Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo. Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja…
Kilimo
Ukizingatia kanuni hizi utafanikiwa kuwa na uzalishaji bora wa mazao
Usafishaji wa shamba. Shamba likiwa safi unapunguza sehemu ambazo wadudu wanaweza kuzaliana kwa urahisi, pamoja na sehemu ambazo vitu vinavyosababisha magonjwa vinaweza kujificha. Mkulima anashauriwa kupalilia shamba lake mara kwa mara na kila inapowezekana kuhakikisha anaondoa masalia ya mazao ya msimu uliopita shambani. Masalia hayo yakibaki shambani wadudu wa magonjwa ya mazao hayo vitaendelea kuwepo na kuzidi kuzaliana. Kilimo…
Kusindika maparachichi kupata guacamole
Maparachichi ni moja ya zao la matunda ambalo hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Kilimanjaro, Morogoro, Kigoma, Kagera, Arusha na Tanga. Zao hili ni muhimu sana katika lishe kwani lina mafuta na protini kwa wingi kuliko matunda yote yanayolimwa nchini. Kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji kila wakati, ambapo mara nyingine husababisha kushuka kwa bei ya matunda haya sokoni, ni…
HIVI UKISIKIA WAKULIMA WAKISEMA MBEGU UNAFIKIRIJE? AMA KWA UFAHAMU WAKO MBEGU NI NINI
Mbegu ni nini? Mbegu ni sehemu ya mmea ambayo ina uwezo wa kuota na kutoa mmea mpya. Kuna makundi makuu mawili ya mbegu tunayoyazungumzia katika kilimo ambayo ni punje na shina/ mizizi. Punje Hizi ni mbegu za nafaka au za matunda, ambazo huzalishwa kwa uchavushaji. Kawaida huwa na kiini na chakula chake huhifadhiwa ndani ya ganda gumu la mbegu. Mfano,…
MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE, EWE MKULIMA, MFUGAJI NA MJASIRIAMALI VIPI UMEJIANDAAJE?
“Hayawi hayawi sasa yamekuwa”. Kama ilivyo ada mwezi wa nane, huwa ni mwezi wenye shughuli nyingi zinazohusiana na kilimo, ufugaji, uvuvi wasindikaji na hata kilimo biashara tangu mwanzoni kabisa mwa mwezi hadi katikati ya mwezi. Wakulima, wafugaji na wadau wengine hupata fursa ya kukutana katika maeneo mbalilmbali ili kuonesha kazi zao pamoja na kushirikishana uzoefu katika suala zima la kilimo…
Wakulima vinara wa MkM ni mabalozi wa kilimo endelevu
Nchini Tanzania, kilimo si kazi tu, ni sehemu ya maisha ya kila siku. Kilimo kinatoa ajira kwa takribani asilimia 80 ya Watanzania na kuchangia takribani asilimia 30 ya pato la taifa. Kiasi kikubwa cha chakula chetu kinazalishwa na wakulima wadogo. Hata hivyo, licha ya mchango wao mkubwa, wakulima hawa hukumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na udongo kupoteza rutuba,…
Ni vyema ukapunguza matumizi ya kemikali shambani mwako
Wakulima wengi hutumia dawa za kemikali kudhibiti magonjwa na wadudu waharibifu shambani. Hata hivyo, tatizo moja kubwa la kutumia dawa za kudhibiti wadudu na magonjwa kwa kiasi kikubwa ni kuwa wadudu hao huwa sugu baada ya muda mfupi. Hii inapelekea wakulima wengine kubuni njia hatari za kudhibiti wadudu na magonjwa. Baadhi yao hutumia dawa ya kuulia kupe kwa ajili ya…
Mbinu za uzalishaji bora shambani
Usafi shambani Ni vyema kuhakikisha kwamba shamba ni safi, haina magugu ambayo yanaweza kushindana na mimea kupata lishe na maji. Inashauriwa kufanya palizi ya mara kwa mara. Pia, Panda mimea ya msimu ikifuatana na mimea ya msimu mfupi. Kwa, mfano, baada ya kupanda mahindi, unaweza kupanda viazi vitamu ambavyo vitasaidia kufunika udongo na kuhakisha upotevu mdogo wa maji. Tumia wadudu…
Zingatia afya ya mmea ili kupata mapato mengi
Mara nyingi wakulima wanapuuza maswala yanayohusiana na nafya ya mimea na kupata hasara kubwa. Ikiwa mkulima hatawekeza muda na rasilimali, atakuwa na mimea iliyodhoofika. Ni nia ya kila mkulima kuwa na mimea yenye nguvu na afya, na yenye uwezo wa kutoa mapato ya hali ya juu. Ni lazima kuwa makini na kuzingatia mbinu zitakazowezesha kufikia lengo hili. Hivyo, swala zima…
Unaweza kutengeneza mbolea ya mboji kwa njia rahisi
Zipo aina nyingi za takataka zin-azoweza kutumika kwa ajili ya kuzalisha mbolea ya mboji kama vile mabaki ya malisho, unga wa maranda unaotokana na shughuli za useremala, majivu na masalia ya ziada baada ya kuvuna mazao shambani. Kwa kutengeneza mboji, kiasi cha mbolea kitakachopelekwa shambani kitaongezeka kwani samadi itachanganywa na takataka zingine na kuozeshwa. Ni jambo zuri zaidi kama mkulima…






