- Kilimo

Uzalishaji wa zao la maharage kwa tija, kanuni kuzingatiwa

Sambaza chapisho hili

Tukiwa tunaelekea katika msimu wa mvua za vuli, wakulima wengi hupendelea kupanda zao la maharage kwani ni moja kati ya zao kuu nchini Tanzania. Hata hivyo changamoto za uzalishaji wa zao hili hupelekea wakulima kupata mazao hafifu.

Ni ukweli usiopingika zao la maharage ni moja kati ya mazao ya chakula na biashara. Zao hili linazalishwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, kwa misimu tofauti hasa kulingana na mvua pamoja na hali ya hewa ya eneo husika.

Aidha, kabla ya kuzalisha zao hili kwa misingi ya kilimo hai, mkulima hana budi kufahamu kanuni sahihi kwa ajili ya kufanya uzalishaji bora na wenye tija.

Kanuni za kufuata katika uzalishaji maharage

  1. Kuchagua eneo la kupanda maharage:
  • Joto: Kiasi cha nyuzi joto 12 hadi 32. Joto likiwa chini zaidi au juu zaidi linapunguza ukuaji.
  • Mvua: Mvua inayohitajika ni kati ya 400mm hadi 1800mm kwa mwaka zinazonyesha kwa mtawanyiko mzuri.
  • Mwinuko: Panda katika maeneo yenye mwinuko wa mita

400-2000 m kutoka usawa wa bahari.

  1. Mbegu: Uchaguzi wa mbegu sahihi ni muhimu ili kupata mavuno bora. Chagua mbegu zenye soko, mavuno mengi, kinzani/uvumilivu wa magonjwa na wadudu. Mapendekezo ya mbegu yatategemea na ukanda husika.
  2. Vyanzo vya mbegu bora:

Mbegu     bora     zinaweza     kupatikana     kutoka     kwa     wakulima wanaozalisha mbegu.

  1. Sehemu ya kupanda maharage:

Panda sehemu zenye udongo usiotuamisha maji na wenye rutuba kwa kilimo  cha  maharage.    Usipande kwenye  mteremko  mkali, udongo wenye mchanga mwingi na kina kifupi.

  1. Kutayarisha shamba:

Shamba la maharage linatakiwa liandaliwe vizuri kwa kusafisha, na kuvundika majani ili yaoze na kuwa mbolea.

Baada ya hapo katua shamba vizuri na kulainisha udongo ili uotaji wa mbegu uwe rahisi kisha lima sesa au matuta kufuatana na mwinuko wa ardhi au hali ya maji kutuama.

  1. Kupanda kwa wakati: Hali ya hewa wakati wa kupanda ni muhimu ili uotaji kuwa mzuri na kupata mimea yenye afya. Mbegu zipandwe kina cha kutosha kupata unyevu na joto  kwa  mahitaji  ya  kuotesha.  Maharage  ni  vyema kupandwa kwa kutegemea aina ya mbegu na sehemu husika. Pia hakikisha maharage yanakomaa kuelekea kiangazi au mvua zinaposimama.
  2. Matumizi mazuri ya mbolea (Aina za mbolea): Kwa maeneo yenye rutuba hafifu mbolea ni    muhimu    kutumia.    Aina    na    viwango    vya    mbolea vinavyoshauriwa ni pamoja na;
  • Mbolea za asili: Kama mbolea za mifugo au mboji na unashauriwa kusambaza shambani kabla ya kulima. Kiasi: 2000-5000 kilo kwa eka moja.
  1. Upandaji: Panda kwa nafasi zinazoshuriwa sentimita 50 mstari hadi mstari na sentimita 10 mbegu hadi mbegu (50sm x 10sm). Kina cha inchi 1 hadi 1.5 kinafaa. Mimea ya kutosha shambani inapelekea mavuno mengi.
  2. Palizi: Palizi inaweza kufanyika kwa kutumia jembe la mkono. Palizi ifanyike angalau mara 1-2 kwa msimu. Wahi palizi ya kwanza ndani ya wiki mbili hadi tatu baada ya maharage kuota na rudia tena kabla ya kuchanua.
  3. 11. Wadudu na   magonjwa:   Funza   wa   maharage   ni   wadudu wanaoshambulia   mimea   michanga   ya      Funza   hawa huweza kusababisha  uharibifu  hadi  kufikia  asilima  100  kufuatana na   hali   ya   hewa au unyevu   kidogo,   rutuba   kidogo,   kuwepo   kwa maotea ya aina ya maharage na magogwa kwenye udongo, kurudia kupanda   zao   la   maharage   kila   msimu   na   aina   ya   maharage.

Magonjwa mengine maarufu kama ndui ya maharage, madoa pembe, kutu, magonjwa yanayo  sababishwa  na   bakteria   na   virusi.

Punguza  athari  kwa  kupanda  mbegu  safi,  aina zinazo  vumilia magonjwa   na  kutunza  shamba

Mbinu za kudhibiti magonjwa na wadudu waharibifu wa maharagwe

Njia moja au zaidi kati ya hizi zinaweza kutumika kama kinga:

  • Matumizi ya mbegu zenye
  • Matumizi sahihi  ya  mbolea ya asili;  mbolea  huimarisha  afya  ya  mimea hivyo    kuiwezesha    kuvumilia    na    kupambana    na    madhara yatokanayo na magonjwa na wadudu
  • Kupanda kwenye    matuta    au    mashamba    yalioinuliwa    ili kupunguza  kutuama  kwa  maji  lakini  pia  kusaidia  kurutubisha udongo kwenye sehemu zenye muinuko na mvua
  • Kupandishia udongo kuzunguka mashina kabla ya maua husaidia mmea kuotesha  mizizi  bandia  kwenye  mimea  iliyoshambuliwa na Rizoktonia, Fusariam na Funza wa
  • Kufukia chini  kabisa  mabaki  ya  mimea  iliyoshambuliwa  wakati wa kuandaa
  • Kuacha mabaki   ya   mazao   yaliyopita   kuoza   kabisa   kabla   ya kupanda mazao
  • Kufanya kilimo  cha  mzunguko  wa  mazao  ya  jamii  tofauti  kama nafaka kila baada ya miaka miwili au

Makala hii imeandaliwa kwa msaada wa maandiko yaliyochapishwa kutoka chuo cha ARI Uyole Mbeya. Wasiliana na Mkulima Mbunifu kwa maelekezo zaidi

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *