- Kilimo

Fahamu dawa za asili kudhibiti magonjwa na wadudu katika kilimo ikolojia

Sambaza chapisho hili

Dawa ya kufukuza wadudu

Dawa hii hutumika kudhibiti wadudu kama nzi weupe katika mipapai, nyanya, tikiti, vitunguu, mboga-mboga na matunda.

Mahitaji muhimu

  1. Mchele kilo 1
  2. Maji lita 1
  3. Chombo cha ujazo wa lita 2.

Jinsi yakutengeneza

Changanya mchele na maji katika chombo kisafi chenye mfuniko wakubana. Vundika kwa siku saba, baada siku saba itakuwa tayari kwa matumizi.

Matumizi

Chukua kiasi cha mils 30mls changanya na maji lita 1 kisha puliza katika mimea yako iliyoadhirika na wadudu Hawa weupe.

NEMSOL -3

Kudhibiti vimamba, ubwiri wa juu na wachini katika mazao ya mboga-mboga, matunda na nafaka.

Mahitaji muhimu

  1. sabuni ya maji mils 10s
  2. Mafuta ya mwarobaini mils 10
  3. Bicarbonate gramu 10

Jinsi yakutengeneza

Changanya malighafi zote hapo juu katika lita moja ya maji na Kisha kuipuliza katika majani yaliyoadhirika. Puliza sehemu za chini na juu ya majani.

Matumizi

Chukua mils 10 na changanya na maji lita 1 kisha puliza kwenye mimea

NEEMSOL-6

Dawa hii limepewa hilo jina kwakuwa Ina viambata vya asili aina sita. Hii kirahisi kukumbusha mahitaji muhimu wakati wakuandaa dawa hii kwakutumia vipimo maalum. Hudhibiti magonjwa na wadudu karibu katika mimea yote kwakuwa ina wigo Mpana. Vimamba, utitiri mwekundu, utitiri mweupe, utando wa buibui, viwavi (caterpillars), ubwiri wa juu, ubwiri wa chini, mnyauko n.k

Mahitaji muhimu

  • Ndulele gramu 100
  • Majani ya mwarobaini gramu 100
  • Mapapai gramu 100
  • Sabuni yam aji mils 100
  • Pilipili kali gramu 50
  • Bicarbonate paketi moja yenye ujazo wa gramu 70
  • Maji lita 20

Jinsi yakutengeneza

Twanga- malighafi ngumu katika kinu chako kisha changanya na malighafi laini kwa muda wa masaa 24 Kisha chuja kwa kitambaa safi. Chuja mara mbili hadi tatu.

Matumizi

Chukua mchanganyiko wote katika Lita 20 Kisha puliza kwenye mimea yenye mwezi mmoja au zaidi

Mkojo wa sungura (rabbit urine.

Jinsi yakutengeneza

Vundika mkojo kwa siku saba katika chombo kisafi kisichopitisha hewa au mfuniko wakubana.

Matumizi

Tumia lita 1.5 changanya na lita 15 za maji kisha puliza katika mimea yako kufukuza wadudu. Dawa hii pia wakati huo huo huongeza kiwango ha nitrojeni katika mimea yako.

Mkojo wa sungura

Hutumika Kama dawa yakufukuzia wadudu pia kuongeza nitrojeni katika mmea kwa njia yakuchachusha kwakutumia mollasI

Mahitaji muhimu

  • Lita za mkojo 5
  • Mollasi Lita 5

Jinsi yakutengeneza

Vundika kwa siku 14. Katika chombo kisichoruhusu hewa kuingia au kutoka.

Matumizi

Tumia 1.5L katika 15 za maji. Dawa hii hukaa bila kuharibika kwa miezi 6

KILUMAGIO

Hii Ni dawa inayodhibiti viwavi jeshi vamizi katika mimea jamii ya nafaka. Kama mahindi, mtama n.k

Mahitaji muhimu

  • Spidex mils 55
  • Sukari kilo 1
  • Unga wa mahindi kilo 5
  • Maji lita 1

Jinsi yakutengeneza

Changanya malighafi malaini kwanza pembeni Kisha changanya katika malighafi malaini kwa mkono. Hakikisha umevaa gloves wakati unaifanya hii zoezi. Changanya hadi malighafi yote yatakapochanganyika vizuri. Kisha hifadhi sehemu Safi katika mfuko.

Matumizi

Weka kidogo kwakudondosha vipunje vidogo vya dawa katika sehemu ya katikati ya mmea. Anza kuweka baada ya siku 10 hadi 15 toka umepanda mahindi Kisha rudia kila baada ya siku 14. Hukaa mwezi mmoja ikiwa imehifadhiwa (sealed)

Vimi-fly

Hii dawa inatumika kudhibiti utitiri mweupe nzi weupe katika nyanya, papai, tikiti na mazao ya mboga mboga

Mahitaji muhimu

  • Lita 25 za maji
  • Kilo moja ya unga wa ngano
  • Lita tatu na robo ya maziwa
  • Siki [vinegar] vijiko viwili vya chai

Jinsi yakutengeneza

Chukua vinegar nyeupe Kisha weka katika kikombe kimoja Cha maziwa. Chukua unga wa ngano kilo moja kicha changanya katika maji Lita 20. Changanya malighafi yote kwa pamoja kisha koroga kwa dakika mbili.

Matumizi

Chuja Mchanganyiko wote kwa kitambaa safi Kisha gawa katika solo yako kwa ajili ya matumizi shambani.

Dawa ya kufukuza wadudu (repellents)

Dawa hii nikwaajili yakufukuza wadudu shambani.

Mahitaji muhimu

  • Saumu gramu 10
  • Pilipili kali gramu 10
  • Sabuni ya maji lita 1/majani ya mpapai
  • Maji lita 1.

Jinsi yakutengeneza

Twanga- malighafi magumu pamoja kisha changanya na malighafi malaini. Kisha chuja kwakutumia kitambaa safi.

Matumizi

Chukua mchanganyiko wote katika Lita moja ya maji Kisha puliza kwenye mimea yako kufukuza wadudu. Inashauriwa kupuliza kabla wadudu hawajaingia shambani.

EM5

Hawa ni vimelea wa tija (beneficial microbes). Dawa hii hutumika katika kuondoa vimelea wabaya wanaosababisha magonjwa katika mimea nakuongeza vimelea wazuri katika mimea na udongo

Mahitaji muhimu

  • Majani ya mwarobaini gramu 200
  • Maua ya bangi pori gramu 100
  • Pilipili kali gramu 50
  • EMAS mils 200
  • Siki [vinegar] mils200
  • Spirit/konyagi mils 200
  • Maji lita 1.2

Jinsi yakutengeneza

Twanga malighafi magumu katika chombo moja Kisha changanya na malighafi malaini Kisha weka katika ndoo yenye mfuniko wakubana vizuri kwa siku 14. Kisha itakuwa imeiva. Chuja mchanganyiko wako vizuri tayari kwa matumizi.

Matumizi

Chukua mils 10 ya Em5 katika lita 1 ya maji. Kisha changanya na puliza kuondoa vimelea wabaya na kuongeza vimelea wazuri kwenye udongo.

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *