Ufugaji wa kuku ni moja ya sekta ambayo imekuwa na faida kwa wafugaji walio wengi, na hata watu ambao wanafanya shughuli nyinginezo, lakini bado hujishughulisha na ufugaji wa kuku. Pamoja na aina hii ya ufugaji kuwa na mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea wafugaji kipato kikubwa, bado inakumbwa na changamoto mbalimbali. Mojawapo ya changamoto hizo ni pamoja na uwepo…
Mifugo
Zingatia kanuni za kilimo hai katika shamba la kuku ili kuzalisha chakula salama
Kuna njia kadhaa za kuongeza idadi ya kuku kama vile kununua kuku wakubwa, kununua vifaranga kutoka kwa wafugaji wengine, kuzalisha vifaranga kutokana na kuku waliokomaa au kutotoa kwa kutumia mashine ya inkubeta. Mbinu inategemea uwezo na uzoefu wa mfugaji. Kila mfugaji angependa kupanua kiasi ya ufugaji wa kuku na kujiongezea kipato. kutokana na mauzo ya kuku au mayai. Kufuga kuku…
Yafahamu magonjwa ya mimea ili kuyadhibiti
Mkakati mzuri kwa wakulima wanaozingatia ikolojia ni kujifunza na kuelewa sababu ya magonjwa, athari zake ili kuweza kukabiliana nayo. Hii inasaidia kulinda mazao ya mimea, kudumisha usalama wa uzalishaji wa chakula. Kwa kawaida, ni ngumu kuzuia ama kurekebisha tatizo ikiwa haujaelewa tatizo lenyewe. Ndio maana wakulima wanashauriwa kuwa makini shamba-ni kutambua kwa haraka uvamizi wa wadudu na pia magonjwa. Maana…
Mifugo wadogo wanachangia pato kwa haraka
Mifugo wanachangia maisha ya kaya, maisha ya vijijini na uchumi wa nchi. Ni chanzo cha mapato na ajira kwa wazalishaji na wengine wanaofanya kazi katika minyororo ya thamani. Ufugaji wa mifugo hawa wadogo unahitaji mtaji mdogo kuanzisha, kudumisha, kupanua na wanahitaji eneo ndogo ya kufugia. Na katika nyakati hizi ambapo kuna mfumuko wa bei ya bidhaa unaosababisha gharama ya maisha…
Ushuhuda kutoka kwa msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu
Kama ilivyo ada, Mkulima Mbunifu tumeendelea kuwatembelea wakulima na wanufaika wa jarida hili kufahamu ni kwa namna gani elimu wanayoipata kupitia makala za kila mwezi zimeendelea kuleta chachu katika shughuli zao za kilimo na hata kuweza kuwabadilisha kimaisha. Bi. Esther Kitomari ni miongoni mwa wanufaika wa jarida la MkM na anaeleza kuwa amejifunza mengi kupitia makala zinazochapishwa kila mwezi hasa…
Tumia mayai ya kuku kuimarisha afya ya mama na mtoto
Mayai nichanzo kizuri cha protini ambayo ni muhimu kwa kujenga tishu za mwili. Mayai yana vitamini na madini kadhaa, ikiwa ni pamoja na choline, ambayo ni nzuri kwa ukuaji wa ubongo wa mtoto. Pamoja na faida za kula mayai, usile mayai mabichi au ambayo hayajapikwa yakaiva vizuri. Ikiwa lengo kubwa la kilimo na ufugaji ni kuhakikisha usalama wa chakula kwa…
NANE NANE 2022, UNAKOSAJE MAONYESHO HAYA, MKULIMA MBUNIFU KAMA KAWAIDA YETU TUTAKUWEPO KUKUJUZA KUHUSU KILIMO NA UFUGAJI
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, nane nane hiyoo imekaribia. Nchini Tanzania, kila mwaka, wakulima na wafugaji hujumuika kwa pamoja kwa muda wa siku takribani kumi kuadhimisha sikukuu ya wakulima nchini. Sherehe hizi hufikia kilele siku ya tarehe nane mwezi wa nane. Katika kipindi hiki wadau mbalimbali wa kilimo, huandaa mazao na bidhaa mbalimbali za kilimo kwa ajili kushirikisha bunifu mbalimbali na…
Fahamu kuhusu homa ya nguruwe na namna ya kudhibiti
Homa ya nguruwe ni ugonjwa hatari wa nguruwe unaosababishwa na virusi aina ya African Swine Fever vinavyoshambulia na kuharibu mfumo wa damu. Virusi vinavyosababisha homa ya nguruwe haviambukizi binadamu. Virusi vinavyosababisha homa ya nguruwe huishi kwenye miili ya ngiri bila kusababisha ugonjwa Kupe laini walioko katika mashimo wanamoishi ngiri, hupata virusi vya homa ya nguruwe wanaponyonya damu kutoka kwa ngiri…
Makosa wanayofanya wafugaji wa nyuki wadogo na jinsi ya kukabiliana nayo
Nyuki ni wadudu wadogo lakini ni wadudu wenye uwezo wa kutengeneza mazao ya chakula na biashara kama asali na nta. Ufugaji wa nyuki pamoja na kumpatia mfugaji pato lakini pia nyuki husaidia katika kuhifadhi mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi. Baadhi ya wafugaji wa nyuki huwa na matamanio ya kupata faida kubwa kutokana na kazi hii lakini…
Maswali toka kwa wasomaji wa Mkulima Mbunifu kwa njia ya simu
Ndugu msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu, ni furaha yetu kuwa umeendelea kufuatilia na kusoma makala mbalimbali zinazochapishwa kwenye jarida hili. Pia tunashukuru wewe uliefatilia na kutaka kufahamu kwa undani kwa kuuliza maswali pale ambapo hujaelewa ama umekwama. Pia tunashukuru kwa mchango wako katika kutekeleza kilimo hai. Katika makala hii ni baadhi tu ya maswali yaliyoulizwa na wakulima wasomaji wa…