- Binadamu

Imarisha afya ya mifupa kwa kuzalisha bidhaa mbalimbali za kilimo hai

Sambaza chapisho hili

Mifupa yetu inarekebishwa kila wakati na tishu za mfupa zinavunjwa na kujengwa mara kwa mara. Uzani wa mfupa kawaida huongezeka hadi wakati wa utu uzima, lakini baada ya hapo, shida inaweza kukupata.

Mifupa huupa mwili mwonekano sahihi, hulinda viungo vya ndani ya mwili (mfano Fuvu linalinda ubongo na kifua na mbavu zinalinda mapafu), hukusaidia kutembea, hutunza madini muhimu ya mwili (mfano phosphorus). Mifupa huzalisha seli za damu, hutunza nishati ya mwili kwa njia ya mafuta na nyinginezo nyingi.

Mwili una kawaida ya kuzalisha seli mpya kila wakati na kuondoa zilizozeeka. Katika umri wa utoto na umri wa ujana, mwili huongeza kutengeneza mifupa mipya kwa haraka na kuondoa ya zamani kwa taratibu sana.

Baada ya miaka 20 mwili huanza kupoteza mifupa mingi kwa haraka kuliko mifupa mipya inayotengenezwa. Kwa hiyo unaweza kuona jinsi ilivyo muhimu kudumisha afya ya mifupa.

Katika makala hii Mkulima Mbunifu inaangazia madini mbalimbali na virutubisho vinavyotokana na mazao yaliozalishwa kwa usahihi. Hapa tutaorodhesha baadhi ya bidhaa zenye virutubisho vinavyohitajika kwa mwili wa binadamu.

Kalishamu: Bidhaa za maziwa ni moja wapo ya vyanzo vya kawaida vya kalishamu, lakini watu wengi huchagua kutokula au hawawezi kuvumilia kwa sababu ya kuwa na mzio (allergy).

Vyanzo vingine vya kalishamu vinavyotokana na vyakula ni pamoja na mboga za kijani kibichi (kama vile broccoli, juisi zilizo na kalishamu, maziwa ya soya nakadhalika.

Vitamini D: Vitamini D ina jukumu muhimu katika kuruhusu mwili kunyonya kalishamu. Tunapata vitamini D kutoka kwenye jua na vyakula kama vile maziwa ya soya, kiini cha yai, ini la ng’ombe, juisi ya machungwa na hata samaki wenye mafuta.

Magnesiamu: Magnesiamu na kalishamu hufanya kazi pamoja kukuza afya ya mfupa. Vyakula vyenye magnesia nyingi ni pamoja na nafaka isiyokobolewa, mchicha, tofu, mlozi, broccoli, dengu na mbegu za alizeti.

Vitamin K: Wanawake wanaotumia vitamini ‘K’ kidogo wana hatari kubwa ya kuvunjika kwa nyonga. Upungufu wa Vitamini ‘K’ unaathiri usawa wa kalishamu, madini muhimu katika metaboliki ya mfupa.

Foods rich in vitamin K. Top view; Shutterstock ID 1388788013; Purchase Order: -; Segment/Job: -; Client/Licensee: –

Vitamini ‘K’ haiwezi tu kuongeza uwiano (density) ya mfupa kwa watu walio na ugonjwa wa mifupa, lakini pia kupunguza viwango vya kuvunjika. Chanzo bora ni mboga za kijani kibichi, kama mchicha na broccoli.

Boron: Boron, kawaida huainishwa kama madini ya athari. Imetambuliwa hivi karibuni kama virutubisho muhimu katika afya ya mfupa kwa sababu hupunguza utokaji wa mkojo wa kalsiamu na magnesiamu. Boron inaweza kupatikana kwenye nyanya, tufaha, soya, zabibu kavu, karanga, mlozi, tende na asali.

Vyakula vya kuzuia ili kupunguzwa uharibifu wa mifupa

Unywaji wa pombe kupita kiasi: Watu wanaokunywa pombe kupita kiasi wanakabiliwa na tatizo hili. Hii inaweza kusababisha upotezaji wa kalishamu kupitia mkojo. Pombe pia inaweza kupunguza unyonyaji wa kalsiamu katika utumbo na kusababisha upungufu wa vitamini D na magnesiamu ambazo zote ni muhimu kwa afya ya mfupa. Kwa kuongezea, wale wanaokunywa pombe kupita kiasi mara nyingi huchagua pombe kuliko vyakula vyenye lishe na hii ni hatari zaidi.

Matumizi makubwa ya sodiamu: Tafiti kadhaa zimeonesha athari ya sodiamu katika lishe. Kupunguza ulaji wa sodiamu kunaweza kupunguza upotezaji wa mifupa. Epuka vyakula vyenye chumvi na vyakula vya kukaanga. Vyanzo vya sodiam kwenye chakula ni pamoja na chumvi ya kupikia nyumbani.

Kafeini: Unywaji wa vikombe zaidi ya viwili vya kahawa kwa siku inaweza kuchangia upotezaji wa mifupa.

Matumizi ya kiasi kikubwa cha protini ya wanyama: Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa lishe iliyo na protini nyingi za wanyama, ambayo hutoa asidi, kweli inaongeza upotevu wa mfupa kwa kutenganisha kalishamu kutoka kwenye mifupa.

Tunajifunza nini hapa

Kwanza kabisa ni muhimu mkulima na msomaji kuzingatia lishe bora, kwamba unapozalisha bidhaa shambani tambua unapata madini ya aina gani katika zao hilo.

Kumekua na mazoea ya watu wengi kutumia aina moja tu ya chakula na kutozingatia vyakula vingine kwa kuona kwamba vinawafaa watu wa hali fulani tu. Kinga ya mwili inajengwa kwa lishe ya chakula.

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *