Ninataka kufuga nyuki wadogo, kwa kuwa nasikia wana faida kubwa sana, lakini sijui namna ya kuwapata na jinsi ya kuwatunza, naombeni msaada-Msomaji MkM Nchini Tanzania na maeneo mbalimbali barani Afrika, imekuwa ni mazoea kwa wanaotaka kufanya ufugaji wa nyuki kufuga nyuki wakubwa au maarufu kama nyuki wakali. Aina hii ya nyuki imekuwa ni rahisi kufugwa kwa kuwa uzalishaji wake ni…
Mifugo
Ufugaji mseto wa samaki na mazao mengine
Katika ufugaji mseto wa samaki na mazao mengine mambo kadha wa kadha ni muhimu sana kuzingatiwa ikiwa ni pamoja na kujua aina ya samaki wanaofaa kufugwa, faida za mboga na hata mifugo mingine kama kuku wanaojumuishwa katika ufugaji huu. Aina ya samaki wanaofaa katika kilimo mseto Perege na Kambale ni samaki wanaofugwa katika maeneo mabalimbali nchini Tanzania. Perege ndiyo aina…
Tumia dawa za asili zinazopatikana katika maeneo ya wafugaji kutibu magonjwa mbalimbali ya mifugo
Yapo magonjwa mbalimbali ambayo mfugaji hasa aliyeko kijijini anaweza kuyatibu kwa kutumia dawa za asili ambazo pia zainapatikana katika maeneo yao bila hata kutumia dawa za madukani. Faida ya kutumia dawa hizi ni kubwa kwani husaidia kuokoa maisha ya mfugo kwa haraka zaidi kama huduma ya madaktari iko mbali, hupunguza gharama za kununua dawa pamoja na kumlipa afisa mifugo. Mimea…
Uandaaji na uoteshaji wenye tija wa miche ya vanila
Vanila ni zao la biashara ambalo asili yake ni mexico zao hili limekua likilimwa na kuzalishwa huko mexico, marekani na bara Hindi kwa karne nyingine. Hivi sasa, zao hili linalimwa maeneo mengi barani Afrika ikiwamo nchi ya Tanzania, japo kwa uchache kutokana na ugumu wake wa kulizalisha, ingawa bei yake ni kubwa sana na wakulima waliofanikiwa kuzalisha wamekuwa wakipata kipato…
Gliricidia: Mti wenye faida lukuki kwa mkulima
Gliricidia ni mti ambao kisayansi hujulikana kwa jina la gliricidia sepium ambao hutumika kwa ajili ya mbolea au kurutubisha ardhi. Mti huu wa gliricidia ni jamii ya miti ya malisho ambayo majani yake hutumika kurutubisha udongo na kulishia mifugo hasa katika kipindi cha ukame. Hii ni kutokana na uwezo wake wa kumudu kuzalisha wakati wa kiangazi pamoja na kudumisha hali…
JAGEF wanaonesha njia katika usindikaji wa vyakula
“Kukaa mwenyewe na kufanya shughuli za ujasiriamali ni rahisi sana kuanguka, kutokutambuliwa au kuweza kupiga hatu, lakini mkiwa kwenye kikundi, mnapiga hatua kwa haraka sana na wepesi zaidi” Ndivyo alivyoanza kueleza mama Ester Moshi, mwenyekiti wa kikundi cha wasindikaji cha JAGEF katika kijiji cha Kikarara Old Moshi mkoani Kilimanjaro alipokuwa akielezea shughuli za kikundi hicho. JAGEF kilianza mwaka 2010 kikiwa…
Mayai yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu
Wakulima wanaowekeza kwenye mradi wa kuku, hupata hasara pale ambapo hawatunzi mayai ipasavyo. Mayai ni bidhaa hafifu na inayoharibika kwa haraka, hivyo, ni lazima ishikwe kwa uangalifu na kutunzwa vizuri baada ya kutagwa ili yasivunjike au kuharibika. Watu wengi wanaonunua mayai kutoka dukani watatambua mara moja kuwa mayai hayo yamevunjika au yameoza. Tatizo hili linaweza kutokana na utunzaji na uhifadhi…
Wanafunzi wa shule ya msingi kioga nao hawako nyuma katika kilimo
Ni miaka tisa sasa tangu kuanzishwa kwa jarida la Mkulima Mbunifu likiwa limejikita katika kutoa elimu kuhusu kilimo, ufugaji, pamoja na kilimobiashara kwa lengo la kusaidia jamii kujikimu kimaisha. Jarida hili, limeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa, katika kufikisha elimu kwa wadau mbalimbali na kuonesha fursa nyingi zilizopo kwenye kilimo na ufugaji hasa katika kilimo hai. Mkulima Mbunifu pia limewafikia wanafunzi…
Wanafunzi washirikishwe katika masuala ya kilimo
Shule ya Sekondari Shambalai ‘‘Tuna furaha sana kukutana na Mkulima Mbunifu katika utoaji wa elimu kwani tuna bustani yetu tuliyoianzisha kwa msaada wa mwalimu mkuu, na tumeshindwa kuiendeleza kwa muda mrefu sasa kulingana na kuwa kila tulichokuwa tukijaribu kuotesha tulikosa mavuno lakini jarida hili limetupa nguvu ya kuanza kwa upya.’’ Hayo ni maneno ya mmoja wa wanafunzi wa shule hii…
Ufugaji wa Sungura: Aina mpya ya ujasiriamali wenye tija kwa mfugaji
Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na unamuda wa kuwahudumia wanyama hawa. Ufugaji wa sungura si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa. Sungura wanahitaji uangalizi hasa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu. Mabanda Kuna aina mbili ya mabanda ya kufugia: • Kwanza ni mabanda ya kufugia ndani muda…