Mahindi ni zao muhimu la chakula, na ni aina ya nafaka inayotumiwa kwa wingi kama chakula, hususani katika mataifa ya Afrika, lakini pia limekuwa likitumika katika nchi zilizopo kusini mwa jangwa la sahara. Mahindi ni chakula cha matumizi ya nyumbani kwa idadi ya watu inayokadiriwa kuwa asilimia 50. Ni chanzo muhimu cha madini cha kuongeza nguvu mwilini, protini, madini ya…
Kilimo
Matumizi ya mabaki ya mimea na wanyama katika kurutubisha udongo na kupelekea uzalishaji bora wa mazao
Je, unafahamu kuwa unatakiwa kujua sifa za udongo ulio katika shamba lako na changamoto zake? Je, udongo una upungufu wa naitrojeni? Je, una upungufu wa fosiforasi? Je, kuna uwepo wa mabaki ya miti au wanyama ya kutosha? Ikiwezekana, udongo huo upimwe na mtaalamu au afisa kilimo ili kuonyesha kwa usahihi udongo una mapungufu ya virutubishi vipi na nini kifanyike ili…
Rutuba ya udongo ndiyo msingi wa kilimo hai
Kwa muda mrefu sasa tumekuwa mstari wa mbele katika kuzungumzia na kuhimiza uzalishaji kwa misingi ya kilimo hai, ikiwa ni moja ya nguzo za kilimo endelevu. Katika makala zote zilizochapishwa katika jarida hili pamoja na machapisho mengine yanayotolewa na Mkulima Mbunifu, tumehimiza pia matumizi sahihi ya dawa za asili na mbolea za asili. Hii inatokana na ukweli kwamba, huwezi kusema…
Mnyororo wa ongezeko la thamani utapunguza manung’uniko kwa wakulima na wafugaji
Sera ya soko huria iliyoanza kutekelezwa toka miaka ya 1990 imefungua fursa kwa wawekezaji kuwekeza kwa wingi kwenye maeneo mbali mbali ya kibiashara. Kwa muda mrefu, Kilimo kimewavuta wawekezaji ambao wamekuwa wakijishughulisha na mashamba makubwa ili kukidhi madhumuni ya biashara ya kuzalisha kwa wingi kupunguza gharama ya kuzalisha kwa kiasi kidogo. Pamoja na kutekelezwa kwa makubaliano baina ya wawekezaji na…
Msomaji wa jarida la MkM atoa ushauri kwa wafugaji wa kuku
Moja ya kazi inayofanywa na Mkulima Mbunifu katika kufikisha elimu kwa wakulima, ni kutumia ujuzi na uzoefu wa wakulima na wafugajhi wengine katika kuelimisha na kushirikisha namna mbalimbali wanavyofanya na kufanikiwa katika kazi zao za uzalishaji. MkM Huu ni ushauri kutoka kwa mmoja wa wasomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu kwa wafugaji wa kuku. “Naitwa Nicodemus Nzenga, ni mmoja kati…
Zingatia afya ya mmea ili kupata mapato mengi
Mara nyingi wakulima wanapuuza maswala yanayohusiana na nafya ya mimea na kupata hasara kubwa. Ikiwa mkulima hatawekeza muda na rasilimali, atakuwa na mimea iliyodhoofika. Ni nia ya kila mkulima kuwa na mimea yenye nguvu na afya, na yenye uwezo wa kutoa mapato ya hali ya juu. Ni lazima kuwa makini na kuzingatia mbinu zitakazowezesha kufikia lengo hili. Hivyo, swala zima…
Vuruga biocide: Kiuatilifu cha asili sasa chapatikana kwa ruzuku
Hayawi hayawi sasa yamekua. Mvumilivu, hula mbivu. Ni muda wakulima wa kilimo hai wamekua wakilalamika upatikanaji wa bidhaa za kilimo hai kwa urahisi. Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya kilimo imepitisha kiuatilifu hai kwa jina la Vuruga. Kiuatilifu hai (VURUGA BIOCIDE) kimetengenezwa kwa vimelea asili vya fangas (A. oryzae) kwa ajili ya kudhibiti visumbufu vya mazao shambani hasa jamii ya…
Jarida la MkM limetupa hamasa ya kutekeleza shughuli zetu za uzalishaji
Kuna msemo aliowahi kuutoa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa; “Elimu sio njia ya kuepuka umasikini bali ni njia ya kupigana na umasikini”. Msemo huu wameudhihirisha wazi na kwa vitendo wakulima wajasiriamali wa kikundi cha kusindika kitarasa ambao wametumia elimu inayotolewa na jarida la Mkulima Mbunifu kupiga vita umaskini na kufanikiwa. Kikundi hiki kinachofanya shughuli mbalimbali za uzalishaji kama vile kilimo…
Utengenezaji wa kiuatilifu cha asili
Kama ilivyo ada wakulima wa kilimo hai, huitaji malighafi asili ili kuzalisha mazao salama na yenye ubora shambani. Si haba, malighafi hizi zinapatikana katika maeneo yetu ya kila siku. Jiulize, Je kwa nini uingie gharama mara mbili ilhali unaweza kutatua changamoto ya wadudu kwa kutumia viuatilifu asili. Katika makala hii Mkulima Mbunifu inakuangazia, jinsi ya kutengeneza kiuatilifu cha kiasili kinachotokana…
Vitamini na madini muhimu ya kujenga kinga ya mwili
Vitamini na madini yanafanya kazi ya kujenga kinga ya mwili, na yanapatikana katika mboga na matunda. Ni muhimu kwa makundi ya watu kama watoto, mama wajamzito, mama anaenyonyesha na wazee, kwani huzuia na kusaidia kupambana na maambukizi ya magonjwa. Watu wengi hawali chakula cha kutosha chenye mboga na matunda, pamoja na vyakula vingine ambavyo ni vyanzo vya vitamini na madini.…