“Hayawi hayawi sasa yamekuwa”. Kama ilivyo ada mwezi wa nane, huwa ni mwezi wenye shughuli nyingi zinazohusiana na kilimo, ufugaji, uvuvi wasindikaji na hata kilimo biashara tangu mwanzoni kabisa mwa mwezi hadi katikati ya mwezi. Wakulima, wafugaji na wadau wengine hupata fursa ya kukutana katika maeneo mbalilmbali ili kuonesha kazi zao pamoja na kushirikishana uzoefu katika suala zima la kilimo…
Kilimo
Wakulima vinara wa MkM ni mabalozi wa kilimo endelevu
Nchini Tanzania, kilimo si kazi tu, ni sehemu ya maisha ya kila siku. Kilimo kinatoa ajira kwa takribani asilimia 80 ya Watanzania na kuchangia takribani asilimia 30 ya pato la taifa. Kiasi kikubwa cha chakula chetu kinazalishwa na wakulima wadogo. Hata hivyo, licha ya mchango wao mkubwa, wakulima hawa hukumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na udongo kupoteza rutuba,…
Ni vyema ukapunguza matumizi ya kemikali shambani mwako
Wakulima wengi hutumia dawa za kemikali kudhibiti magonjwa na wadudu waharibifu shambani. Hata hivyo, tatizo moja kubwa la kutumia dawa za kudhibiti wadudu na magonjwa kwa kiasi kikubwa ni kuwa wadudu hao huwa sugu baada ya muda mfupi. Hii inapelekea wakulima wengine kubuni njia hatari za kudhibiti wadudu na magonjwa. Baadhi yao hutumia dawa ya kuulia kupe kwa ajili ya…
Mbinu za uzalishaji bora shambani
Usafi shambani Ni vyema kuhakikisha kwamba shamba ni safi, haina magugu ambayo yanaweza kushindana na mimea kupata lishe na maji. Inashauriwa kufanya palizi ya mara kwa mara. Pia, Panda mimea ya msimu ikifuatana na mimea ya msimu mfupi. Kwa, mfano, baada ya kupanda mahindi, unaweza kupanda viazi vitamu ambavyo vitasaidia kufunika udongo na kuhakisha upotevu mdogo wa maji. Tumia wadudu…
Zingatia afya ya mmea ili kupata mapato mengi
Mara nyingi wakulima wanapuuza maswala yanayohusiana na nafya ya mimea na kupata hasara kubwa. Ikiwa mkulima hatawekeza muda na rasilimali, atakuwa na mimea iliyodhoofika. Ni nia ya kila mkulima kuwa na mimea yenye nguvu na afya, na yenye uwezo wa kutoa mapato ya hali ya juu. Ni lazima kuwa makini na kuzingatia mbinu zitakazowezesha kufikia lengo hili. Hivyo, swala zima…
Unaweza kutengeneza mbolea ya mboji kwa njia rahisi
Zipo aina nyingi za takataka zin-azoweza kutumika kwa ajili ya kuzalisha mbolea ya mboji kama vile mabaki ya malisho, unga wa maranda unaotokana na shughuli za useremala, majivu na masalia ya ziada baada ya kuvuna mazao shambani. Kwa kutengeneza mboji, kiasi cha mbolea kitakachopelekwa shambani kitaongezeka kwani samadi itachanganywa na takataka zingine na kuozeshwa. Ni jambo zuri zaidi kama mkulima…
Unaweza kukausha karoti na kusaga kwa matumizi ya baadaye
Imezoeleka kuwa karoti ni moja ya kiungo maarufu cha chakula, ambacho mara nyingi kinatumika kikiwa kibichi, na mara nyingi hakihifadhiwi kwa muda mrefu. Tofauti na dhana hii, karoti inaweza kusagwa na kuwa unga, ambao unaweza pia kutumika kama chakula. Utayarishaji Osha karoti kwa kutumia maji ya moto hadi zitakate. Katakata vipande vidogo vidogo. Kausha kwenye kikaushio cha sola ili kulinda…
Fahamu madhara ya kiafya unayoweza kupata kutokana na viuatilifu
Wakulima wengi wamejisababishia madhara ya kiafya kutokana na matumizi ya viuatilifu. Hii ni kutokana na kutokua na maarifa sahihi na kutokutumia hatua zinazostahili za kinga au kutekeleza mbinu sahihi za udhibiti. Viuatilifu vya kiwandani na zana zake kwa kawaida huhifadhiwa majumbani ambako kuna hatari ya kugusana na chakula na watoto. Pia mazao yaliyopuliziwa dawa wakati mwingine huvunwa bila ya kuzingatia muda…
Unaweza kutumia chokaa na majivu kuangamiza viwavijeshi vamizi
Wakulima walio wengi katika mikoa mbalimbali hapa nchini wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiwavijeshi vamizi, mdudu ambaye husababisha hasara kubwa kwa wakulima hasa wa mahindi kwani hupoteza maelfu ya hekari za mazao endapo watavamiwa na mdudu huyu. Kuna mbinu mbalimbali za kudhibiti mdudu huyu kama vilekufanya kilimo bora mfano kupanda kwa wakati, matumizi ya mbegu kinzani (tolerant/resistant varieties), matumizi ya viumbe…
Tengeneza unga wa mbegu za parachichi na tumia kwa afya
Unga wa mbegu za parachichi Parachichi ni moja ya matunda maarufu duniani kote. Tunda hili hutumika kwa shughuli mbalimbali, kama vile kuliwa kama tunda, utengenezaji wa mafuta ya kula, vipodozi, n.k. Pia, matawi ya mparachichi yanaweza kutumika kama malisho kwa mifugo, huku mti wake ukitumika kama kuni au hata magogo ya kujengea. Hivi karibuni imegundulika kuwa mbegu za parachichi zina…








