- Kilimo

Tumbaku kwenye mbogamboga

Sambaza chapisho hili

Tumbaku ni dawa ya asili inayoweza kutumika katika kilimo cha mbogamboga

  • Tumia ugoro au chemsha miche 20 ya tumbaku.
  • Dawa hii inazuia wadudu wanaoshambulia mahindi shambani, wadudu wanaokata miche, kupe, vidukari, viwavi na wengine.
  • Chukua gramu 500 za tumbaku, changanya maji lita nane na uchemshe. Chuja baada ya kupoa, ongeza maji lita nane tena na gramu 60 za sabuni ili kuongeza ubora.
  • Ni muhimu kuwa na tahadhari kwa kuwa tumbaku ni sumu kwa binadamu na wanyama, hivyo weka mbali na wanyama wafugwao.

Inashauriwa kuvuna mazao siku 4-5 baada ya kunyunyiza aina hii ya dawa.

Maoni kupitia Facebook
Sambaza chapisho hili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *