- Mifugo

Wanafunzi wa shule ya msingi kioga nao hawako nyuma katika kilimo

Ni miaka tisa sasa tangu kuanzishwa kwa jarida la Mkulima Mbunifu likiwa limejikita katika kutoa elimu kuhusu kilimo, ufugaji, pamoja na kilimobiashara kwa lengo la kusaidia jamii kujikimu kimaisha. Jarida hili, limeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa, katika kufikisha elimu kwa wadau mbalimbali na kuonesha fursa nyingi zilizopo kwenye kilimo na ufugaji hasa katika kilimo hai. Mkulima Mbunifu pia limewafikia wanafunzi…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mifugo

Wanafunzi washirikishwe katika masuala ya kilimo

Shule ya Sekondari Shambalai ‘‘Tuna furaha sana kukutana na Mkulima Mbunifu katika utoaji wa elimu kwani tuna bustani yetu tuliyoianzisha kwa msaada wa mwalimu mkuu, na tumeshindwa kuiendeleza kwa muda mrefu sasa kulingana na kuwa kila tulichokuwa tukijaribu kuotesha tulikosa mavuno lakini jarida hili limetupa nguvu ya kuanza kwa upya.’’ Hayo ni maneno ya mmoja wa wanafunzi wa shule hii…

Soma Zaidi

- Mifugo

Ufugaji wa Sungura: Aina mpya ya ujasiriamali wenye tija kwa mfugaji

Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na unamuda wa kuwahudumia wanyama hawa. Ufugaji wa sungura si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa. Sungura wanahitaji uangalizi hasa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu. Mabanda Kuna aina mbili ya mabanda ya kufugia: • Kwanza ni mabanda ya kufugia ndani muda…

Soma Zaidi

- Kilimo

Wakulima wazidi kutoa shuhuda

Loseriani Sikayoni: “Nimepungunza ujinga kwa kiasi kikubwa baada ya kusoma jarida la Mkulima Mbunifu. Nimejua namna ya kufanya kilimo cha mzunguko, natunza mifugo yangu kisasa, faida ni kubwa.” Ndivyo alivyoanza kusema mzee Loseriani Sikayoni mkulima kutoka kijiji cha Ilkiding’a, mkoa wa Arusha. Kwa miaka mingi, mzee huyu amekuwa akifanya shughuli za kilimo, na maisha yake kwenda vizuri; ikiwa ni pamoja…

Soma Zaidi

- Binadamu

Wakulima Waliotia fora

Augustino Olturia: Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa “Nimefanya shughuli za kilimo na ufugaji toka mwaka 1984. Sikuwa nimefahamu kuwa naweza kuwalisha ng’ombe wangu kwa kipimo na nikapata mafanikio mpaka niliposoma jarida la Mkulima Mbunifu.” Ni maneno ya Mkulima msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu Bw. Agustino Olturia kutoka Kijiji cha Oloigeruno Mkoani Arusha. Bwana Agustiono anasema kuwa jarida la Mkulima…

Soma Zaidi

- Mifugo

Punda anahitaji kutunzwa kama mifugo mingine

Punda ni mnyama anayefugwa na wengi lengo likiwa kutumika kutoa msaada wa nguvu kazi nyumbani hasa kwa kuwa njia nzuri ya kubebea mizigo. Mnyama huyu ambaye hutumiwa hasa na kina mama na watoto wa jamii ya kimasai na nyinginezo kwa ajili ya kubebea maji, kuni, majani, kupelekea mizigo sokoni na shughuli zote zile za nyumbani amekuwa hana thamani kama waliyonayo…

Soma Zaidi

- Kilimo

Maji moto (weaver’s ant) wadudu rafiki wanaowezesha kilimo hai

Maji Moto au Sangara ni aina ya wadudu, ambao ni rafiki kwa mkulima yeyote anayefanya shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya kilimo hai. Ni wadudu wadogo sana ambao huishi katika miti ya mikorosho pamoja na miembe. Mara nyingine hupatikana pia katika pamba. Ikumbukwe kuwa tangu kuumbwa dunia, kila kitu kilikuwa kiasili, watu walikula vyakula na matunda ambayo yalikuwa katika mfumo…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Samadi ya wanyama na mimea

Ubora wa samadi ya wanyama hutegemea zaidi kile kilicholiwa na mnyama. Ikiwa wamelishwa chakula duni au nyasi zilizomea katika udongo usio na rutuba, basi samadi yao pia itakuwa na ubora duni. Ikiwa wanyama wamelishwa chakula kizuri basi samadi pia itakuwa bora na iliyojaa virutubisho. Samadi iliyo tayari kwa matumizi Samadi huhitaji kupevuka kwa majuma au miezi kadhaa kabla ya kuwa…

Soma Zaidi

- Kilimo, Mimea

Mapapai bora hupelekea soko lenye tija

Mapapai ni zao moja kati ya mazao ya matunda yenye vitamin A na madini ya kalsiamu kwa wingi na zao hili hulimwa karibu kila mahali hapa nchini kwa wastani wa tani 2,582 kwa mwaka. Ili kuweza kuzalisha zao la papai kwa wingi na kwa ubora unaotakiwa ni muhimu kuhakikisha unazingatia kanuni zote za kilimo bora za uzalishaji wa mapapai. Ubora…

Soma Zaidi

- Mifugo

Chokaa au majivu huweza kuangamizi kiwavijeshi vamizi

Wakulima walio wengi katika mikoa mbalimbali hapa nchini wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiwavijeshi vamizi, mdudu ambaye husababisha hasara kubwa kwa wakulima hasa wa mahindi kwani hupoteza maelfu ya hekari za mazao endapo watavamiwa na mdudu huyu. Kuna mbinu mbalimbali za kudhibiti mdudu huyu kama vilekufanya kilimo bora mfano kupanda kwa wakati, matumizi ya mbegu kinzani (tolerant/resistant varieties), matumizi ya viumbe…

Soma Zaidi