Mifugo

- Binadamu, Kuku, Mifugo

Tumia mayai ya kuku kuimarisha afya ya mama na mtoto

Mayai nichanzo kizuri cha protini ambayo ni muhimu kwa kujenga tishu za mwili. Mayai yana vitamini na madini kadhaa, ikiwa ni pamoja na choline, ambayo ni nzuri kwa ukuaji wa ubongo wa mtoto. Pamoja na faida za kula mayai, usile mayai mabichi au ambayo hayajapikwa yakaiva vizuri. Ikiwa lengo kubwa la kilimo na ufugaji ni kuhakikisha usalama wa chakula kwa…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara, Kuku, Kutuhusu, Masoko, Mazingira, Mifugo, Udongo, Usindikaji

NANE NANE 2022, UNAKOSAJE MAONYESHO HAYA, MKULIMA MBUNIFU KAMA KAWAIDA YETU TUTAKUWEPO KUKUJUZA KUHUSU KILIMO NA UFUGAJI

Hayawi hayawi sasa yamekuwa, nane nane hiyoo imekaribia. Nchini Tanzania, kila mwaka, wakulima na wafugaji hujumuika kwa pamoja kwa muda wa siku takribani kumi kuadhimisha sikukuu ya wakulima nchini. Sherehe hizi hufikia kilele siku ya tarehe nane mwezi wa nane. Katika kipindi hiki wadau mbalimbali wa kilimo, huandaa mazao na bidhaa mbalimbali za kilimo kwa ajili kushirikisha bunifu mbalimbali na…

Soma Zaidi

- Mifugo

Fahamu kuhusu homa ya nguruwe na namna ya kudhibiti

Homa ya nguruwe ni ugonjwa hatari wa nguruwe unaosababishwa na virusi aina ya African Swine Fever vinavyoshambulia na kuharibu mfumo wa damu. Virusi vinavyosababisha homa ya nguruwe haviambukizi binadamu. Virusi vinavyosababisha homa ya nguruwe huishi kwenye miili ya ngiri bila kusababisha ugonjwa Kupe laini walioko katika mashimo wanamoishi ngiri, hupata virusi vya homa ya nguruwe wanaponyonya damu kutoka kwa ngiri…

Soma Zaidi

- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara, Kutuhusu, Mazingira, Mifugo

Maswali toka kwa wasomaji wa Mkulima Mbunifu kwa njia ya simu

Ndugu msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu, ni furaha yetu kuwa umeendelea kufuatilia na kusoma makala mbalimbali zinazochapishwa kwenye jarida hili. Pia tunashukuru wewe uliefatilia na kutaka kufahamu kwa undani kwa kuuliza maswali pale ambapo hujaelewa ama umekwama. Pia tunashukuru kwa mchango wako katika kutekeleza kilimo hai. Katika makala hii ni baadhi tu ya maswali yaliyoulizwa na wakulima wasomaji wa…

Soma Zaidi

- Binadamu, Mifugo

Unaweza kuokoa pesa nyingi kwa kutumia mwarobaini 

Mimi ni msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu, na nimefaidika mengi sana. Ningependa kufahamu kuhusiana na mti wa mwarobaini ambao nimekuwa nikisikia kwa muda mrefu kuwa unatibu wanyama na binadamu. Je naweza kuutumia kutibu kuku na mifugo mingine ninayofuga, na je unafaa kwa mazao? Msomaji MkM Mwarobaini () ni mti unaofahamika kwa uwezo wake wa kutibu magonjwa ya aina mbalimbali.…

Soma Zaidi

- Mifugo

Njia bora ya kugawanya makundi ya nyuki wadogo

Nyuki wasiong’ata maarufu kama nyuki wadogo hufikia kiwango cha kuwa kundi kubwa lenye kuhitaji kuendelezwa kutoka katika mzinga mama na kuelekea katika mzinga mpya. Zoezi la kugawanya makundi ya nyuki huhitaji utalaamu na uangalifu wa kutosha ili kusaidia ugawanyaji wa kundi kuwa wenye tija kwa mfugaji. Kuna faida kubwa ya kugawanya makundi ya nyuki wasiong’ata Huongeza idadi ya nyuki katika…

Soma Zaidi

- Mifugo

Tumia mpungate/kakati kutibu ugonjwa wa ndigana baridi

Ng’ombe wangu anapata choo kigumu sana na mara nyingine, kinaambatana na ute kama makamasi na damu, huu ni ugonjwa gani, na nasikia kuna dawa za kienyeji zinazotibu! Ni dawa gani, na inaandaliwaje? Kuna uwezekano mkubwa kuwa ng’ombe wako anasumbuliwa na ugonjwa unaojulikana kama ndigana baridi au kitaalamu Anaplasmosis. Huu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria ambapo mnyama hujisaidia kinyesi kilichochanganyikana na…

Soma Zaidi

- Mifugo

Kuroila: Kuku wa ajabu wenye faida kubwa

Kuroila wanaweza kufugwa ndani na kulishwa katika banda au kuachiwa huru kujitafutia. Wanaweza kulishwa kwa kutumia mabaki ya vyakula au vyakula maalumu. Kuroila ni aina ya kuku wa kienyeji ambao wanakuwa kwa haraka sana na hutaga mayai mengi zaidi ukilinganisha na aina nyingine ya kuku, wawe wa kienyeji au wa kisasa. Kwa nchi za ukanda wa Afrika ya Mashariki, kuku…

Soma Zaidi