- Binadamu, Kilimo, Kilimo Biashara

Mazao ya chakula na lishe kamili ni muhimu kwa mkulima

Sambaza chapisho hili

MkM kwenye mtandao wafugaji kwa miaka kadhaa wamekuwa wakifuga kimazoea, bila kuzingatia kwa kiasi kikubwa uzalishaji wenye tija.

Hali hiyo imekuwa ikisababisha kiasi Tanzania ni nchi yenye uwezo wa kuzalisha mazao mengi ya chakula na ya biashara. Hii ni kutokana na hali ya hewa nzuri pamoja na udongo wenye rutuba ya asili unaowezesha mazao hayo kukua na kufanya vizuri katika uzalishaji.

Pamoja na hayo, wakulima wengi wakubwa na wadogo wamekuwa wakijikita katika kuzalisha mazao fulani tu mara kwa mara, lengo kubwa likiwa ni kulenga soko. Si vibaya kufanya hivyo lakini ni vyema tukatambua kuwa hatuna budi kujikita katika uzalishaji wa aina mbalimbali ya mazao ya chakula kwa ajili ya kujenga na kulinda afya za wakulima wenyewe pamoja na walaji.

Mara kwa mara watu wengi hasa watoto wadogo wamekuwa wakipoteza maisha na wengine kudhoofika kiafya na kudumaa kutokana na kukosekana kwa lishe bora. Hii yote hutokana na kula vyakula vya aina moja kila wakati hasa vyakula vya wanga kwa wingi na ambavyo havina virutubisho kamili vinavyohitajika mwilini.

Orodha ya mazao na viini lishe vyake

Mazao Viini lishe muhimu

Mtama: fosforasi, chuma, magnesiamu

Mihogo: wanga, vitamini C, nyuzinyuzi

Mahindi ya asili: antioxidants, vitamini B, zinc, nyuzinyuzi

Kunde: folate, chuma, zinki

Choroko: protini, vitamini B9, nyuzinyuzi

Maharagwe ya asili: chuma, protini, folate, potasiamu

Mehe (Mahindi): mafuta ya asili, chuma, protini

Njugu karanga: protini, vitamini E

Alizeti: mafuta yenye afya, vitamini E, selenium

Maboga: vitamini A, C, zinki, nyuzinyuzi

Viazi vitamu: beta-carotene, vitamini C, nyuzinyuzi

Kisamvu: vitamini A, C, kalsiamu

Mlenda: vitamini K, C, chuma

Mnavu: chuma, vitamini A, kalsiamu

Majani ya maboga: vitamini C, chuma

Karoti: beta-carotene, vitamini A

Ndizi mbichi: potasiamu, wanga, vitamini B6

Tende: sukari ya asili, nyuzinyuzi, potasiamu

Embe la asili: vitamini C, A, nyuzinyuzi

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *