengine kwenye jamii ya ndege.

5.Pambo la nyumba

Mti  wa  Moringa  hupandwa  kwa  wingi  kwenye  bustani  kama  ua  au  mti  wa  kivuli na  hutumika  katika  upambaji.  Pia miti ya moringa ikipandwa karibu karibu inaweza kutumika kama fensi.

6.Chanzo cha kipato

Mti  wa  Moringa  ukitumiwa  vizuri  ni  chanzo  kizuri cha  kipato.  Mfano  ni  uuzaji  wa  miche  ya  mti  wa  moringa  na  utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na moringa.

 

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *