Binadamu

- Binadamu

Zingatia usalama wa chakula kipindi hiki cha ugonjwa wa COVID-19

Janga la Covid-19 linachangia changamoto ya usalama wa chakula na lishe bora duniani. Kuwepo na mfumo endelevu wa chakula na mahali panapoweza kuhakikisha usambazaji wa chakula bora katika nyakati kama hizi, ni fursa ambazo miji michache ulimwenguni zinafurahia.  Nchi nyingi na mashirika yanaongeza jitihada za kufanya kilimo salama, ili kupambana na changamoto za usalama wa chakula, ambao unaweza kusababisha janga…

Soma Zaidi

- Binadamu

Lishe bora ni muhimu kwako na kwa familia yako

Kuna uhusiano mkubwa kati ya kile tunachokula, hali ya afya yetu na uwezo wa miili yetu kupambana na magonjwa na vimelea vinavyosababisha magonjwa. Chakula bora kwa afya zetu na watu wanaotuzunguka ni muhimu kwa ajili ya kuendelea kuzalisha mali na kujenga jamii iliyo bora. Kuwa na afya njema, inatukumbusha wazalishaji wa mazao ya kilimo juu ya aina ya chakula tunachozalisha…

Soma Zaidi

- Binadamu

Ni muhimu kuwa kwenye vikundi ili kupata maendeleo thabiti

Mara nyingi nimesikia na kuona MkM Mkisisitiza wakulima na wafugaji kujiunga kwenye vikundi, je kuna umuhimu gani, na ni hatua zipi za kisheria tunazopaswa kufuata ili vikundi vyetu vitambuliwe na kuwa rasmi?-Bakari Buhari, Msomaji MkM Handeni. Kikundi ni muunganiko wa watu wenye nia/lengo moja katika kutekeleza jambo fulani walilolikusudia kwa faida ya hao walioamua kuwa pamoja.  Lengo kuu la kuwa…

Soma Zaidi

- Binadamu

Je tunajali lishe bora kwa ajili ya watoto wetu kila siku

Tofauti na ilivyo kwa watu wazima, watoto wanahitaji kupata lishe bora kila siku ili kuweza kujenga miili yao, na kukua katika kiwango kinachotakiwa na hatimae kuwa watu wazima. Ni muhimu kufahamu lishe inayotakiwa kwa watoto. Lishe bora ni nini? Lishe bora ni mlo unaojumuisha uwiano unaotakiwa wa virutubisho vyote muhimu vinavyotakiwa kutoka katika makundi makubwa ya vyakula. Miili yetu huhitaji…

Soma Zaidi

- Binadamu, Mazingira

Madhara ya kiafya kutokana na viuatilifu

Wakulima wengi wamejisababishia madhara ya kiafya kutokana na matumizi ya viuatilifu. Hii ni kutokana na kutokua na maarifa sahihi na kutokutumia hatua zinazostahili za kinga au kutekeleza mbinu sahihi za udhibiti. Viuatilifu vya kiwandani na zana zake kwa kawaida huhifadhiwa majumbani ambako kuna hatari ya kugusana na chakula na watoto. Pia mazao yaliyopuliziwa dawa wakati mwingine huvunwa bila ya kuzingatia…

Soma Zaidi

- Binadamu

Wakulima Waliotia fora

Augustino Olturia: Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa “Nimefanya shughuli za kilimo na ufugaji toka mwaka 1984. Sikuwa nimefahamu kuwa naweza kuwalisha ng’ombe wangu kwa kipimo na nikapata mafanikio mpaka niliposoma jarida la Mkulima Mbunifu.” Ni maneno ya Mkulima msomaji wa jarida la Mkulima Mbunifu Bw. Agustino Olturia kutoka Kijiji cha Oloigeruno Mkoani Arusha. Bwana Agustiono anasema kuwa jarida la Mkulima…

Soma Zaidi

- Binadamu, Mimea

Tumia mazao funikizi kwa chakula na kulisha mifugo

Mazao funikizi siyo mageni sana kwa wakulima walio wengi isipokuwa kwa wale ambao ndio kwanza wanaanza kujiingiza katika kilimo hifadhi. Si mazao yote funikizi yanayoweza kutumika kulishia mifugo moja kwa moja mara baada ya kuvuna kutoka shambani. Mengine ni lazima yafanyiwe maandalizi fulani ndipo yatumike kulishia. Mazao funikizi kama vile, canavalia yanahitajika kukaushwa kwanza na kuandaliwa vyema kabla ya kulisha…

Soma Zaidi