Kudondoka kwa maua kwenye miembe yako inaweza kutokana na upungufu au ukosefu wa aina fulani ya madini. Virutubisho na madini kwenye miembe vinahitaji ufahamu na uelewa wa hali ya juu kwa kile kinachohitajika. Tofauti na hilo, unahitaji kuzingatia kiasi cha fosiforasi ili kuchochea uwezo wa mizizi na ukuaji wa mmea. Mkulima anatakiwa kuweka utaratibu wa kuweka mbolea kwenye mimea yake…
Kilimo
Lishe na vyanzo asili ya chakula
Lishe bora inajumuisha aina mbalimbali za vyakula kutoka makundi tofauti ya chakula, na hutoa virutubisho na ladha tofauti. Makundi haya ni muhimu kwa afya na ukuaji wa mwili: Nafaka na mizizi: Mahindi, viazi, ndizi — hutoa wanga kwa ajili ya kuongeza nguvu. Mikunde: Maharagwe, soya — chanzo cha protini kwa ajili ya kujenga mwili. Karanga na mbegu: Njugu, korosho —…
Mifano ya ujumuishaji yanayotumiwa na wakulima
1. Mifumo Mseto Wakulima wanalima mazao makuu pamoja na kufuga ng’ombe, wakitumia mabaki ya mazao kulisha ng’ombe na samadi kurutubisha mashamba. 2. Kilimo cha mzunguko na malisho ya muda Mzunguko wa mazao na malisho ya muda mfupi ambayo huliwa na mifugo. Awamu ya malisho inaboresha rutuba ya udongo kwa mazao yanayofuata, na mifugo hunufaika na malisho. 3. Malisho kwenye bustani…
Je, wajua kuwa unaweza kufanya ufugaji mesto wa Samaki, kuku na mboga katika eneo dogo, kwa gharama nafuu na kipato kikubwa?
Ufugaji wa samaki umeendelea kukua hata katika maeneo ambayo hakuna ziwa, bahari, bwana na kusaidia jamii kujipatia kipato kinachokidhi mahitaji muhimu, na hata kufanya maendeleo binafsi. Mafanikio ya ufugaji wa Samaki ni kutokana na uhakika mkubwa wa soko. Katika Makala hii Mkulima Mbunifu inakuletea Ufugaji mesto wa Kuku, Samaki na uzalishaji wa mboga katika mbinu rahisi. Ufugaji wa mesto ni…
Je, wajua kuwa unaweza kulima mboga kwenye matairi na ukafanikiwa?
Hupunguza uchafuzi wa mazingira Kila siku watumiaji wa vyombo vya usafiri hubadilisha matairi. Mbali na kuwa matairi hutumika kutengeneza vitu kama viatu, mipini ya mapanga n.k, pia matairi yanaweza kutumiwa katika kilimo cha mbogamboga na matunda badala ya kuchoma matairi na kuzalisha kemikali zenye sumu kwa binadamu. Ni rahisi kutumia Ukilinganisha na kulima kwa kutengeneza matuta ya mbao au mawe,…
MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE; TUAMBIE UMEJIFUNZA NINI? JE, UNAKWAMA WAPI?
Kama umeweza kuhudhuria maonyesho ya wakulima Nanenane katika kanda yeyote, njoo utuambie ni kipi umejifunza kipya, au ni maarifa ama ujuzi gani umeongeza? Je, ni wapi unakwama au changamoto uliyonayo ni ipi? Njoo tusemezane ewe mkulima!!!!!!!!!!!!!
Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai
Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo. Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja…
Ukizingatia kanuni hizi utafanikiwa kuwa na uzalishaji bora wa mazao
Usafishaji wa shamba. Shamba likiwa safi unapunguza sehemu ambazo wadudu wanaweza kuzaliana kwa urahisi, pamoja na sehemu ambazo vitu vinavyosababisha magonjwa vinaweza kujificha. Mkulima anashauriwa kupalilia shamba lake mara kwa mara na kila inapowezekana kuhakikisha anaondoa masalia ya mazao ya msimu uliopita shambani. Masalia hayo yakibaki shambani wadudu wa magonjwa ya mazao hayo vitaendelea kuwepo na kuzidi kuzaliana. Kilimo…
Kusindika maparachichi kupata guacamole
Maparachichi ni moja ya zao la matunda ambalo hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Kilimanjaro, Morogoro, Kigoma, Kagera, Arusha na Tanga. Zao hili ni muhimu sana katika lishe kwani lina mafuta na protini kwa wingi kuliko matunda yote yanayolimwa nchini. Kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji kila wakati, ambapo mara nyingine husababisha kushuka kwa bei ya matunda haya sokoni, ni…
HIVI UKISIKIA WAKULIMA WAKISEMA MBEGU UNAFIKIRIJE? AMA KWA UFAHAMU WAKO MBEGU NI NINI
Mbegu ni nini? Mbegu ni sehemu ya mmea ambayo ina uwezo wa kuota na kutoa mmea mpya. Kuna makundi makuu mawili ya mbegu tunayoyazungumzia katika kilimo ambayo ni punje na shina/ mizizi. Punje Hizi ni mbegu za nafaka au za matunda, ambazo huzalishwa kwa uchavushaji. Kawaida huwa na kiini na chakula chake huhifadhiwa ndani ya ganda gumu la mbegu. Mfano,…








